Nimekutana na mwanamke wa ajabu, naanza kuingiwa na hofu walimwengu nisaidieni

Nimekutana na mwanamke wa ajabu, naanza kuingiwa na hofu walimwengu nisaidieni

Nafikir ww unaweza kunielewa Ni kitu gani nazungumzia Ni wiki mbili tu, ila mambo ninayo kutana nayo...sijapata kuona maishani mwangu

Sent using Jamii Forums mobile app
Yep hayo kama ni Mazur kula maisha acha woga umependwa na mtoto wa kitajiri. Kula mzigo fasta zari hilo la. Mentali lisije hamia kwangu ila.mi nmeoa labda atakua mkw mdogo

(Pambana na hali yako) ..# Kwetu Mwanza Nyegezi#
 
Dah maisha mwanzoni yalikuwa km kawaida tu lkn baadae nikaanza kuporomoka kiuchumi,nikayumba sn then unabanwa kila kona unakosa kibali kwa kila mtu si ndugu,jamaa wala rafiki. Unakosa wa kukusapot then anakuchonganisha nao wote unabaki km bundi yaani ni balaa mwanzo mwisho.

Sent using Jamii Forums mobile app
ungeweka full mkasa ingependeza mkuu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Inawezeakana zimwi lenyewe limefungua ID humu linasoma tu komenti haha. Inawezekana hicho kidada kinachojifanya jini ni wale waganga matapeli anakuvuruga halafu baadae mwenzake anatokea akupe tiba ya majini.

On a serious note nenda kawaone viongozi wa kiroho. Tatizo lako inawezekana ni kubwa sisi tunafanya utani hapa
 
SEHEMU YA TATU: Nimekutana na mwanamke wa ajabu naanza kuingiwa na hofu walimwengu naomba mnisaidie.

Baada ya sms ile ya tigo pesa...nikajaribu kupiga ile namba iliyotuma pesa simu haikupokelewa. Mwishoni nikaamua kuacha nayo. Nikaona mambo yanazidi kuniwia magumu, nikaona kabisa Tatizo linaenda kuwa kubwa, ikabidi nichukue simu nimpigie mama yangu, nikamuelezea ilivyokuwa kuanzia mwanzo wa tukio mpk hatua tuliyofikia, kiukweli mama yangu aliogopa sana, ingawaje hakuonesha wazi zaidi ya kunitia Moyo na kuniasa nimuombe Mungu bila kuchoka lkn pia, nitafute mtumishi wa Mungu anifanyie maombi maalum.
Ila nilimuonya sana mama yangu, asije akamshirikisha hiyo ishu mtu yoyote mpk nitakapo mpa ruksa ya kufanya hvy, kwa 7bu anaweza ndio Akawa anaongeza Tatizo na sio kulipunguza.

Mama alinielewa, ila akanishauri si vyema kuendelea kukaa dukani kwa kipindi kile yanaweza kunikuta makubwa zaidi ya Yale. Siku hiyo ilikuwa ijumaa nilimpigia simu mdogo wangu anaeishi maeneo ya kigambon aje kunishikia Kuna dharula nimepata, Mara nyingi anakuwaga yy kipindi mm sipo nimetoka kwa mambo yangu mengine. Mpk kufikia mida ya saa 10 jion alikuwa ameshafika nikamkabidhi duka na kurudi zangu nyumban. Sikuwa na furaha siku Hy, nilikuwa nawaza mambo mengi nisiyokuwa na majibu nayo, nikiwa kwenye gari mdogo wangu akanipigia simu kuwa Kuna mgeni wangu pale dukani, nikamuuliza Ni wa kike au wa kiume, akanijibu ni wakike, nikastuka! Nikamuuliza amesema anashida gani, akasema amekuja kuchukua mzigo wake alikuachia ww Jana...akasema umtunzie atakuja kupitia.

Hapo ndio nikachanganyikiwa kabisa, inawezekanaje. Huyu dada atakuwa anataka nini. Niliishiwa pozi, nikakataa simu, baada ya muda kidogo simu ikaita Tena ila sikupokea. Ikumbukwe nguo anazohitaji ndio nimezivaa wakat huo, na niyeye ndie aliesema ameninunulia iweje aje na kuzidai Tena, ina maana Hawa Ni watu tofauti? Je huyu anae nipigia simu Ni Nan? Na maswala ya nguo kayafahamu vp! Nilibaki na mshangao, nikiwa kwenye dimbwi zito la mawazo, sms ikaingia kwenye simu yangu, kuisoma nakuta imeandikwa .." Nakupenda ila usisubutu kuniepuka, Kama unampenda mama yako, fwata nitakacho kwambia, kesho njoo feri saa 7 mchana upande wa kigamboni ukiwa umeziweka hizo nguo kwenye mfuko, uje kunikabidhi nimpelekee niliemkusudia.
Baada ya ujumbe huo, nikastuka sana hapo hapo nikampigia simu mama, nikamuuliza uko salama? Akasema ndio...akaniuliza Kuna nini, nikamjibu hakuna kitu, najua mama yangu anapresha pia ananipenda sana, hapendi kusikia nateseka...ila nikaendelea kumsisitiza juu ya Jambo nililomwambia kuhusu huyo mwanamke anayenifatilia asisubutu kumwambia mtu yoyote. Hii siku niliumia sana...tuwapende sana mama zetu mama alilia sana, akaniambia mwanangu kuwa makini wanataka kukuuwa, nikawa namwambia asijali hawawez niua, naamini Mungu yuko nami. Sikutaka kuendelea kusikia mama yangu akiangua kilio kwa ajili yangu. Niliwaza mambo mengi sana siku Hy, ki ukweli ilikuwa Ni siku mbaya kwangu. Nikamtumia sms mdogo wangu nikamwambia mwambie huyo dada aondoke nitawasiliana nae...akanijibu ameshaondoka muda mrefu amesema atakutafuta kwenye simu nikamjibu poa.

Nilifika nyumbani, nikaingia bafuni kaoga..nilivyorudi nikawa nimejilaza kitandani...nikapitiwa na usingiz mzito sana..nikiwa usingizini nikaota tupo kwenye ile ile bustani ya Jana tuliyokuwa tunalazimishana kuoga, Ila wakat huu haikuwa, hivyo wote tulikuwa tumevaa nguo nyeupe, mm nilivaa mavazi Fulani hv meupe mfano wa kaunda suit na yeye alikuwa amevaa Yale mavazi Kama ya kihindi ila nimeupe kabisa, tulikuwa tunakula na kunywa, yalikuwa ni matunda ndizi, apples, zabibu na vitu Fulani hv mfano wa tende ila ile juice ilikuwa Ni nyekundu Kama mvinyo hvy...

Tukawa tunacheka na kufurah sana, akaniambia Fulani....(Akataja jina langu) akasema Nilikuwa nakupenda kitambo...ila Fulani (Akataja jina la x girlfriend wangu) tuliekuwa tumeachana Kama miez nane iliyopita, kwamba yule ndie aliekuwa akiniekea vikwazo..nikamuuliza kwa nini, akasema alikiwa mtu wa dini sana, (Ni Kweli nikipata mdada alikuwa mlokole na mtu wa maombi sana yeye na kanisa kila wakati) hukumbuki hata sababu ya kuachana kwenu ilikuwa ni pombe alizokuwa anakukataza usinywe lkn pia ukawa unataka mfanye mapenz yy akasema hayuko tyr mpaka mpaka utakapo muoa? Na we ukamwambia hauko tayar kuoa kwa muda huo Ni heri muachane kuliko kuendelea kuwa na mpenzi jina mnaishi Kama kaka na dada, Nikawa nashangaa sikumjibu kitu.....Akacheka sana huku akinibusu kwenye paji la uso...akaniambia we ndio mume wangu mtarajiwa, ila kuanzia Sasa hata mm sitak unywe pombe...sitak uwe na mwanamke mke mwingine tofauti na mm...akaendelea kusema mpenzi mm Nina wivu sana, pia Nina hasira...na hasira zangu Ni mbaya sana, naweza kukuharibia kabisa maisha yako, tafadhali fuata nilichokuwa utanufaika na vingi sana. Sikumjibu kitu pia nikawa nimeshikwa na bumbu wazi akaniambia tusimame Kuna kitu nataka kukuonesha, tukatembea Kama mwendo wa dk tatu....Akaniambia unapaona kule...akanionesha kwa kidole kwa mbali nikamwambia ndio, kuna nyumba nzuri sana zimepakwa rangi Kama ya dhahabu, akaniambia kule Ni kwetu mpenz mm na wewe, tukishakuwa mke na mume tutaishi kwenye zile nyumba kule. Baada ya kuniambia hvy akanikumbatia huku akinibusu maeneo ya shingoni...nikastuta, kuangalia simu ilikuwa ni usiku sana mida ya Kama saa 8 hv usiku. Nikasali sana usiku ule nikalia sana, hafla nikasijikia kichefu chefu na tumbo kunivuruga sana, nikatapika vitu Fulani hv vyeusi sana vinatoa harufu mbaya mno.

Sikupata usingiz mpaka kunakucha, nikawa najiuliza ile ndoto ina maana gani hasa, ina maana nimeshafunga ndoa na jini? Nikaona hapana...alikuwa ananilisha Nini ambacho kilifanana na matunda kupelekea kutapika kiasi kile! Huwez amini nilishikwa na hasira Sana asubuhi ile.

Ikumbukwe siku hiyo ya J.mosi tarehe 29 ndio yule dada anataka tuonane feri nimkabidhi nguo zake ambazo tayari nilikwisha zivaa, tukutane pale saa 7 mchana, nilichoshangaa kwenye ndoto hakuzungumzia kabisa swala lile...nikajiapiza sitomwogopa Tena na tukionana nitamwambia sitaki anifwatikie Kama Ni ele zake sijatumia hata Mia, na Niko tayar kumrejeshea ili mradi aachane na maisha yangu niwe na amani.

Ilipofika mida ya saa 5 hv asubuh safar ya kwenda feri ikaanza nikiwa na mfuko niliweka zile nguo na Wala sikuzifua..nlipofika feri pale posta nikaa sehemu nasubir saa 7 ifike ili nipande panton...nikijaribu kupiga ile namba yake inaita lakini haipokelew, ilipofika Kama saa 7 kasoro dk8 hv, sms ikaingia nimefika njoo nakusubiria. Nikakataa ticket ya kupanda panton kwa ajili ya kuja upande wa pili wa kigamboni....Nilikuwa naangaza macho kila mahali kuangalia Kama yupo karibu yangu...sikumuona, tulipofika wakat tunashuka hamadi nakutana na gari nyeusi aina ya kulga inapiga honi mbele yangu naona mkono umetolewa nje upande wa dereva kuashiria nimpe kitu na Nilikuwa karibu nalo...kuchungulia hv, Ni yule yule mwanamke...alionesha ishara ya kuhitaj ule mzigo nilivyomkabidhi akafunga kioo(vilikuwa tinted)..gari ikaanza kutembea taratibu kuelekea kwenye panton, nilikaa pale getini wanapouzia viatu vya kike nikiwa nachungulia lile gari mpk linaingia kwenye panton, simu yangu ikaita Tena...kuangalia Ni yeye...alisema tu Ahsante mpenzi akawa anacheka, kabla hajakata simu nikamwambia aniache na maisha yangu...nilimtukana sana siku Hy sijui nilikumbwa na Nini, sikumwachia hata nukta ya kuongea..kuja kuangalia simu hv...muda mrefu ilisha katwa, Ni Kama nilikuwa naongea mwenyewe.

Kimbembe...siku ya tar 31 mkesha wa mwaka mpya, tulikuwa tumepanga kwenda mkesha uwanja wa taifa na rafiki yangu, mchana alipiga simu nyingi sikupokea...akatuma sms akaniambia najua unachotaka kufanya olewako uende huko unakotaka kwenda, nitakuonesha Mimi Ni Nani. Nikatuma sms mfululizo za kumtukana sana, nikamwambia asinitishe, asinipangie Cha kufanya...naweza kufanya Jambo lolote ninalijisikia...hakujibu kitu, ilipofika jion kichwa kiliniuma sana...naweza sema sijawah umwa kichwa kiasi kile jamaa tuliyepanga nae kwenda alikuwa anapiga simu sikuweza hata kupokea, nikiwa katika maumivu makali kuangalia hv mbele yangu namuona live...amechukia sana, nilipiga kelele lakini sauti haikutoka..nguvu ziliniisha...kuna mambo aliongea siwez kuweka hapa nahofia usalama wangu, Jamani nipo kwenye kiapo kibaya sana...Kama Kuna mtu anajiamini anaweza niepusha na haya majanga anisaidie tofauti na hapo, naweza potea Mimi, mama yangu pamoja na huyo atakaenisaidia endapo atashindwa nguvu na huyu jini. Siwez kuendelea kuelezea chochote, nipo kwenye kiapo kizito sana hapa ninapongea Nina alama kwenye paja langu la kushoto...wanaojua haya mambo nafikir wanafahamu hiyo alama ina maana gani kwenye jamii hz za majini. Nipo kwenye kitanzi sijui nachomokaje!

Nahitaji msaada wenu wa dhati ndugu zangu. Zile nguo nilizompa nilifanya kosa kubwa sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
Sasa wewe muda wote unalialia tu niko kwenye wakati mgumu,wakati mgumu. Mimi sijaona jini alipokuweka kwenye wakati mgumu au mazingira hatarishi,ila ni wewe mwenyewe unajihatarishia. Kuna shida gani wewe ukiolewa na jini? Hakuna mahala amekufanyia vibaya,wala kukutukana,ila wewe unamtukana. Kweli cha moto unaweza ukakiona ksbb unamtukana,kama kumchokoza. Mshana (nafikiri) slishawahi kuna majini wazuri na wabaya. Huyo jini mzuri kabisa huyo,unamuogopa nini?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pole Mkuu kwa mkasa huu. Haya mambo yapo Sana Tena sana.

Kuna makosa kadhaa umeshayafanya tayari na yatakukusababishia fadhaa na mateso zaidi km hutachukua ushauri wa moto uliopewa na wadau.

Makosa hayo ni pamoja na kukubali kuvaa zile nguo ulizopewa zawadi kwa sababu rahisi ya umeme na mikunjo ya nguo zako.
(Tayari zilisharogwa kupitia manukato uliyoyahisi/nusa)

Pili kukubali kuzipeleka kwake ukiwa tayari ulishazivaa(zikiwa na jasho lako). Ni rahisi kwa mshirikina yeyote kukufanyia lolote kupitia jasho hilo.
Tatu kuendelea kuzishikilia zawadi unazopewa za pesa (zirudishe kwa namna yoyote), ikishindikana kazitoe zaka na sadaka tena bila tamaa ya moyoni. Na uwe tayari kuzilipa km utadaiwa baada ya kuzitoa sadaka.

Nne ni kuwa naona unapuuza ushauri ya kufanya maombi maalumu ya kufunga hata kwa kushirikisha watumishi/ wamwabuduo BWANA MUNGU kwa roho na kweli.
(Hapa niwe serious kidogo) epuka mambo ya roho ya uponyaji na jamii ya waabuduo miujiza kama silaha ya UKRISTO - utaongezewa mapepo huko.

Jitahidi kuwaza na kutenda km unavyokusudia pasipo hofu hata km atakuingilia katija Kila hatua ya kujiondoa kwako kwake.(huyo jini)

Nne hakuna mwanadamu anayeweza kupambana na jini/shetani kwa nguvu zake/zetu wenyewe. Ni ubatili kuita mtu mwenye nguvu aje akusaidie.
(Wenye nguvu ni wale wanaomtegemea BWANA MUNGU PEKEE)

TANO NA MWISHO.
Usiendelee kutoa muendelezo wa mashindano yako na jini kwa sasa. Kwani kupitia haya unayoyaandika ndivyo unavyojianika udhaifu wa roho yako (siyo moyo wako). Na hivyo adui akatumia fursa hii.

Jitahidi kuiokoa nafsi yako kwa gharama KUU YA DAMU YA YESU KRISTO. Tumepewa fursa ya uhai na MUNGU MWENYEZU si kwa bahati mbaya mkuu. Uzima na uhai ni jukumu letu kuvilinda na kuvitunza kwa nguvu na bidii zote.


HAKUNA BAYA LINALOMSHINDA BABA MUNGU MUUMBAJI KUPITIA YESU KRISTO

BWANA MUUNGU NA AKUKINGE KWA UOVU HUU UNAOKUAMBATA KWA SASA NA HATA MILELE. NAKUOMBEA HAYA KATIKA JINA LA YESU KRISTO. AMINA.
 
Pole Mkuu kwa mkasa huu. Haya mambo yapo Sana Tena sana.

Kuna makosa kadhaa umeshayafanya tayari na yatakukusababishia fadhaa na mateso zaidi km hutachukua ushauri wa moto uliopewa na wadau.

Makosa hayo ni pamoja na kukubali kuvaa zile nguo ulizopewa zawadi kwa sababu rahisi ya umeme na mikunjo ya nguo zako.
(Tayari zilisharogwa kupitia manukato uliyoyahisi/nusa)

Pili kukubali kuzipeleka kwake ukiwa tayari ulishazivaa(zikiwa na jasho lako). Ni rahisi kwa mshirikina yeyote kukufanyia lolote kupitia jasho hilo.
Tatu kuendelea kuzishikilia zawadi unazopewa za pesa (zirudishe kwa namna yoyote), ikishindikana kazitoe zaka na sadaka tena bila tamaa ya moyoni. Na uwe tayari kuzilipa km utadaiwa baada ya kuzitoa sadaka.

Nne ni kuwa naona unapuuza ushauri ya kufanya maombi maalumu ya kufunga hata kwa kushirikisha watumishi/ wamwabuduo BWANA MUNGU kwa roho na kweli.
(Hapa niwe serious kidogo) epuka mambo ya roho ya uponyaji na jamii ya waabuduo miujiza kama silaha ya UKRISTO - utaongezewa mapepo huko.

Jitahidi kuwaza na kutenda km unavyokusudia pasipo hofu hata km atakuingilia katija Kila hatua ya kujiondoa kwako kwake.(huyo jini)

Nne hakuna mwanadamu anayeweza kupambana na jini/shetani kwa nguvu zake/zetu wenyewe. Ni ubatili kuita mtu mwenye nguvu aje akusaidie.
(Wenye nguvu ni wale wanaomtegemea BWANA MUNGU PEKEE)

TANO NA MWISHO.
Usiendelee kutoa muendelezo wa mashindano yako na jini kwa sasa. Kwani kupitia haya unayoyaandika ndivyo unavyojianika udhaifu wa roho yako (siyo moyo wako). Na hivyo adui akatumia fursa hii.

Jitahidi kuiokoa nafsi yako kwa gharama KUU YA DAMU YA YESU KRISTO. Tumepewa fursa ya uhai na MUNGU MWENYEZU si kwa bahati mbaya mkuu. Uzima na uhai ni jukumu letu kuvilinda na kuvitunza kwa nguvu na bidii zote.


HAKUNA BAYA LINALOMSHINDA BABA MUNGU MUUMBAJI KUPITIA YESU KRISTO

BWANA MUUNGU NA AKUKINGE KWA UOVU HUU UNAOKUAMBATA KWA SASA NA HATA MILELE. NAKUOMBEA HAYA KATIKA JINA LA YESU KRISTO. AMINA.
Nashukuru kwa ushauri wako mzuri mkuu, kwanza nipende kubainisha hili mm Ni mkristo kamaili naamini katika Yes kristo, hv ninavyoongea naendelea na huduma ya maombezi kwa Hali niliyokuwa nayo mwanzo nisingeweza hata kuandika uzi huu, Maombi ndio yamenipa ulinzi na nguvu juu ya Vita kubwa niliyonayo kwa Sasa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hahahah bro watch out, gari yangu iliniwakia moto, kazi nikafukuzwa, nilikua nalipwa 2M nikaishia kwenye umasikini uliotukuka, hiyo perfume kalii harufu yake naijua..washenzi sana hawa viumbe..michezo ya kukatiwa umeme, gate kufungiwa (imenitokea) kila nikitaka kuingia home halifunguki inabidi nimtafute nikalale kwake..so sad! Mbaya zaidi anapoanza kuku.control..
Duh! Mkuu una mengi ya kutueleza
 
Nashukuru kwa ushauri wako mzuri mkuu, kwanza nipende kubainisha hili mm Ni mkristo kamaili naamini katika Yes kristo, hv ninavyoongea naendelea na huduma ya maombezi kwa Hali niliyokuwa nayo mwanzo nisingeweza hata kuandika uzi huu, Maombi ndio yamenipa ulinzi na nguvu juu ya Vita kubwa niliyonayo kwa Sasa.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mungu akusaidie na ulete mrejesho ukiwa mzima kabisa
 
nikakuta jamaa ananiangalia kwa utulivu na hata alipojua nimemuona hakuondoka nilipopiga kelele hakuondoka nikaduwaa siamini baada ya dk tatu akaondoka mwenyewe

Hapo ndio umejua kusolve vitu kistaarabu
 
Back
Top Bottom