Nimemsomesha, nimegharamika, leo kaniacha anaolewa na mtu mwingine

Nimemsomesha, nimegharamika, leo kaniacha anaolewa na mtu mwingine

Pole sana mkuu hapa ndo naamini ule msemo unaosema Mchumba hasomeshwi. Utakuja kula sumu bure. Na kazi ya kumuaanda MKE ni ya MUNGU PEKEE ww unaanda mazingira tu piga moyo konde maisha lazima yaendelee.. Usichoke kumuomba MUNGU NI MWAMINIFU anaandaa ushuhuda wako.
 
Sikujua laiti ningejua.... Najuta

Wakuu nilikutana na huyu binti miaka kadhaa iliyopita mimi nikiwa nimepangiwa kazi mkoa fulani... katika mihangaiko yangu nikakutana na huyu binti nilitokea kumpenda.. mzuri kisura na kitabia...very innocent niliamini kwake nimefika baada ya kash kash nilizopitia katika mahusiano ya nyuma.

Wanasema usiusemee moyo ila najua yule binti alinipenda kidhati tena moyoni kabisa.. na mimi kwangu she was a queen na niliapa kumuoa baada ya yeye kumaliza masomo yake. Binti huyu kwao ni familia maskini nikisema familia maskini ni familia maskini kisawasawa. Baba yake alifariki miaka kadhaa nyuma kabla sijaonana nae hivyo aliishi na mama yake na wadogo zake.. ni story ndefu kuhusu familia yao. Mimi nikawa ndio kama msaada katika familia yao, sikua na hiyana na nilisaidia niwezavyo kwani binti yule nilimpenda kutoka moyoni.

Yule binti alimaliza shule na kuhitajika kwenda chuo lakini familia ikawa haina uwezo wa kumsomesha na mkopo alikosa. Akakosa raha na ikawa kama jukumu ni langu. Mama yake aliniita tushauriane kwasababu kwao nilikua nafahamika. Kwakuwa mimi nilisema nitamuoa binti wakashauri nimsomeshe kama nina nia yakweli. Uwezo wa kumsomesha nilikua nao nikakubaliana na tukaandikishana kwamba namsomesha mimi lakini mwisho wa siku yeye atakuja kuwa mke wangu na hata mahari sintolipa kwani itakua imeingia huko. Familia ilinishukuru sana kwani waliamini kusoma kwa binti itakua afadhali katika ukombozi wa maisha yao. Binti alikuwepo wakati maandikishano yanafanyika na mashahidi walikuwepo.. nakumbuka binti alilia yule akiapa kunipenda milele na mapenzi tuliyofanya siku hiyo siwezi kusahau... ilikua best sex ever.

Wakuu nifupishe binti alianza chuo kila kitu nililipa.. Nauli.. hosteli ada matumizi kila kitu ilikua mimi ,mwaka wa kwanza ukaisha vizuri mapenzi yanachanua.. likizo naenda likizo zao anakuja.. mama mtu alinishukuru sana. Mwaka. Mwaka wa pili matatizo yakaanza nikipiga sim naambiwa yuko library.mara assignment nikiuliza zaidi anakua mkali nikasema labda labda kweli shule lakini hata mimi nilisoma muda wa kuongea na mwenzi wangu nilikua nao nikasema labda shule ya sasa ni ngumu. Binti akabadilika majibu ya jeuri nikaenda kuongea na mama yake amkanye naona akajirekebishe na kweli akatulia maisha yakaendelea. Upside zikiwa chache. Mahusiano yalitawaliwa na migororo

kufupisha...Miezi kadhaa imepita binti kaniandikia meseji eti "NAKUSHAURI UTAFUTE MWANAMKE MWINGINE MIMI SIKO TAYARI KUWA NA WEWE NIKUTAKIE MAISHA MEMA"

Naandika huu uzi wakuu acha nikipiga simu haipokelewi mara haipatikani. Nikampigia mama yake kumuuliza kama anajua lolote akasema hafaham. Nikaomba likizo kazini nifatilie sikuamini siku naambiwa ana mimba na anaishi na mwanaume mwingine. nilitamani ardhi ipasuke kumbe ndio maana niliandikiwa ule ujumbe nikajiuliza maswali bila majibu... basi angefanya nisijue na mimba juu kapata inauma sana. Kumuuliza mama yake hana analonijibu, kumbe chuo kapostpone sijui anaishi na huyo mwanaume moja ya mitaa Dar.. yote hiyo nafatilia kwa baadhi ya marafiki zake. na kibaya zaidi huyo mwanaume alishamlipa tena huyo mama pesa nyingine. Na ndio kamchukua binti yake.

Nimechukia kuuziwa mbuzi kwa gunia.. Love is blind inakuwaje sikuona yote hayo?? Why me..Why.. najiuliza sipati majibu. sikuwahi kupenda kama nilivyompenda huyo binti. Nilimpenda kutoka moyoni na kujitoa kwake sijawahi kumfanyia mwanamke yoyote niliyomfanyia leo ameniacha kwenye mataa na nyodo juu.. kuna muda natamani ningekua na bastola nimsambaratishe ila that is not me. Juzi nimeona whatsup kaweka picha yake tumbo kule na namba yake nikafuta

NILICHOFANYA

Nimepeleka hii kesi mahakamani kwasababu tuliandikishana kama mke nimekosa basi nilipwe gharama zangu najua haiwezi kuziba pengo.. kufuta maumivu naona is the least i can do for my self... wakuu nifanyaje au nimekosea kupeleka shtaka polisi tumeshaitwa mara mbili hakuna mtu aliyetokea upande wao . Nimetokea kuwachukia wanawake saaaana... kwanini mnatufanyia hivi jamani tuwapende vipi. Nimekaa hapa kitandani nimewaza mawazo mengi moyo wangu kama barafu naishia kusononeka.

Sijui nimfanyie kisasi gani aumie kama mimi nilivyoumia.

Adios.
Na am sure ulishasikia girlfriend hasomeshwi. Lakini ulipuuza. Inawezekana tatizo likawa kwako hebu jaribu kujichunguza. Angalia ni mahala gani hasa mlikuwa mnatofautiana na kwanini na wewe ulireact vipi? Ulisema nini na Ulifanya nini? Alipenda nini? Kwanini unasema alikupenda? Mapenzi yenu yalitawaliwa na nini? Nafasi pesa ilikuwaje? Alikuvumilia ktk nini na wewe ulivumilia nini?

Acha kulalama trust me haisaidii kitu sana sana unajiongezea maradhi ya Moyo. Jifunze kisha songa mbele. Hakuna anehitimu elimu dunia. ILa tunashauriwa kujifunza kutoka kwa waliotangulia kukosea. Japo tunaelewa zaidi ama kujifunza zaidi kutokana na makosa yetu wenyewe. Maana gharama tunailipa wenyewe.

Jifunze kuishi na Mwanamke kiakili. Jifunze kushinda mihemuko yako. Don't put all your Eggs in one basket.

Nakutakia kila lakheri katika kujifunza kwako. Next time uje na thread ya nini umejifunza kutokana na kosa flani ulilofanya.
 
Usitumie muda wako kufuwatilia msaliti. Fanya umetoa sadaka songa mbele utarudi kushuhudia.
 
Sasa wewe gharama za KU DO huzioni? Wewe kila siku ukiwa na hamu ulikuwa unamaliza kwa huyo Binti hadhani kwanza ulikuwa unatembea na Mwanafunzi wa Secondari na unahitaji kufungwa miaka 30 maana inavyoonekana ulitumia nafasi ya kuwa Masikini huyo Binti. Je kwa nini usingesubiri afike Chuo Kikuu ndo uanze na harakati za kuoa?. Ushauri wangu, achana na hizo Pesa, tafuta maisha mengine. Watu wanaosomesha wachumba wengi hawajiamini, matokeo yake ndo hayo. Kwa kifupi, Mchumba hasomeshwi bali hupewa fedha za Snap Chips,Bager,Azam Juice,Nguo,Kusuka,au shopping. Hayo menyewe niliyoyataja ni zaidi ya kusomesha sasa uanze kusomesha Chuo atakutana na watu wanamkuna kwelikweli na wewe ulikuwa unagusa kisitaarabu!!!!!!!!!!!
 
Ndugu kama una amini katika Mungu samehe tu inabidi usamehe hili mambo yako mengine yakae sawa nakuhakikishia atakukumbuka sana Na ipo siku ataumia zaidi yako wewe ulivyoumia kila kitu anapanga Mungu Mungu kakutumia wewe kama daraja la yeye kufika mbali katika elimu Yake kama kapostpond muuombee Mungu amalizie awe msada kwa familia Yake achana Na mambo ya mahakamani Mungu kukuepusha Na mengi hawa ndio wale ukaja Kuoa aoni tabu kukuua kisa afanye mambo Yake kwa amani
 
Kumpa mimba au kumzalisha is not a solution, jamaa yangu aliachwa asubuhi saa kumi na mbili....!!

Demu kamusomesha,mwaka wa pili akamchapa mimba,demu kazaa,mwaka wa tatu wakafunga ndoa,demu karudi chuo last semester,yakaanza manyau nyau,mchizi kapigwa chini,Mtoto kapewa,demu kaolewa na jamaa mwingine...

Jamaa alikonda sana,msongo wa mawazo ukawa unamkondesha balaa,akahama na kanisa,kutoka Roman Catholic hadi now anasali kwa Kakobe....
Nadhani tatizo hasa lipo kwenye tafsiri. How do we define our happiness. Wapo ninao wafahamu ambao wameachana na wake zao waliozaa nao watoto and they are Okay with a different life style. Sio wanaume wote tutajaaliwa kuoa au kuwa na Familia. Maisha hayana guarantee anything can happen any time. It is somehow better to be prepared for the wost psychologically.

Haya Mambo yanaumiza sana. Na hakuna master. Jambo la Msingi ni kuomba Mungu kisha unasonga mbele.
 
Pole sana kaka, umeandika kwa uchungu kweli najua inavyouma lkn hakuna namna cha msingi jitahidi kuvumilia achana na hiyo kesi ya kudai gharama zako kaa kimya wanawake wapo wengi sana cha msingi achana na habari ya kubeba jukumu la mzazi next time maana unashindwa kuelewa kuwa je umependwa kwa dhati au umependwa coz ya msaada wako.

Pole sana, achana naye anza upya.
 
Pole sana mkuu...ila hata na wewe ulikosea toka mwanzo ~ungemtia mimba kwanza ili hata kama angebadilika kama hii leo ungekuwa na kafaida japo kidogo
 
Mkuu pole. Alikuwa anasoma chuo cha mji gani? Isije kuwa DSM?
 
Tatizo wanaonyesha kiburi hata mahakamani hawakanyagi. Na barua walipelekewa.Kusamehe nashindwa mkuu wangu.

Asante pia
Unashindwa vp kusamehe, hili ni jaribu kwako na unapaswa ulishinde ushasema mwenyewe kuwa hiyo familia ni maskini sasa unategemea kipindi hiki ndio wamekuwa matajiri wa kuweza kulipa gharama zako? misukosuko km hii ndio ukomavu wako kimahusiano, watu wanaacha asset km nyumba, gari na vitu vingine na kuanza maisha mapya sembuse hiyo ada na matumizi ambayo hata million 10 haifiki, hasara roho ndugu yangu, pesa makaratasi tu.
 
Mmhhh, pole sana mkuu hawa viumbe ndo walivyo ni wa ajabu sana hawana utu wanatanguliza tamaa mbele ila nadhani itakuwa fundisho kwa wengine
 
Kitu nilichojifunza;
1. Mchumba hasomeshwi.
2. Mchumba hakopeshwi hela.
3. Mchumba anunuliwi wala kupewa vitu vya thamani.
 
Mkuu nakushauri ukubaliane na matokeo, kubali kuachwa ama kutendwa na mtu uliyempenda kwa moyo wote, akili yote na the one whom you had sacrificed you whole body, love, heart and money to.
Achana na kesi hiyo itakupotezea muda tu na hela ndugu.
Madem hawa tulioumbiwa hawajitambui ndio maana hata maandiko matakatifu yanatuambia "ishini kwa akili sana na wanawake" fumbo ambalo mme hulifumbua tu punde aingiapo mgogoro na mke wake ampendae.
Pole sana mkuu, I know how much painful it's when you see your beloved one going away with her hand in the hand of another guy in the name of love. I'm the victim of such unbelievable breakup and taking a lover to school, taking care of her entire family. Pole sana mkuu, utapata mwingine don't worry.
 
Sikujua laiti ningejua.... Najuta

Wakuu nilikutana na huyu binti miaka kadhaa iliyopita mimi nikiwa nimepangiwa kazi mkoa fulani... katika mihangaiko yangu nikakutana na huyu binti nilitokea kumpenda.. mzuri kisura na kitabia...very innocent niliamini kwake nimefika baada ya kash kash nilizopitia katika mahusiano ya nyuma.

Wanasema usiusemee moyo ila najua yule binti alinipenda kidhati tena moyoni kabisa.. na mimi kwangu she was a queen na niliapa kumuoa baada ya yeye kumaliza masomo yake. Binti huyu kwao ni familia maskini nikisema familia maskini ni familia maskini kisawasawa. Baba yake alifariki miaka kadhaa nyuma kabla sijaonana nae hivyo aliishi na mama yake na wadogo zake.. ni story ndefu kuhusu familia yao. Mimi nikawa ndio kama msaada katika familia yao, sikua na hiyana na nilisaidia niwezavyo kwani binti yule nilimpenda kutoka moyoni.

Yule binti alimaliza shule na kuhitajika kwenda chuo lakini familia ikawa haina uwezo wa kumsomesha na mkopo alikosa. Akakosa raha na ikawa kama jukumu ni langu. Mama yake aliniita tushauriane kwasababu kwao nilikua nafahamika. Kwakuwa mimi nilisema nitamuoa binti wakashauri nimsomeshe kama nina nia yakweli. Uwezo wa kumsomesha nilikua nao nikakubaliana na tukaandikishana kwamba namsomesha mimi lakini mwisho wa siku yeye atakuja kuwa mke wangu na hata mahari sintolipa kwani itakua imeingia huko. Familia ilinishukuru sana kwani waliamini kusoma kwa binti itakua afadhali katika ukombozi wa maisha yao. Binti alikuwepo wakati maandikishano yanafanyika na mashahidi walikuwepo.. nakumbuka binti alilia yule akiapa kunipenda milele na mapenzi tuliyofanya siku hiyo siwezi kusahau... ilikua best sex ever.

Wakuu nifupishe binti alianza chuo kila kitu nililipa.. Nauli.. hosteli ada matumizi kila kitu ilikua mimi ,mwaka wa kwanza ukaisha vizuri mapenzi yanachanua.. likizo naenda likizo zao anakuja.. mama mtu alinishukuru sana. Mwaka. Mwaka wa pili matatizo yakaanza nikipiga sim naambiwa yuko library.mara assignment nikiuliza zaidi anakua mkali nikasema labda labda kweli shule lakini hata mimi nilisoma muda wa kuongea na mwenzi wangu nilikua nao nikasema labda shule ya sasa ni ngumu. Binti akabadilika majibu ya jeuri nikaenda kuongea na mama yake amkanye naona akajirekebishe na kweli akatulia maisha yakaendelea. Upside zikiwa chache. Mahusiano yalitawaliwa na migororo

kufupisha...Miezi kadhaa imepita binti kaniandikia meseji eti "NAKUSHAURI UTAFUTE MWANAMKE MWINGINE MIMI SIKO TAYARI KUWA NA WEWE NIKUTAKIE MAISHA MEMA"

Naandika huu uzi wakuu acha nikipiga simu haipokelewi mara haipatikani. Nikampigia mama yake kumuuliza kama anajua lolote akasema hafaham. Nikaomba likizo kazini nifatilie sikuamini siku naambiwa ana mimba na anaishi na mwanaume mwingine. nilitamani ardhi ipasuke kumbe ndio maana niliandikiwa ule ujumbe nikajiuliza maswali bila majibu... basi angefanya nisijue na mimba juu kapata inauma sana. Kumuuliza mama yake hana analonijibu, kumbe chuo kapostpone sijui anaishi na huyo mwanaume moja ya mitaa Dar.. yote hiyo nafatilia kwa baadhi ya marafiki zake. na kibaya zaidi huyo mwanaume alishamlipa tena huyo mama pesa nyingine. Na ndio kamchukua binti yake.

Nimechukia kuuziwa mbuzi kwa gunia.. Love is blind inakuwaje sikuona yote hayo?? Why me..Why.. najiuliza sipati majibu. sikuwahi kupenda kama nilivyompenda huyo binti. Nilimpenda kutoka moyoni na kujitoa kwake sijawahi kumfanyia mwanamke yoyote niliyomfanyia leo ameniacha kwenye mataa na nyodo juu.. kuna muda natamani ningekua na bastola nimsambaratishe ila that is not me. Juzi nimeona whatsup kaweka picha yake tumbo kule na namba yake nikafuta

NILICHOFANYA

Nimepeleka hii kesi mahakamani kwasababu tuliandikishana kama mke nimekosa basi nilipwe gharama zangu najua haiwezi kuziba pengo.. kufuta maumivu naona is the least i can do for my self... wakuu nifanyaje au nimekosea kupeleka shtaka polisi tumeshaitwa mara mbili hakuna mtu aliyetokea upande wao . Nimetokea kuwachukia wanawake saaaana... kwanini mnatufanyia hivi jamani tuwapende vipi. Nimekaa hapa kitandani nimewaza mawazo mengi moyo wangu kama barafu naishia kusononeka.

Sijui nimfanyie kisasi gani aumie kama mimi nilivyoumia.

Adios.
pole sana mkuu kwa yaliyokukuta kwani hawa viumbe ni hatari sana na wakiamua kufanya ktu hawogopi na wala hawajali na hawafikiri nyuma na sijui wanatumia kiungo gani kufikiria.cha kukushauri ni kwmba ktk kpndi hki kigumu jitahid kutokaa peke yako maana kufanya hvyo kunaweza kukuletea mawazo mabaya ni bora ujichanganye tu kwa marafik mkpga stori mbili tatu ,pia hata ukimshtaki sidhani kama atakuwa na mkwanja wa kukulipa cha msingi ni kumwachia mungu tu ,sku hzi malipo ni hapa hapa duniani tukifa znaendA hesabu tu.
 
Mtu masikini si mtu wa kumwamini hata kidogo
Masikini ndo wanatuumiza sana, nimesomesha, nimelisha familia ya demu wangu nikitegemea kuja kumuoa ila ile anamalizia tu kozi yake nikaambiwa piga gharama zako unadai shiling ngapi nikulipe... Aiseee ndani joto lilipanda kwa nyuzi 40 kidogo nife na hadi hapa bado unauguza majeraha moyoni japokuwa unaelekea mwezi sasa (bado siku 4 tu mwezi ukamilike).
MCHUMBA HASOMESHWI
 
Wewe shukuru amesepa mapema ungeoa labda angekuletea ukimwi. Kuhusu kusomesha ichukulie kama hasara kwenye business.
 
Wakuu asanteni sana kwa maoni na ushauri wenu... nazidi kusoma na ninaamini nitaendelea kujifunza mengi kutoka kwenu
 
Back
Top Bottom