Nimelima nyanya heka 1 nimepata faida ya Tsh. Milioni 9 ndani ya miezi minne

Nimelima nyanya heka 1 nimepata faida ya Tsh. Milioni 9 ndani ya miezi minne

Ewe msomaji wa uzi huu, epuka kilimo cha aina yoyote nchi hii. Kilimo cha nyanya ndiyo usijaribu kabisa.

Waliokulia kwenye maeneo ya kilimo cha nyanya wana msemo wao usemao "nyanya, nyanyasa".
 
JF wasaalam 🙏

Kama unataka mali utaipata shambani.

Nianze kuwaomba vijana na sio kuwashauri maana kama kushauriwa mmeshauriwa sana hadi basi lakini hambadiliki.

Mimi nami ni kijana mwenye miaka 30+ hivi hiki nachokisema ni kweli na nimekifanya mwenyewe.

Uzi utakuwa mrefu kidogo vumilia tujifunze kitu.

Najua umesoma una elimu yako au pengine una kazi yako (ajira) unaingiza kiasi fulani cha pesa hii ni nzuri.

Lakini kamwe haikufanyi usijishughulishe na kuwaza nje ya box!

Binafisi mimi ni muajriwa wa company flani ya madini hapa Tanzania nipo kwenye mgodi mkubwa tu. Malipo yapo vizuri pia ukilinganisha na sector zingine.

Naowamba rafiki zangu huo ufahari mliojipatia kwenye mitandao ya kijamii uvueni na vaeni uhalisia wa maisha yenu.

Mara nyingi tunabishana humu kijana anakuambia tecno, Huawei,nk eti sio simu hizo Ili hali hata kwenye bandiko lake unatumia simu hiyohiyo

Lakini kiuhalisia maisha yako yanazidiwa mbali na mtu anayemiliki hiyo simu.

Kijana kuwa na vitu vya gharama usivyofaidika navyo ni hasara rafiki yangu.

Kama una mtaji hata kidogo tu usisite au hata uza hiyo simu yako ingia kwenye kilimo ukiwa na mtaji hata 600k-1000k ni kianzio kizuri mno na simu nzuri utanunua humo.

Tarehe 7/3/2024 nilipandikiza nyanya zangu na mwishoni mwa mwezi wa5 nikaanza mavuno ya nyanya.

Gharama nilizotumia ni m
Tsh. Milioni 3 tu ikiwa pamoja na vijana wenzangu wa kazi, madawa, mbolea na vifaa vya kazi kama majembe solo nk.

Hii nimepata hasara makadilio ilikuwa nipate faida walau 15+ Hivi

Na hii ilitokana na bei kuwa chini, vilevile Kuna mbegu nilinunua Kwa mkulima mwenzangu baada ya kwangu kutokuota vzr na hivyo kupeleka kuhitaji mbegu haraka iliyo tiyari kupandwa. ndipo nilipo nunua Ili niweze kumalizia sehemu iliyopelea.

Pamoja na hayo hii miezi 4 kupata Milioni 9 faida na kazi yangu na fanya sio Hela kidogo. Ni faida kwangu.

Saivi issues kuhusu wateja sio ya kuuliza tena wanyarwanda,waganda na wakenya wanafika hadi shambani kwako wanachukua mzingo na kupewa cash yako na wanaacha na hela ya andvance usiuuze kwa mwingine ila uwe na mzigo wa maana tu.

Na shangaa mno vijana ku fake maisha yasiyo Yako asee.

SISEMI UONGO!
Kwa sasa nina miaka 3 bila kufika Dar na wala Sina mpango wa kuja dar Kwa sababu Sioni kipya cha kunileta Dar.

Sana sana napoteza muda wangu tu bure pamoja na hela. Japo wapo wenzangu na wadogo zetu wasio jitambua wao Kila off wanaenda Dar tena kwa ndege ukiangalia wanachoenda fanya ni kula bata.

Tena wanasimuliana amelala na wanawake wa hadhi gani na wanaonyeshana picha!

Kumbuka sisi tunatinga siku 7 day night siku7 then off siku7 (mapumziko)

Hicho ndo huwa kina wa
Peleka Dar! Unabaki kuwaonea huruma tu kujenga hawajajenga nk.

Simu walizo nazo Sasa utacheka simu kubwa ya thamani kuliko Gm (general manager) wa hapa mgodini!

Ni sawa hatuwezi kupangiana maisha lakini kumbuka kesho utakuwa na familia na pia uzee upo mbioni!!

Kwa Sasa vitu vyangu naagiza online Dar hadi nilipo kwa gharama ya 10k au 20k naokoa zaidi ya 300k ya nauli chakula na malazi.

Ninayo mengi sana ya kusema lakini kilimo kinalipa sana.

Hasara ipo kila sehemu asee iwe biashara ufugaji nk. Nilichojifunza tusikate tamaa tu.

Nimewahi kuagiza vifaranga vya kuku 400 asee vilkufa nikabaki na kuku 17 tu kati ya hizo nilizani nimelogwa hadi siku Moja nipo mitandaoni nadhurula nikaona clip ya jamaa analia kuku wake zaidi 10 Elfu wamekumbwa na mafuriko na kufa wote nilimuonea huruma na kujifunza Somo hapo!

Nikaja kuagiza vifaranga 500 walikufa 17 ikawa kinyume chake hadi nauza nilikuwa na kuku 478. (Wengine nilikuwa najipongeza)

Na niliuza Kwa 18,000/=Kila kuku bei ya load wanaita.

Ndani ya miezi 4 na wiki3 tu walikuwa kroiler na nilinunua AKM huko huko Daslam .

Kwenye kupambana tegemea lolote. Visa kadhaa nitakuwa naleta Kwa comment hapo chini

Ahsanteni.

View attachment 3050886View attachment 3050892
Kazi nzuri.

Umesahau jambo Moja kwamba tumezaliwa tofauti , wengine mna Ile spirit ya upambanaji by nature na wengine wanajifunza kwenu na wengine wao huridhika tuu.

Sasa maisha Yako hivyo haitakuja kutokea watu wakafanana ,ndio sababu Matajiri na Viongozi Huwa wachache.
 
Uhakika mkuu. Umenena vyema
Kazi nzuri.

Umesahau jambo Moja kwamba tumezaliwa tofauti , wengine mna Ile spirit ya upambanaji by nature na wengine wanajifunza kwenu na wengine wao huridhika tuu.

Sasa maisha Yako hivyo haitakuja kutokea watu wakafanana ,ndio sababu Matajiri na Viongozi Huwa wachache.
 
Sorry, Naombeni site ya kudownload full movie free za makampuni ya movie kama universal pictures
 
Usisambae sana mapema
Kama nyama zinalipa jikite kwenye nyanya tu

Usifanye diversity mapema concentrate kwenye hiyo nyanya inalipa

Nyanza imeonyesha faida ya milioni 9 faida kwa mwezi endelea na Nyanya tu kwa miaka mitano mfukulizo kabla ku divesfy expand ekari za Nyanya ni mapema mno kufanya diversification kama Nyanya inalipa fanya diversification after five years kama profit ya nyanya iko consistent for all those five years

Ku diversity kwenye business huhitaji utulivu wa akili za kibiashara don't rush

Hata uki diversify hiyo new business ipe at least five years huku una nyanya na huku una hiyo new business ukiziangalia zote before diversifying kwenye product ingine ya tatu

Usione akina Azam wana Products nyingi Azam food,Azam Marine,Azam Media na Azam Sport nk diversification haiendi mbio kama fast food kukaangiwa chips kuku chap chap

Diversification ni serious business consideration
Hili swala mimi linanishangaza mno kuna dogo alilima nyanya miche 7000 akapiga milion 11 sasa chakushangaza anadai halimi nyanya anataka kulima tikiti
 
Muongo huyuu limeni lakin msifuate maneno Yake et wanyarwanda..!! Sijui mil 15
 
achana na nyanya.
Mkuu Mimi NI OP vipi kazi za excavator huko?
 
Eneo lilipo shamba ni wapi? Na gharama za kukodi kwa eka ni zipi? Pia malipo ya vijana wa kazi ni yapi? Asante.
 
Kilimo cha nyanya kinalipa ukikipatia ni kama matikiti😁
 
Back
Top Bottom