Nimekuwa na mahusiano na mume wa mtu kwa miaka 3 nahitaji kuachana naye, nimuachaje bila yeye kuweka kinyongo

Hapana, sijipigii pasi. Ni utani tu, anaweza kwenda popote na inaonesha ni mzoefu wa kusafiri. Kama anaishi Arusha akienda kujificha Mtwara au Songea au hata Mbeya ataishi kwa amani. Siwezi kumshauri Kubaki sehemu ambayo haridhiki.
Wee bwana huyu mrembo wa mjini kazoea raha za huku mujini huko kwengine ataona shida tuu
 

Bila hata kuuza nyumba i have more than that. Ndio maana natamani nimuachie vitu vyake vyote niendelee na maisha yangu.
 
Sahii kabisa,
Hizo Ni mbwembwe za penzi jipya kwasababu anajua mwanamke wa class ya juu asionekane marioo

Ila uwezo wa kuhudumia Kama mwanzo ndo asahau kabisa[emoji4]

Ni kweli wanatofautiana na mchepuko kiuwezo lakini yeye sio mnyonge kama mnavyomfikiria. Ni mtu namfahamu vizuri tu kwa muda sasa. Labda apretend kuhusu kunipenda ila kuhusu mali anazo zake na ni mpambanaji sana.
 
Basi kama na huyu wa huyu yupo kama wewe,hapo utata!

Niliwahi kumuuliza hivi mkeo akijua itakuwaje? Akaniambia akijua ndio vizuri ili tusifiche fiche sasa maana hana cha kufanya. Tatizo moyo wa mtu kichaka, sio wanawake wote ni wanyonge unaweza pigwa tukio la hatari.
 
Niliwahi kumuuliza hivi mkeo akijua itakuwaje? Akaniambia akijua ndio vizuri ili tusifiche fiche sasa maana hana cha kufanya. Tatizo moyo wa mtu kichaka, sio wanawake wote ni wanyonge unaweza pigwa tukio la hatari.
Ni kweli mtu akijiona 'mnyonge' basi anaenda kutafuta 'nguvu' popote zinapopatikana
 
Wanavyosema ni kama mimi sina ninachopoteza katika hili.
Hawa viumbe ni wabinafsi sana ni wa kuishi nao kwa akili sana. Kuna mdau kasema hapo chukua mkopo then jifanye huwezi kuulipa ili akuone duwanzi akuache. Nami naungana nae maana naona kama ukilianzisha wewe utapigwa na kitu kizito.
 
Sasa kwa yote hayo alokufanyia mbona tayari ni mumeo!? Hapana mie sikushauri umuache unaweza pata laana! Hapo tafteni tu namna muyarasmishe hayo mahusiano na uhesabike ni mke mdogo!
nina hakika hata ukipata mume huyo jamaa hutaachana nae, mtaachana kwa muda tu!
 
Wapendwa badala mnipe ushauri mnaniongezea magazijuto kweli? Najua i messed up big time and an not proud. Nisaidieni najikwamuaje hapa.
Ngoja tuongeze sauti basi,

Hapo HUKWAMUKI dada!
 
Kaa naye uongee naye kwa kina na uwe tayari kumrudishia mali zake kama atapenda umrudishie ili ukaanze maisha upya na huyo mpenzi wako mpya, kila lakheri.
 
Ushauri mzuri ila mleta mada hajasema kuwa hampendi ila shida iliyopo ni kwasababu ya kuwa kwenye mahusiano na Mume wa mtu.
 

Mume wangu kivipi sasa na ni mume wa mtu? Hatuwezi kurasimisha maana ni mkristo.
 
kwan polepole yeye anasemaje....?! tumsbil atakuja kutolea ufafanuzi
 
Dini hairuhusu mke wa pili.
Mfalme Sulemani alikuwa na wake wangapi? Yeye hakuwa na dini? Mfalme Daudi alikuwa na wake wangapi? Yeye hakuwa na dini? Haya, Ibrahimu ambaye wewe mwenyewe unamuita baba wa Imani alikuwa na wake wangapi? Yeye hakuwa na dini? Au wewe Mungu wako ni bora zaidi ya Mungu wa Ibrahimu, Yacobo na Isaka?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…