Nimempiga mtoto wa mdogo wangu, ndugu wananilaumu lakini Mama ananiunga mkono

Nimempiga mtoto wa mdogo wangu, ndugu wananilaumu lakini Mama ananiunga mkono

Chizi Maarifa

JF-Expert Member
Joined
Jul 29, 2013
Posts
10,931
Reaction score
24,816
Huyu mdogo wangu wa kike wa mwisho ana kitoto chake kina miaka 6. Weekend hii alikileta kije msalimia uncle. Mi sikuona shida kabisa. Wazo lilikuwa jema.

Shida ikawa kwenye utekelezaji. Kile ki uncle kina kera balaa... Kinakera mpaka mwisho. Kimefika home ndani ya muda mfupi kimeshaingia vyumba vyote, kimechafua kwenye friji na kimeshavunja jug la juice.

Mi niliweka pause tu kwanza kuvumilia nikiomba Mungu asaidie wageni waondoke haraka. Kikaanza kulilia remote kiangalie tamthiliya za A**m. Mimi nilishapiga marufuku pale home. Nikakikatalia ...kikaanza kulia. Mama yake anakimbembeleza....

Hakitaki kikamrushia remote usoni. Hapo nilitaka kunyanyuka....malaika akanizuia. Mama yake akawa tu anasema "Jamaani... Amran na hasira kama baba yake....yaani huyu mtoto" huku anajichekesha akifikicha fikicha jicho.

Nikainuka nikaichukua remote nikaijaribu nikaona inafanya kazi. Nikashusha pumzi kumshukuru Mungu maana nilijua pale hali ya hewa ingechafuka.

Kakawa kana mghasi sana mwanangu....uzalendo ulinishinda kalipomwambia "mshenzi weeee" hapo nilijikuta nimeamka nikakamata na kukapeleka uani. Nikavunja ua langu zuri maskini nipate fimbo. Nilikatandika sana... Heeehhh .... Si kanalia kananambia ... "Toka hapa...." Nikaona haka kametumwa kunitafutia kesi na Serikali au ustawi wa jamii....

Nikakacharaza viboko miguuni, mamaa yake akaja ...na kudai inatosha nitamuumiza mwanaye si vizuri kumchapa mtoto, inatakiwa kukaa naye kuongea naye.

Nilimwambia hilo la kukaa naye kuongea naye akafanyie huko kwao. Hapa kwa uncle katulie hasa. Mama yake ali mind. Eti....mtoto anapaswa apewe muda wa kucheza atakavyo. Nilimwambia akacheze huko ila asichezee vitu vyangu na sitaki kabisa uharibifu.

Akasema: "Kaka ndo maana wengi hatupendi kuja kwako ...mkoloni sana na hupendi watoto" alinikwaza....yaani yeye kukilea kitoto chake vile kama kimbwa koko anaona ndo mapenzi. Kitoto kina sugu, vidonda na kimekuwa cheusi, kimekauka kama kinakula cement eti ndo anakipenda nikasema wacha iwe hivyo.

Kimekaa kaa kidogo kwa utulivu kikajisahau tena ...kikajikojolea.... Mtoto wa miaka 6 anajikojoleaje? Mimi wangu ameanza kukojoa mwenyewe akiwa na miaka 2 huyu sita anakojolea carpet?

Mama yake anasema ndo alivyo yaani ...ukichelewa tu kumvua nguo anajikojolea hapendi kukaa na mkojo. NIlimwita mtoto wangu nikamwambia niitie dada. Dada alipokuja nikamwambia kanichumie fimbo.

Sister akaamua akachukue katoto kake akakapeleka kwenye gari kukaepusha na dhahama. Wakaamua kuondoka. Nikasema na iwe hivyo...alaaaah yaani kafanye ujinga nikaogope sababu ya mama yake.....sister kawaambia wadogo zangu wengine kuwa nime mnyanyasa mtoto wake. Ndugu wananisema....mama akapata taarifa.

Akanipigia simu kuwa nimefanya swadakta kile kitoto kinalelewa hovyo. Mama yake anakikiss mpaka ulimi.....anasema ndo mapenzi kwa mtoto. Mama anasema hataki hata kikamtembelee kilimtia hasara nyingi ikiwepo kudumbukiza simu yake majini.

Nimejisemea tu wacha na iwe. Asiyefunzwa na mamaye sisi tutamfunza tu ...
 
Mzee bora huyo. Aisee mimi mke wangu wapili si nilimkuta na mtoto wa kiume. Pumbavu zangu. Dogo alikuwa ni nunda hatari, alikuwa anamkata mama mikwara kwa kwenda mbele, anaamua yeye kila kitu na alipojichanganya eti akasema yeye ndo mwenye maamuzi ya tunachotakiwa kufanya.

Pumbavu, dogo siku moja kanitunishia misuli kama vile anataka kupigana na mimi. Nilichofanya nilimpa wiki kama tatu hivi namsoma tu taratibu. Mama yake anamuogopa dogo plus aibu. Yaani dogo alikuwa ni kufoka tu, hasikilizi chochote. Mtoto wa kiume mama miaka sita eti mama anambeba kama wa mwaka mmoja.

Nilipoanza kazi, alisoma namba. Nilijisemea eti namkaza mama yake alafu anitunishie misuli. Daadeki, leo akisikia nimekohoa anakimbia tu. Single mothers wanaharibu watoto sana.

Siku hizi dogo anajielewa freshi kweli. Ni baada ya mimi kusimamia show kama mwanaume. Ila ajabu sikuwahi kumchapa hata siku moja.
 
Hata kama umekwazika bado unatakiwa kuulinda utu wa mtu na heshima yake, sio "kile kitoto" ni "yule mtoto". Mtoto bado ni mtu na kuwa mtundu au kukosa adabu hakumuondolei heshima ya utu wake

Mkuu haya matukio ya hivi yapo karibu kila nyumba, kila mtu akiyaleta humu asijui patakuwaje. Hongera kwa kuwajibika kuwapa nidhamu watoto wenu na ndio jukumu lako kama mtu mzima, usilalamike pambana.
 
Mzee bora huyo. Aisee mimi mke wangu wapili si nilimkuta na mwanaume wa kiume. Pumbavu zangu. Dogo alikuwa ni nunda hatari, alikuwa anamkata mama mikwara kwa kwenda mbele, anaamua yeye kila kitu na alipojichanganya eti akasema yeye ndo mwenye maamuzi ya tunachotakiwa kufanya.
Mzee unamiliki K mbili home kabisa? Hongera
 
Hata kama umekwazika bado unatakiwa kuulinda utu wa mtu na heshima yake, sio "kile kitoto" ni "yule mtoto". Mtoto bado ni mtu na kuwa mtundu au kukosa adabu hakumuondolei heshima ya utu wake

Mkuu haya matukio ya hivi yapo karibu kila nyumba, kila mtu akiyaleta humu asijui patakuwaje. Hongera kwa kuwajibika kuwapa nidhamu watoto wenu na ndio jukumu lako kama mtu mzima, usilalamike pambana.
Huoni kuwa hiyo ni staili ya uandishi tu?
Wanavyofundisha fasihi, ulisinzia?
 
Huoni kuwa hiyo ni staili ya uandishi tu?
Wanavyofundisha fasihi, ulisinzia?
Angalia dhamira ya nini anataka kuwasilisha alafu unambie fasihi unayoisema ili kupunguza uzito wa maneni aliyotumia kama ni sahihi
 
  • Thanks
Reactions: Cyb
Huyu mdogo wangu wa kike wa mwisho ana kitoto chake kina miaka 6. Weekend hii alikileta kije msalimia uncle. Mi sikuona shida kabisa. Wazo lilikuwa jema.

Shida ikawa kwenye utekelezaji. Kile ki uncle kina kera balaa... Kinakera mpaka mwisho. Kimefika home ndani ya muda mfupi kimeshaingia vyumba vyote,kimechafua kwenye friji na kimeshavunja jug la juice.
Nina mtoto wangu wa kiume ana miaka 3 sasa, anajua kila kitu, ukichukia anajua, kama hutaki afanye kitu fulani anajua, na ana limits zote, ninampenda ila pia namuadibisha hadi amekuwa na adabu.

penye haki yake anaelewa na anamind, ila pale anapoharibu nikisema aache anachosumbua huwa siongei sauti mbili, mwenyewe utakuta ameacha na kutulia. kulea mtoto kama mjinga ni kumharibu tu.
 
Nililetewa mtoto wa sista nikae nae ameenda kozi ,kalikua kakojozi kameacha,kalikua hakajui hata kula kanalishwa mwenye kanakula sasa hivi tena anakula mpk wanamshangaaa,anacheza vzr na ananenepa.Mama ake haamini mtoto wa miaka 6 hajui chochote!

Kuna wazazi wanalea watoto kama hakuna kesho!!Mimi binafsi malezi ya kudekezq kizembe sinaga ,kuna Siku tumeenda kwenye sherehe kuna mtoto akawa analilia nyama jikoni wakawa wanamchekeq na wakampa..nilikaa kimya lakini nkasema moyoni angekua wangu angeimba aleluya!!!
 
Huyu mdogo wangu wa kike wa mwisho ana kitoto chake kina miaka 6. Weekend hii alikileta kije msalimia uncle. Mi sikuona shida kabisa. Wazo lilikuwa jema.
Mkuu we acha mimi kuna mtu yuko hapa kwangu na mwanae mwezi wa tatu ninavumilia mengi, mtoto anaelekea miaka saba akiamua anajikojolea, ikifka muda wa kula eti anaanza kulia, anaweza amgomee kwenda kulala hata saa sita usku.
Yani kuna muda uvumilivu unataka kunishinda. Mwanangu uwa anataka kuiga, namtia kerebu
 
Huyu mdogo wangu wa kike wa mwisho ana kitoto chake kina miaka 6. Weekend hii alikileta kije msalimia uncle. Mi sikuona shida kabisa. Wazo lilikuwa jema.

Shida ikawa kwenye utekelezaji. Kile ki uncle kina kera balaa... Kinakera mpaka mwisho. Kimefika home ndani ya muda mfupi kimeshaingia vyumba vyote,kimechafua kwenye friji na kimeshavunja jug la juice.
Kimbwa kikoko [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Back
Top Bottom