HesabuKali
JF-Expert Member
- Jan 4, 2016
- 2,791
- 5,687
Habari wanajamii forum, ni matumaini yangu kuwa mko salama. Ama la, basi Mungu awafanyie wepesi.
Ndugu zangu nahitaji msaada wa mawazo yenu sana. Ninapitia sijui niseme ni wakati mgumu au ni ujinga wa kujitakia. Niko kwenye mahusiano na mume wa mtu sasa yapata miaka mitatu. Imefikia hatua nimechoka na nahitaji kujingβatua ila nakosa njia nzuri ya kuachana nae. Am not even proud with what i did so if you judge me iβll understand.
Huyu mtu tangu nafahamiana nae ameyabadilisha sana maisha yangu maana ana mchango mkubwa sana. Alinisaidia kupata kazi nzuri na kuachana na kakazi kangu nilikokuwa nafanya, alinihamisha na kunipangishia sehemu nzuri zaidi. Baadae alininunulia gari nami nikawa natembea nimekaa, pia amenijengea nyumba iliyo kwa jina langu ila kwakuwa ipo nje ya mji nimeipangisha nakula kodi ila bado analipia kodi hapa ninapoishi.
Mahusiano yalipoanza sikufikiria hata yangechukua miezi 6, ila sasa ni miaka mitatu+. Ni mwanaume anayejali sana ila ana wivu balaa. Ni mara kadhaa amekuwa akinitishia kuwa akigundua ninamsaliti atanikata shingo. Sasa huwa najiuliza huyu ni mume wa mtu, anatarajia kweli niwe na yeye tu ili iweje?
Sasa nimechoka jamani, natamani niwe na mpenzi wangu na sio mume wa mtu. Kuna huyu kijana nimeanza nae mahusiano sasa ni miezi 5, kusema kweli nampenda na ninaona kabisa nae ananipenda. Haya ndio aina ya mahusiano niyatakayo. Nimekuwa nikitafuta visingizio kuwa asije kwangu maana sio maadili ila ukweli ni kuwa naogopa mlipa kodi akijua atanitoa roho.
Huyu mume wa mtu nishamtafutia visingizio ili tuachane ila inashindikana. Natamani yeye ndio aanze ili asije kuwa na kinyongo. Ila kuna wakati najipa moyo kuwa nimwambie tu tuachane lakini nikikumbuka aliwahi kunikunja nusura anipige alipokuta msg asizozielewa kwenye simu nahisi kutetemeka. Aliwahi kunionyesha silaha anayomiliki, nilipomuuliza ni ya nini akasema hata mimi nikimletea ujinga ananifyatua. Japo ulikuwa utani ila niliogopa kusema kweli.
Balaa zaidi recently ameanza kungβangβania nimzalie. Nimekuwa nikijifanya mimba hazishiki ila kusema kweli natumia dawa zisishike maana siko tayari kuzaa nae. Kwanza nahisi kama suffocation maana ananibana sana. Kwangu anakuja tu muda wowote akijisikia, na ole wangu asinikute nyumbani ni tatizo kubwa. Kila ninachofanya anahitaji apate taarifa kwanza, yaani kama mkewe vile jamani.
Nimejaribu kuelezea haya ili angalau muelewe ni kwanini nahitaji msaada wa mawazo yenu ili nijikwamue kwenye hili shimo nililojichimbia. Nipeni ushauri naachanaje na huyu mwanaume bila kuleta madhara kwangu.
Watu komenti kama hizi sijui hawazioni [emoji1787][emoji1787][emoji1787] au wewe Mama pretty ni mwanaumeRudisha mali zake ili uwe na maisha ya amani.. vitu hutafutwa ila uhai once ukiondoka haurudi tena...
Hama alipokupangishia ikiwezekana tafuta kazi sehem nyingine maana bila hivyo ataendelea kukutafuta.. piga block kila sehem.. hayo ni madhara ya kudate mume wa mtu .. pole sana kwa hali hiyo ya kujitakia.. unahitaji nawe uwe na familia lakini uliendekeza kudanga kwako kwa kumtegemea kila kitu..
Hivi dada unajiskiaje kudate na mtu ambae akitoka kwako anaenda kulala na mwanamke mwingine? Mnawezaje jaman.. I don't judge you by the way
'Mwanaume ukimfanya danga lako nae atakufanya malaya wake..'
Cc: DeepPond
Ni kwake, anauhuru wa kuingia na kutoka anavyohisi
Kejeli na kumkandia na kumtisha na kumkatisha tamaa hujaona hilo?Ni nani uliyeona amefurahia hili jambo hapa? Au umekuja kutema nyongo ulizotoka nazo kwa mkeo ndugu yangu?
Rudisha vitu vyake vyote ,then acha hio kazi kaanzishe biashara kigamboniHabari wanajamii forum, ni matumaini yangu kuwa mko salama. Ama la, basi Mungu awafanyie wepesi.
Ndugu zangu nahitaji msaada wa mawazo yenu sana. Ninapitia sijui niseme ni wakati mgumu au ni ujinga wa kujitakia. Niko kwenye mahusiano na mume wa mtu sasa yapata miaka mitatu. Imefikia hatua nimechoka na nahitaji kujingβatua ila nakosa njia nzuri ya kuachana nae. Am not even proud with what i did so if you judge me iβll understand.
Huyu mtu tangu nafahamiana nae ameyabadilisha sana maisha yangu maana ana mchango mkubwa sana. Alinisaidia kupata kazi nzuri na kuachana na kakazi kangu nilikokuwa nafanya, alinihamisha na kunipangishia sehemu nzuri zaidi. Baadae alininunulia gari nami nikawa natembea nimekaa, pia amenijengea nyumba iliyo kwa jina langu ila kwakuwa ipo nje ya mji nimeipangisha nakula kodi ila bado analipia kodi hapa ninapoishi.
Mahusiano yalipoanza sikufikiria hata yangechukua miezi 6, ila sasa ni miaka mitatu+. Ni mwanaume anayejali sana ila ana wivu balaa. Ni mara kadhaa amekuwa akinitishia kuwa akigundua ninamsaliti atanikata shingo. Sasa huwa najiuliza huyu ni mume wa mtu, anatarajia kweli niwe na yeye tu ili iweje?
Sasa nimechoka jamani, natamani niwe na mpenzi wangu na sio mume wa mtu. Kuna huyu kijana nimeanza nae mahusiano sasa ni miezi 5, kusema kweli nampenda na ninaona kabisa nae ananipenda. Haya ndio aina ya mahusiano niyatakayo. Nimekuwa nikitafuta visingizio kuwa asije kwangu maana sio maadili ila ukweli ni kuwa naogopa mlipa kodi akijua atanitoa roho.
Huyu mume wa mtu nishamtafutia visingizio ili tuachane ila inashindikana. Natamani yeye ndio aanze ili asije kuwa na kinyongo. Ila kuna wakati najipa moyo kuwa nimwambie tu tuachane lakini nikikumbuka aliwahi kunikunja nusura anipige alipokuta msg asizozielewa kwenye simu nahisi kutetemeka. Aliwahi kunionyesha silaha anayomiliki, nilipomuuliza ni ya nini akasema hata mimi nikimletea ujinga ananifyatua. Japo ulikuwa utani ila niliogopa kusema kweli.
Balaa zaidi recently ameanza kungβangβania nimzalie. Nimekuwa nikijifanya mimba hazishiki ila kusema kweli natumia dawa zisishike maana siko tayari kuzaa nae. Kwanza nahisi kama suffocation maana ananibana sana. Kwangu anakuja tu muda wowote akijisikia, na ole wangu asinikute nyumbani ni tatizo kubwa. Kila ninachofanya anahitaji apate taarifa kwanza, yaani kama mkewe vile jamani.
Nimejaribu kuelezea haya ili angalau muelewe ni kwanini nahitaji msaada wa mawazo yenu ili nijikwamue kwenye hili shimo nililojichimbia. Nipeni ushauri naachanaje na huyu mwanaume bila kuleta madhara kwangu.
Good kama umejutia..Well natambua kabisaaa what i did sio kitu cha kuwa proud nacho na nimesema kabisa. Kabla ya kuwa na huyu mume wa mtu nilikuwa kwenye toxic relationship hadi pale nilipokutana na huyu. To be honest hajawahi nifanyia baya, amenipa good times sana, nimetembea nchi nyingi kwa sababu yake. Hizi good times na kujali kwake ndiko kulinipiga upofu japo kweli kuna muda nafsi inauma kuwa sio wangu. Lakini muda mwingi sana nakuwa nae kama tu vile watu wengine wenye mahusiano wanavyokuwa.
Anyway nimechoka kuwa mchepuko wake na nafsi inazidi kunisuta ndio maana nataka niachane nae.
Kwanini dada angu πππWatu komenti kama hizi sijui hawazioni [emoji1787][emoji1787][emoji1787] au wewe Mama pretty ni mwanaume
Mpendwa wangu kama huna kikwazo cha kuolewa mke wa pili olewa tu maana huyo bwana anaonekana anakujali, unaweza kwenda kutafuta wa peke yako naye akawa na mambo yake ya ajabu au akakuletea wenzio yakawa yaleyale
Kuna kitu kipo ndani yetu wanaume ambacho hamnacho nyie wanawake nacho ni kupenda.
Tunauwezo wa kupenda Mwanamke zaidi ya mmoja na kuheshimu wote kwa nafasi zao.
Kwenu wanawake ni changamoto kidogo kuwa na upendo kwa wanaume wawili.
Sisi tunaweza kutamani ukajua tumependa kumbe la!
Tunaweza kupenda ukajua tumetamani.
Kipimo cha mwanaume anayependa ni ile kujali na kuhudumia, fikiri mtu ama make na pengine ana familia lakini bado amejitoa kukujali na kukuhudumia na kukulinda.
Hapo hajakutamani bali amekupenda.
Na kama unavyojua maswala ya kupenda huenda mpaka ndani ya moyo na nafsi na akili na matokeo huonekana kwenye mwili.
Sasa mtu kama huyo kumtoka sio rahisi sana maana mchakato wake ni kuanzia ndani ya nafsi mpaka aje akubali atakua amesumbuka sana na pengine kupoteza vingi wakati akichakata kuondoka kwake moyoni mwake.
Kwa sisi wengine tunaweza kuvumilia kipindi kigumu kama hiko kwa tumaini ya kwamba yatapita tu lakini tutabakiwa na majereha makubwa sana moyoni.
Wengine kwa kweli hawana uwezo wa kuvumilia hali hiyo, wanafanya maamuzi magumu yenye gharama kubwa mpaka ya uhai, na vile umesema ana bunduki, jiadhari sana.
Unaweza ukafanya jambo hilo bila athari kubwa iwapo unatumia busara na akili kubwa na hoja za nguvu.
Kuna dawati la jinsia,kuna viongozi wa dini, kuna wanasheria,kuna watu wa heshima kwako na kwake, na pia nyie wawili mkikaa mkiambina ukweli naamini kabisa mtafika mwafaka ulio bora.
Binafsi nakuombea na kukutakia yote mema,naamini kidogo unapitia pagumu lakini wakati mmoja utafika na utakuwa na heri na furaha na amani.
Mwambie mpenzi wako mpya haya yote ajajuwe before. All the bestMali zake na kazi niko tayari kumuachia maana i can manage without him. Tatizo nawaza hatokuwa na kinyongo au hata kunidhuru maana ana wivu balaa. Halafu mpenzi wangu sio serengeti boy ananizidi umri, elimu hadi mali. Kiufupi yuko vizuri na anayamudu maisha vizuri tu.
Ushauri gani unataka wakati bado tamaa zimekujaa mpaka kwenye kope za macho? Rudisha nyumba yake, rudisha kodi zake na kila ulichopewa kwa makubaliano kuwa muwe wapenzi halafu muambie huyo kijana mwenzako akupe unavyopenda au mbaki na shida zenu ndio mfurahie hayo mapenzi yenu na kijana mwenzako.
Kingine chunguza sana huyo kijana huenda kakupenda kwa kuwa una gari, kazi nzuri na nyumba ulivyopewa na mume mwenzake.
Mwisho kabisa cha mtu hakiliwi bure.
Sasa akifa kwa stress si tutamkosa?ππππKhaa we Luky [emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Mimi nahisi unashindwa kuelewa kwamba jamaa anakuchukulia kama mke wake mpaka hapo na kwa hayo aliyoyafanya, nadhani ungejiandaa kisaikolojia kuwa mke wa pili tu.
Ina changamoto zake ila sidhani kama mtu mzima angewekeza kiasi hicho kwako bila kuwa na malengo na wewe. Fahamu kwamba mara nyingi mke wa pili anaanza kama mchepuko. Mtunuku jamaa mtoto, mpe ushirikiano uyaishi maisha yako.
Leo unampenda huyo kijana kwasababu umetengenezwa ukatengenezeka ila utakapoingia tu na kumuacha mumeo ndo utajua hujui.
Vijana ni wana mambo mengi sana na utapata msongo wa mawazo bure. Mimi nadiriki kusema inawezekana mahusiano yako na huyo kijana hata yasidumu.
Sasa wewe unavyotaka kimbwaga baada ya yote aliyokifanyia ndio fair?!!Hii sio fair hata kidogo.