Nimemshangaa sana aliyesema hapa JF kuwa Waziri Ulega hajui Kiingereza na katutia Aibu Watanzania kwani amejitahidi na kueleweka vyema tu

Nimemshangaa sana aliyesema hapa JF kuwa Waziri Ulega hajui Kiingereza na katutia Aibu Watanzania kwani amejitahidi na kueleweka vyema tu

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2013
Posts
60,660
Reaction score
121,325
Simkubali kutokana na Uchawa wake na Kofia aliyoivaa ikiwa na Herufi Kero fulani fulani Kwangu ila nimemsikiliza Kiingereza alichokiongea na niseme tu amejitahidi na kaeleweka. Halafu huwa nawashangaa sana Watanzania tunaacha Kujivunia lugha yetu adhimu na pendwa Afrika na Duniani kwa sasa ya Kiswahili tuko busy Kuchekana na Kutambiana kwa mmoja Kutokujua au Kuchapia Lugha ya Kiingereza. Ukimkuta huyo anayejivunia hicho Kiingereza na kuangalia Maisha yake unaweza hata Ukalia na Kumuonea huruma.

Tujifunze Kiingereza na Lugha zingine kama tu ziada ila tusijifunze Kiingereza ili tukijue na tuje tuwadharau Wasiojua Oky?
 
Back
Top Bottom