Nimemcheki Samatta kwenye Game ya Genk vs Anderletch. Samatta hana uwezo wa kucheza England

Umeanza kumcheki kwenye game ngapi?au hii ndiyo yakwanza?Kabla hujaandika ulitakiwa umcheki walau game 3 ndio utuambie
 
Pia mkumbuke kwenye mexhi hiyo ndio aliweka kimiani goli LA ushindi.na kwenye top scorers yupo namba 2 akiwa na magoli 4 nyuma ya kinara mwenye ,5
 

Nimekuelewa. Ila vichwa maji vya Kibongo havitoelewa. Na utapoteza nguvu nyingi kujaribu kuwaelewesha bora uwaache tu.
 
pole shabiki mwenzangu wa manjesta... Leo tumlaumu nan?
 
Tunamshukuru raisi Magu kwa Sammata kufanya vizuri uko majuu, Samatta anatekeleza ipasavyo ilani ya ccm.
 
Si sawa kumukumu kwa mechi moja ukizingatia mwaka jana ndo kawa mfungaji bora. Aubemeyang mwaka jana mechi dhidi ya liverpool aligusa mpira mata 13 tu ndani ya dakika 71 alizocheza. Tena kati ya hizo mara 6 ilikua ni wakati wa kuanzisha mpira katikati. Lakini hiyo haikumfanya kuonekana kuwa hana uwezo wa kucheza hapo England
 

Genk wanapitia kipindi cha mpito baada ya Kocha wao P. Clement kujiunga na Club Brugie (Makamu Bingwa). Kila mchezaji pale Genk bado anajaribu kuzoea mbinu na mfumo we kocha mpya F. Mazzu hivyo ni vyema kumpa muda pia Mbwana Samatta.

Ahsante
 
Ile team 900 toka simiyu inamuurika samatta kwa uzi huu
 
Kuna aina tofauti tofauti za strikers...

Si lazima uwe na nguvu kama Drogba, mbwembwe kama Messi au mbio kama Ronaldo...

Wapo wafungaji wanaojulikana kama goal poachers, yaani wao uwanjani hawana mbwembwe isipokuwa wanajua mno kukaa maeneo yanayowarahisishia kufunga...

Mathalani unawakumbuka watu kama Mateja Kezman, Mario Jardel, Dwight Yorke, Tore Andy Flo, Ruud Van Nisterlooy, Roy Makaay n.k ni aina ya washambuliaji hawakuwa na pilika nyingi ila wao ilikuwa ni kujiposition panapotakiwa na kutupia tu

Kazi ya striker ni kufunga na kashafanya hivyo mara kibao, kafanya akiwa Mazembe na sasa Genk hivyo Samatta anaweza akacheza ligi yoyote Ulaya....
 
Acheni roho za korosho,kufanya vizuri kunaendeana na mapenzi ya Mungu.
 
Mleta mada ni aina ya mashabiki walioujulia mpira kupitia Messi au Ronaldo,wanadhani kila striker atakuwa wa aina hiyo.
 
Asome hapa kwa faida yake ubongoni.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…