Nimelima ekari tano za mihogo, itakuwa tayari kwa mavuno mwezi wa Ramadhani

Nimelima ekari tano za mihogo, itakuwa tayari kwa mavuno mwezi wa Ramadhani

Sky Eclat

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2012
Posts
57,761
Reaction score
216,011
Ekari tano kulima ilinigharimu laki nne, nilipata vijana wanne kwa makubaliano unawapa sehemu ya kulala, wanatembea na kapu lao ndani wana sufuria. Wanaamaka asubuhi wanakwenda kulima mpaka saa tano wamemaliza. Wakirudi wanapika chakula chao wenyewe. Iliwachukua siku tatu kumaliza ekari tano na kila mtu alishika laki yake mkononi.

Tulipanda mwezi November, palizi tumemaliza wiki iliyopita. Palizi ilichukua laki mbili. Kuna wanunuazi wameomba kuchukua shamba kwa milioni tatu. Hili bado sijaafikiana nao. Ninataka kuuza rejareja kwa watakao hitaji ya iftar.

Shamba liko katika barabara kuu kwahiyo changamoto ya usafiri sina. Faida nyingine ni kula kisamvu, baada ya palizi tumeanza kula kisamvu na kitamu sana.
 
Ni muda muafaka wa kutufundisha kutengeneza chapati za mihogo kwa utaalamu wa Brazil.
  1. Stir together the flour and salt. Make a well in the centre and add 5–6 tablespoons of lukewarm water with the oil. Using your hands, bring the dough together into a ball. Turn out onto a work surface and knead for 5–10 minutes, wrap in cling film and leave to rest for 20 minutes.
  2. Divide the dough into four portions and roll into small balls. Dust a work surface with a little flour. Roll out each ball until around 18cm/7in in diameter, around 2–3mm/⅛in thick.
  3. Dry-fry over a medium heat for 20 seconds, pressing lightly with a spatula. Flip over and cook on the other side for 20 seconds, or until the tortilla is cooked, but remains soft and pliable. Repeat with the remaining three tortillas.
 
Shamba liko sehemu gani tuangalie logistic za kuja kununua pia unaweza kuangalia uwezekano wa kuongeza mnyororo wa dhamani kwa kuprocess starch ya muhogo ni dili sana huko duniani
 
Ekari tano kulima ilinigharimu laki nne, nilipata vijana wanne kwa makubaliano unawapa sehemu ya kulala, wanatembea na kapu lao ndani wana sufuria. Wanaamaka asubuhi wanakwenda kulima mpaka saa tano wamemaliza...
Mkuu ni kweli au ya Majaliwa haya 🤣
 
shamba liko sehemu gani tuangalie logistic za kuja kununua pia unaweza kuangalia uwezekano wa kuongeza mnyororo wa dhamani kwa kuprocess starch ya muhogo ni dili sana huko duniani
Mhh mihogo ekari tano ni majaribio tu, hayo mambo ya logistic nitatawaza nikifanya ekari 10-20.

Mwaka huu hii nitauza tu kwa wateja rejareja.
 
Usiwauzie hao kwa kila eka moja ukiuzia dalali shambani haukosi milioni moja na nusu, kama una soko lako mahali haukosi mpaka milioni mbili na nusu, ukifanikiwa kupata soko cocobeach kama shamba ni jirani na Dar, ndo unaula kabisa
 
Bagamoyo hyo au vikindu na kisemvule au mkuranga Hilo chini ndio chimbo lako lilipo
 
Back
Top Bottom