Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Mi sijaoa, bado msela
Huna kosa kisheria kama mwanamke haku declare kua yeye ni mke wa mtu na ww hukujua kama ni mke wa mtu lakin you need to prove beyond reasonable doubt. Pia itategemea jamaa ata formulate vipi kesi yake.
Njia pekee ya kumaliza swala hili ni kupatana na huyo mwenye mke.
Mueleze kila kitu, yaani tukio zima ili aelewe, na upatane nae, bila kujali kama ana ugomvi na mkewe.
Maana, huwezi kujua jamaa atachukua maamuzi gani, kwani kama ana ugomvi na mkewe, basi wewe ndio unaonekana kuwa ndio chanzo, au ndio unazidi kuchochea na kuingilia ndoa yao.
Hivyo kupatana nae na kumwomba msamaha ndio suluhisho la mkasa huu na inaweza kuwa ndio mwanzo wa yeye kupatana na mkewe.
Huu ni ushauri wangu tu, maamuzi ya mwisho ni yako mwenyewe.
Mkuu, asante sana...pamoja na kumweleza kuwa mkewe ndiye alitenifool kutoniambia ukweli kama ana mume, pamoja na mkewe kumweleza kuwa yeye ndio alinianza na kunificha kama ameolewa...Lakini jamaa hataki kusikia na anachosema ni kunipeleka mahakani. Kwa sasa mke hamtaki kbs mume wake.
Nimekuja kutaka msaada coz kuna mishe moja naanza kuifanya this month au baadae mwezi ujao, nahisi kama atanipeleka mahakamani nitapoteza baadhi ya mambo yangu..
Wewe jitahidi sana upatane naye, hakuna mtu asiyetaka suluhu.
Tumia watu wake wa karibu, wamshauri na kumsihi kuwa unataka suluhu, ataelewa tu.
Tumia watu kama hao kutoka upande wako pia, itasaidia sana.
Tafuta suluhu hii kwa bidii sana maana hakuna njia nyingine ninayoiona hapa.
Mkuu, asante sana...pamoja na kumweleza kuwa mkewe ndiye alitenifool kutoniambia ukweli kama ana mume, pamoja na mkewe kumweleza kuwa yeye ndio alinianza na kunificha kama ameolewa...Lakini jamaa hataki kusikia na anachosema ni kunipeleka mahakani. Kwa sasa mke hamtaki kbs mume wake.
Nimekuja kutaka msaada coz kuna mishe moja naanza kuifanya this month au baadae mwezi ujao, nahisi kama atanipeleka mahakamani nitapoteza baadhi ya mambo yangu..
Usiogope hata kidogo huna kosa, hujabaka wala kumrubuni kimapenzi ni yeye kakufuata kwa hiari yake. Wewe endelea na mishemishe zako usijipe stress hata kidogo huna kosa kisheria. Nimeshuhudia kesi kama hii jamaa aliachiwa huru. Ila walipimwa DNA test confirm kama mtoto ni wake baada ya confirmation jamaa aliambiwa na mahakama kua ahudumie mtoto.
Nahisi kisheria huenda ukafaulu,ila mkuu umejiandaaje na kupigwa kipapai!
Maswala ya mimba yanauma sana!au uko fiti!
Najua inauma sana na hata ningelijua kabla kuwa ni mke wa mtu nisingefanya huo ujinga...
Zaidi ya kunipeleka mahakamani sifikiri kama kuna kingine anaweza kunifanya labda aniloge
Mamahakani utautoa huo ushahidi Kama Kweli mwanamke ndo aliyekutongoza wewe uone Kama huo utetezi utakutoa. Ni bora ukomae tu kwamba hakuwahi kukuambia Kama kaolewa kuliko kudai alikutongoza kwa nini hukukataa?
Habari zenu wanajukwaa.
Sakata hili limenitokea karibuni kibaya zaidi mumewe akajua mimba ni yangu...Sasa jamaa ananitafuta na kutaka kunishtaki, je nina mashtaka ya kujibu
Kama uyasemayo ni kweli basi leo nitalala usingizi mzito sana
Mi naona michango mingi ni kumpa mwongozp huyo mzinzi. Na je mbona hamjatoa mawazo kuhusu maisha ya mtoto huyo atakaezaliwa??