Nimeona hapa ndo kuna shida kwa vijana wengi Tanzania

Nimeona hapa ndo kuna shida kwa vijana wengi Tanzania

Kuna mtu ananipaga pesa nyingi tu millions kadhaa.
Juzi nilikwama laki 4 nadaiwa.
Aiseeee ikabidi nimuingie anikopeshe.
Akanikopesha.
Lakini najua hiyo hela kwake hawezi nidai na ni hela upande wake ni ya kuspend ijumaa usiku, napengine haitoshi.
Lakini ni lazima nimlipe maana kanikopesha.


Sent using Jamii Forums mobile app
Hatari sana.

Kuna ndugu zangu fulani, kadhaa, na waliokuwa marafiki, kadhaa, nimewapoteza kwa sababu ya mikopo.

Yani unamkopesha mtu, halafu huo mkopo mdogo tu ndio unakuwa sababu anakomesha urafiki nawe, mwingine ndugu kabisa lakini kakopa, hataki kulipa, na anakukwepa kwa sababu ya mkopo. Kuna watu sijaongea nao sasa zaidi ya mwaka wa pili, kwa sababu ya mkopo mdogo tu.

Sasa hapo mtu anapata mtihani mgumu sana, mara nyingine naona bora niseme sina hela, ili mkopo usije kunikosesha ndugu, jamaa na marafiki.

Lakini mara nyingine, unaangalia mtu ana shida, unaona imani, unaamua ngoja nimpe tu, akinifanyia ubaya kutolipa ni ubaya wake yeye.
 
Mie nishakopwa na majirani wote, wanalipa wanavyojisikia wao, wengine mwaka wa tatu hawajalipa Jan. iliyopita wanakuja niwakopeshe, kwanza nikakubali ila nikamwambia anisubiri kama siku tatu, zikapita siku tatu kwenye simu ikawa kama deni! Asubuhi naamka na sms yake, lunch simu, jioni hadi usiku kwa siku mbili mfululizo, nikampigia siku ya sita kumwambia mipango yangu imefail so sitakuwa na uwezo wa kumsaidia. Kanuna balaa, jana tumekutana sehem ya manunizi ya mahitaji kajifanya hajaniona nami nikala jiwe. Kukopeshana bongo ni kuua urafiki.
True
 
Hatari sana.

Kuna ndugu zangu fulani, kadhaa, na waliokuwa marafiki, kadhaa, nimewapoteza kwa sababu ya mikopo.

Yani unamkopesha mtu, halafu huo mkopo mdogo tu ndio unakuwa sababu anakomesha urafiki nawe, mwingine ndugu kabisa lakini kakopa, hataki kulipa, na anakukwepa kwa sababu ya mkopo. Kuna watu sijaongea nao sasa zaidi ya mwaka wa pili, kwa sababu ya mkopo mdogo tu.

Sasa hapo mtu anapata mtihani mgumu sana, mara nyingine naona bora niseme sina hela, ili mkopo usije kunikosesha ndugu, jamaa na marafiki.

Lakini mara nyingine, unaangalia mtu ana shida, unaona imani, unaamua ngoja nimpe tu, akinifanyia ubaya kutolipa ni ubaya wake yeye.
Mwachie Mungu atakulipa kwa wakati wake
 
Moderators mmekuwa na chuki na threads zangu.mara nyingine mnahamishia mnakojua wenyewe.tatizo nini nilitatue? Mjiweke wazi tu.

Habarini wadau. Nlikuwa na mizunguko kidogo ya kikazi.Canada,Egypt,Sweden,South Africa na Kenya.

Nipo bongo. Nmesikitika leo kukuta jamaa wanagombana sababu ya tsh 100,000 tu.hii hii ya madafu.jamaa mmoja aliazimwa pesa hiyo sasa mwaka wa pili hajarudisha na namba akachange.leo kakutana na mdai hapa M.City. Ndo ikawa Issue.

Tunakwama sana.100,000 si pesa.si pesa ya kuvunja urafiki.lakini watanzania wengi hawajui maana ya kukopa na kuomba kupewa.

Mwaka jana nlikuwa sehemu na jamaa nmemtoa out.Hotel moja ufukweni. Naye akamwita Girfriend wake mpya amwoneshe yeye matawi.nikalipia bill yangu nikawa naaga. Jamaa akashtuka maana ndo wakati huo huyo dada amekaa tu. Mimi nliona niwaachie nafasi.
Akanambia nimsubiri anisindikize.akanifuata kwenye Jeep na kuomba nimkopeshe tsh 200,000. Atanirudishia.nikavuta draw nikahesabu nikampa.

Mwisho wa mwezi nikamkumbusha jamaa.akaanza kunambia sijui alikuwa na makato mengi na hadithi nyingi sana.nilimwambia hayo sasa yanahusiana nini na pesa yangu.akaanza kucheka cheka na kudai mimi nina pesa nisimdai hiyo 200,000.nlimwambia alikopa which means anapaswa arudishe.

Akakwepa kwepa miezi ikaisha.hakurudisha.juzi nmerudi amekwama.anataka nimkopeshe tsh 1,800,000. Nikamwambia arudishe kwanza ile 200,000. Akapita siku moja ya pili akaniletea ile pesa.

Nilipopokea nikaiwapa walinzi wagawane. Akanambia sasa inakuaje lile ombi lake. Nilimjibu tu sina.

Imekuwa issue ofisini.analalamika sana kuwa nmemfanyia ubaya.ubaya wangu ni upi hapo? Anadai namiliki magari makali lakini nmemnyima mkopo mdogo tu kama huo aongezee kweye kodi.nikashangaa sana.magari ni yangu,pesa ni yangu.sijamdhulumu why anivishe ubaya?

Vijana wa tanzania tunakwama ,tunapoteza imani,tunapoteza uaminifu kwa mambo madogo.tunapenda makuu. Siku ile nimemtoa out yeye.naye anamwita girlfriend wake...huku hana pesa.why?
Kuwa na roho safi ya kizungu kiduku lilo..... mungu atakuongezea msamehe kama unawsza msaidia msaidie kumbuka mtu mpaka afikirie jujidhalilisha kwako ina maana kaona una kitu special

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Umefurahiii.

Watu wanaona usipoamini Mungu unakuwa mtu muovu.

Kumbe wengine tunakataa kuamini Mungu kwa sababu kuamini Mungu kunaweza kuruhusu kufanya maovu.
Mimi na wewe wote tupo kwenye boat 1...maono yetu kuhusu mungu yanafanana ...binafsi siamini pia katika uwepo wa mungu
 
Back
Top Bottom