MchunguZI
JF-Expert Member
- Jun 14, 2008
- 4,011
- 2,185
Anasema hata kama una matatizo na Mh. Samia kuwa rais au yeye (Januari) kuwa waziri tutafute jambo jingine siyo mambo ya nje. Hii ndiyo rubbish ya Januari. Katika mjadala ule hakuna aliyemshambulia rais Samia. Januari anaanza kueleza underperfomance ya wizara anayoiongoza.
TANESCO iko chini yake, sababu anazotaja za waya zilizo uchi, vikombe vilivyopasuka au kVA 11 na 33 hayo ni yake na TANESCO, hakuna anayewasaidia au aliyewasaidia kuzifunga nyaya hizo. Kama ni makosa ni yao na sisi hayatuhusu. Huo ndo udhaifu wa TANESCO yake au watu wa TANESCO na waiziri wao.
Swali kwake Januari; Rais Samia ameingiaje hapo? Au ni mbinu ya kujilinda udhaifu wake usisemwe? Au ni kutuonesha kwamba yeye na rais Samia ni mwili mmoja? Anapohitaji miaka minne kama Kalemani, nini faida ya kumuondoa Kalemani na yeye aje kuomba miaka 4?
Hisia yangi ni kwamba hatfika kokote hata akariri majina ya vifaa vyote vya Tanesco na Hydro ya Nyerere ijayo, wizara hii apewe mwenye uwezo.
TANESCO iko chini yake, sababu anazotaja za waya zilizo uchi, vikombe vilivyopasuka au kVA 11 na 33 hayo ni yake na TANESCO, hakuna anayewasaidia au aliyewasaidia kuzifunga nyaya hizo. Kama ni makosa ni yao na sisi hayatuhusu. Huo ndo udhaifu wa TANESCO yake au watu wa TANESCO na waiziri wao.
Swali kwake Januari; Rais Samia ameingiaje hapo? Au ni mbinu ya kujilinda udhaifu wake usisemwe? Au ni kutuonesha kwamba yeye na rais Samia ni mwili mmoja? Anapohitaji miaka minne kama Kalemani, nini faida ya kumuondoa Kalemani na yeye aje kuomba miaka 4?
Hisia yangi ni kwamba hatfika kokote hata akariri majina ya vifaa vyote vya Tanesco na Hydro ya Nyerere ijayo, wizara hii apewe mwenye uwezo.