Nimemsikiliza Padre Kitima, hoja zake zimejikita kwenye hofu zaidi sijaona kipengele kibaya kwenye mkataba

Bams vipi kaka?!!!

Kwa hiyo Tanzania hakuna wanasheria nguli kwa sababu tu unaamini "dola" inazichezea mahakama?!!!

Kama ndivyo tunajadili nini sasa nasi hatuko huko mataifa uliyoyasema?!!![emoji1787][emoji1787]

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
Nimesoma MoU kwa kurudia mara 3.
Nimegundua watanzania wengi ni wavivu wa kusoma kwa umakini.
Wanapenda zaidi kusimuliwa hata kama kuna chumvi.
Huyu msomi hakuna alichoongea cha maana saanaaa zaidi ya kuyarejea mawazo ya jumla kama ilivyo mtandaoni.
Msomi yupi ?!!!

Mwanasheria mweka uzi ?!!!

Kama ndiye ,unatanguliza choyo ,wivu na husuda kwa kushindwa hata kumpa KONGOLE kwa kizuri alichoandika na kukimbilia kujificha kuwa tuwavivu wa kusoma na ameyakusanya mitandaoni ?!!!![emoji15][emoji15][emoji15][emoji1787][emoji1787]

Duuuh hatari sana [emoji1787][emoji1787]

#MamaAnaupigaMwingi[emoji7][emoji7]

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
Huenda unamjibu mpagani sugu🤣
 
Ukuu wa wilaya hupati kabisa kabisa
Ningeweka namba zangu hapa basi ningekuwa nautaka huo ukuu wa wilaya.

Natumia fake Id na hata siku moja sijawahi reveal my true identity humu. Sasa nitaupataje huo ukuu wa wilaya?
 
Kwanza wewe umekuja hoja mpya.

Mimi thread yangu imejikita kwenye hoja za Padre wangu Kitima. Sio hoja zako

Sasa ngoja nirudi kwenye hoja zako
Kuhusu IGA kutokuwa na muda wa ukomo, unajua maana halisi ya hii IGA? Unajua tofauti baina ya IGA na HGA?
Huu ni mkataba unaofungua nafasi ya kuingia kwa mikataba mingine kwenye maeneo husika ( Specific areas) kwa hiyo unamaanisha IGA ingekuwa na ukomo alafu tena mkataba kuhusu eneo specific pia uwekewe ukomo? Nini logic ya kufanya hivyo?

Alafu kifungu cha 5 kisome vizuri. Exclusive right inayozungumziwa ni kuhusu ku endeleza, kusimamia na kufanya kazi eneo la mradi (project) kama ilivyoanishwa katika apendix 1. Sasa hapo shida ipo wapi? Mwekezaji kuendeleza na kusimamia eneo la mradi kuna shida gani?

Kuhusu Je ni ninaamini kama miradi itaisha wakati IGA imetoa fursa ya kubuni maeneo mengine ya uwekezaji sijaelewa hapa shida iko wapi? Labda ungedadavua vizuri zaidi? Maana kwa mujibu wa mkataba sisi tutawataarifu tu kuhusu fursa , mkataba hausemi lazima tuwape izo fursa sasa sijui shida iko wapi?

Kuhusu Serikali kurithishana mkataba sijaelewa hofu yako iko wapi? Hili ni jambo la kawaida sana kwenye mikataba ya namna hii ya sio mara ya kwanza kufanyika. Huwa linafanyika impliedly na hata likiwekwa kimaandishi sioni shida yeyote.

Nikupe mfano. Serikali yetu iliingia makubaliano na China kujengewa reli ya Tazara na ilikuwa kipindi cha Mwalimu. Makubaliano yale yameendelea kuheshimiwa na kurithiwa na awamu zingine hadi sasa .

Pia kipindi cha Magufuli tulikopa madeni mbalimbali na pamoja na Serikali ya magufuli kuondoka Serikali ya Samia imerithi hayo madeni na inaendelea kuyalipa. Sasa nieleweshe wewe hapo shida iko wapi?
 

Safi sana
 


Mwanasheria Huyu hapa, wewe ni mtu wa hovyo :

 
Ningeweka namba zangu hapa basi ningekuwa nautaka huo ukuu wa wilaya.

Natumia fake Id na hata siku moja sijawahi reveal my true identity humu. Sasa nitaupataje huo ukuu wa wilaya?
Uchawa acha we bado kijana mambo ya unafiki noo
 
Wewe huwezi kukubali kama amepangua hoja zako au la, wengine tunaona amepangua!
 
Waarabu ni washenzi hawa majangili

Wamehonga wabunge ili wauze nchi

Never let's say they won for while
 
Waarabu ni washenzi hawa majangili

Wamehonga wabunge ili wauze nchi

Never let's say they won for while
Kumbe shida ni wawekezaji kuwa waarabu?

Sijaona sehemu wabunge wameuza nchi labda utusaidiaje na kwa ushahidi? Wameuzaje?
 
utajaribu kutetea sana hata kama ni mwanasheri kwanza tanzania hatuna wanasheria tuna wababaishaji wa sheria tu.ukweli utakuja fahamika na mtaumbuka kweupe na mtashindwa kuzificha nyuso zenu.time will tell.
 
Kumbe shida ni wawekezaji kuwa waarabu?

Sijaona sehemu wabunge wameuza nchi labda utusaidiaje na kwa ushahidi? Wameuzaje?
hakuna mtu aliyesema shida ni waarabu na kama wewe umeona hivyo basi na wewe unaenda kwa hisia tu.
 
Uelewa wako ni mdogo sana. Kama umeshindwa kumuelewa Kitima unatia mashaka sana. Kitima ametoa facts dhidi ya propaganda na uongo wa CCM kuhusu maktaba. Mkataba huu unamadhara makubwa sana kwa taifa but huenda ukawa na faida mwa CCM ya wachache.
 
Uelewa wako ni mdogo sana. Kama umeshindwa kumuelewa Kitima unatia mashaka sana. Kitima ametoa facts dhidi ya propaganda na uongo wa CCM kuhusu maktaba. Mkataba huu unamadhara makubwa sana kwa taifa but huenda ukawa na faida mwa CCM ya wachache.
Isitoshe Dubai siyo nchi (state) hivyo haiwezi kuingia mkataba wa kimaifa (IGA - kati ya nchi na nchi). Mkataba unapaswa kuwa baina yake au DPW ns TPA.

Bunge lisiridhie kutunga sheria ya kuupa nguvu ya utekelezaji
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…