Nimelima ekari tano za mihogo, itakuwa tayari kwa mavuno mwezi wa Ramadhani

Nimelima ekari tano za mihogo, itakuwa tayari kwa mavuno mwezi wa Ramadhani

Tabia yenu Wanaume wa Dar wengi kupenda kula ftari la chapati ,tambi ,andazi

Na kuacha kula mazao ya mizizi kama mihogo ,magimbi, viazi nk muache hio tabia
We mwenyewe ni Kunguru wa Manzese. Ungekuwa Kunguru wa Kibondo au Simbiti ningeelewa hoja yako.
 
Ekari tano kulima ilinigharimu laki nne, nilipata vijana wanne kwa makubaliano unawapa sehemu ya kulala, wanatembea na kapu lao ndani wana sufuria. Wanaamaka asubuhi wanakwenda kulima mpaka saa tano wamemaliza. Wakirudi wanapika chakula chao wenyewe. Iliwachukua siku tatu kumaliza ekari tano na kila mtu alishika laki yake mkononi.

Tulipanda mwezi November, palizi tumemaliza wiki iliyopita. Palizi ilichukua laki mbili. Kuna wanunuazi wameomba kuchukua shamba kwa milioni tatu. Hili bado sijaafikiana nao. Ninataka kuuza rejareja kwa watakao hitaji ya iftar.

Shamba liko katika barabara kuu kwahiyo changamoto ya usafiri sina. Faida nyingine ni kula kisamvu, baada ya palizi tumeanza kula kisamvu na kitamu sana.
Tunaomba mrejesho bimkubwa
Maana mfungo ndo umeisha hv
 
Naona atakuwa bado anakokotoa hisabu ya mapato na matumizi ili aje na mrejesho ulioshiba.
Mama yetu huyu kwa msio mjua huwa ni kama motivation speaker. Utakuta anasema vitu vingii, utadhani kweli anafanya, kumbe kaja tu hapa ku-socialize. Yeye yupo zake nje ya nchi Uzunguni anakula maisha. Sasa hizi kazi za wavuja jasho ataziwezea wapi?

Unakuta siku nyingine anasema kaona fursa baada ya kwenda Ferry hivyo ataanza kukaanga dagaa na kuawauza kwenye Mwendokasi, kumbe wakati huo yupo zake Uzunguni ndani ya nyumba kawasha heater anaondoa ubaridi. Hapa kaja ku-refresh mind kutokana na loneliness iliyopo kwa Wazungu maana uzunguni ukitoka kazini kama siyo wakati wa summer ni kukaa ndani mwako na kujifungia kama kuku wa kisasa.. Ha ha haaa.
 
Madamme, niko very impressed na mapambano yako[emoji119][emoji119]
 
  1. Stir together the flour and salt. Make a well in the centre and add 5–6 tablespoons of lukewarm water with the oil. Using your hands, bring the dough together into a ball. Turn out onto a work surface and knead for 5–10 minutes, wrap in cling film and leave to rest for 20 minutes.
  2. Divide the dough into four portions and roll into small balls. Dust a work surface with a little flour. Roll out each ball until around 18cm/7in in diameter, around 2–3mm/⅛in thick.
  3. Dry-fry over a medium heat for 20 seconds, pressing lightly with a spatula. Flip over and cook on the other side for 20 seconds, or until the tortilla is cooked, but remains soft and pliable. Repeat with the remaining three tortillas.
nmejikuta nmecheka hatar [emoji1][emoji1][emoji1]
 
Chondechonde usiwauzie wajanja wa mjini sitasahau walimliza dada mmoja mjane aliamua auze ili apate ada ya watoto, kilichomtokea si yeye hata Mimi sitosahau, jamaa walikuja na Fuso wakaanza kuvuna mihogo Fuso halijai heka ya kwanza, ya pili, ya tatu na mihogo imeishia nusu ya gari, mwisho dada wa watu akawaambia basi acheni wakang'ang'ania kuvuna mwisho akawaambia na hela yenu msinipe nikama nimewalimia ninyi. Sio hadithi hii ilitokea chanika miaka ya nyuma 2006, nadhani Sasa watakuwa wameongeza utaalam zaidi wa kuwaibia wakulima.
Walimwibiaje?
 
Mbegu nililetewa mizigo 40 kwa 8,000 mzigo mmoja
Kwa hiyo mpaka hapo ni
Mbegu 320,000
Kulima 400,000
Palizi 200,000
JUMLA 920,000

Ofa 3,000,000
Ukikubali ofa, faida 2,080,000

Je imechukua miezi mingapi toka upande mpaka ulipopata ofa ya Tshs. 3,000,000?
Vipi hakuna gharama za wadudu waharibifu au ulinzi wa shamba dhidi ya wezi?
 
Kwa hiyo mpaka hapo ni
Mbegu 320,000
Kulima 400,000
Palizi 200,000
JUMLA 920,000

Ofa 3,000,000
Ukikubali ofa, faida 2,080,000

Je imechukua miezi mingapi toka upande mpaka ulipopata ofa ya Tshs. 3,000,000?
Vipi hakuna gharama za wadudu waharibifu au ulinzi wa shamba dhidi ya wezi?
Ingia shambani usilimie hewani
 
Inategemea na mchumaji mkuu, kisamvu cha mihogo kwa usalama zaidi inatakiwa achume mwanaume,
Hata kunde na mazao mengineyo ya mboga inatakiwa achume mwanaume, usiruhusu hata siku moja achume mwanamke au binti maana huwezi juwa yupo kwenye hali gani

Ila kisamvu cha mihogo ni kitamu asikwambie mtu
Watu wa pwani wakisema kisamvu kitamu ,tunajiuliza sana maana iswahili chenu kigumu
(Sorry ni chombezo )
 
Back
Top Bottom