Nimemsikiliza Mkurugenzi wa kituo cha uwekezaji Tanzania (TIC) na mipango ya kuinua uwekezaji hakika nimefarijika sana

Nimemsikiliza Mkurugenzi wa kituo cha uwekezaji Tanzania (TIC) na mipango ya kuinua uwekezaji hakika nimefarijika sana

Kama ni hivyo, kwa nini DPW na TICTS zinagombea bandari ya Dar es salaam bila kuhusisha TIC? 😲
 
Leo nilikuwa nafuatilia mahojiano katika channel ya Zamaradi TV kati ya mtangazaji na Mkurugenzi wa kituo cha uwekezaji Tanzania ndg Gilead Teri. Katika mahojiano hayo, Mkurugenzi alijikita zaidi katika kuangazia mageuzi makubwa yanayofanywa na kituo hicho na zaidi namna wanavyotembea kwenye ndoto na maono ya Rais Samia katika kuona uwekezaji unakuwa nguzo kubwa ya kukuza uchumi wa nchi yetu. Mambo ambayo yamenifariji na naamini wale wenye ndoto ya kuwekeza watajifunza ni kama ifuatavyo;

1. Kuwawezesha wawekezaji kuanza kutumia mtaji wao wa uwekezaji bila kulipia Kodi ya VAT na badala yake mwekezaji anaweza kulipia ndani ya miezi 36. Ametolea mfano wa kichwa/vichwa vya roli kwamba mwekezaji anaweza akaanza shughuli za usafirishaji na akizalisha ndani ya muda uliopangwa atawasilisha/kulipia kodi ya VAT. Hii imeleta/italeta unafuu kwa wawekezaji na haya ndio mazingira wezeshi yanayopigiwa kelele kila siku na wadau na Kwa hatua hii, hakika uwekezaji utaongezeka sana ndani ya nchi yetu.

2. Kufanya vikao vya mara Kwa mara na wadau waliopo kwenye mnyororo wa uwekezaji kama vile TBS, TRA n.k. Lengo ni kuchochea ufanyikaji wa tathmini na kupunguza mlolongo wa vikwazo katika uwekezaji na hakika ni hatua nzuri katika kuchochea uwekezaji nchini.

3. Kuwatambua na kiwaunganisha wawekezaji wa ndani wenye nia ya kushirikiana na wawekezaji toka nje pindi wakijitokeza katika eneo la uwekezaji lonalofanana.

4. Katika kuyaongea haya alikuwa akiirejea Sheria ya uwekezaji Tanzania iliyotungwa na bunge ya mwaka 2022. Hii Sheria nitaiweka kama attachment ili kila anayetaka kuifahamu iwe rahisi kwake.

Yapo mengi sana mazuri yaliyoongelewa na kwa kifupi haya ni baadhi tu kwa leo. Asante sana Rais Samia na serikali kwa ujumla kwa jitihada za kuendeleza uwekezaji wenye tija Tanzania, asante TIC.
Wabongo vichwa maji sana! Makelele mengi vitendo zero!
 
Katika watanzania Rais Samia alipatia kuwapa nafasi eneo sahihi ni Gilead Teri. Ana maono,bidii na unyenyekevu wa kusaidia uwekezaji ndani na nje ya Tanzania na anafanya kazi nzuri. Mungu amsaidie kuutumia ujana na nafasi yake kwa uaminifu na kwa maslahi ya wengi.
Hakika, anastahili kuwa mahali alipo
 
Wawekezaji wa ndani wameshindwa kuwapa nishati ya uhakika umeme, ndio wataweza kuwavutia Wawekezaji wa nje waje kuwekeza?

NCHI YA AJABU KUWAHI TOKEA.

KaziKweliKweli/JobTrueTrue
Nchi hii imetoka mbali. Lazima tujifunze kureconize hata hatua chache kuelekea nyingi ambazo serikali imefanya. Kumbuka idadi ya watu waliounganishiwa umeme si sawa na Ile ya enzi za Mkapa pia matumizi yameongezeka na hivyo kuongeza changamoto ambayo kimsingi hatua zinaendelea kuchukuliwa siku hadi siku. Mwisho jielekeze katika kujikumbusha kuwa maendeleo ni mchakato.
 
Nchi hii imetoka mbali. Lazima tujifunze kureconize hata hatua chache kuelekea nyingi ambazo serikali imefanya. Kumbuka idadi ya watu waliounganishiwa umeme si sawa na Ile ya enzi za Mkapa pia matumizi yameongezeka na hivyo kuongeza changamoto ambayo kimsingi hatua zinaendelea kuchukuliwa siku hadi siku. Mwisho jielekeze katika kujikumbusha kuwa maendeleo ni mchakato.
Hakuna aliekataa, ila kwanini tunadanganywa kilasiku kuwa umeme utakuwa Stable na mwisho wa siku hamna kitu zaidi ya mgao.?

UKWELI NI JAMBO JEMA KWA WANANCHI, WATUAMBIE UKWELI.
 
Hakuna aliekataa, ila kwanini tunadanganywa kilasiku kuwa umeme utakuwa Stable na mwisho wa siku hamna kitu zaidi ya mgao.?

UKWELI NI JAMBO JEMA KWA WANANCHI, WATUAMBIE UKWELI.
Serikali ina namna yake ya kufanya mambo yake. Tuipe muda kwani naamini hakuna kiongozi anafurahia mgao wa umeme na mateso dhidi ya wananchi wake. Juzi tu mh Rais ametoka kuelezea mchakato wa til 4 ambazo ameanza kuzitoa katika wizara ya nishati ili kukabiliana changamoto ya upatikanaji wa umeme
 
Serikali ina namna yake ya kufanya mambo yake. Tuipe muda kwani naamini hakuna kiongozi anafurahia mgao wa umeme na mateso dhidi ya wananchi wake. Juzi tu mh Rais ametoka kuelezea mchakato wa til 4 ambazo ameanza kuzitoa katika wizara ya nishati ili kukabiliana changamoto ya upatikanaji wa umeme
Umeelewa lakini nilichokiandika Mkuu?
 
Back
Top Bottom