Nimeoa wiki mbili tu zilizopita lakini tayari nimechoshwa na maisha haya

Namshakende

JF-Expert Member
Joined
Sep 23, 2021
Posts
671
Reaction score
1,644
Nimeoa wiki mbili tu zilizopita, lakini tayari nimechoshwa na maisha haya. Nahisi kama ninaishi maisha ya kipumbavu . Nashangaa jinsi watu ambao wamekuwa kwenye ndoa kwa miaka mitano au zaidi wanawezaje kuvumilia huu ujinga!

Niko kitandani na huyu Binadamu , lakini ameninunia tangu jana. Nimejaribu kuzungumza naye, lakini hataki kuonyesha ushirikiano .

Nafikiria kumfukuza arudi kwao.

Nadhani ni bora niishi peke yangu kuliko kuishi na mtu huyu.

Ninahisi kuchanganyikiwa na kukata tamaa. Je, kuna mtu yeyote anaweza kunipa ushauri?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…