#COVID19 Nimepata Chanjo ya Corona nchini Marekani, puuzeni uzushi

#COVID19 Nimepata Chanjo ya Corona nchini Marekani, puuzeni uzushi

Nimefanikiwa kupata chanjo ya Corona hapa napoishi na kufanya kazi Dallas, Texas. Nimepata dose mbili za sindano kwenye bega ya kwanza tarehe 5 mwezi wa pili na ya pili tarehe 4 mwezi wa tatu. Nimepata chanjo kutoka kampuni ya Moderna. Nilivimba kidogo kwenye bega kwa mara zote lakini sijapata homa kama watu wengine wanapata homa kwenye sindano ya pili.

Chanjo ni muhimu na zinaokoa maisha hasa kwa wale wenye au ambao waliwahi kuwa na pumu, kisukari, wazee, wenye magojwa ya moyo na wamegundua pia wenye type A ya damu nao wanaumwa sana wakipata corona. Asilimia 90% ya watu wakipata hawazidiwi hivyo inawezekana hata wewe umeshapata Corona bila kujua. Lakini baada ya siku 90 unaweza kupata tena na inaweza kuwa mbaya zaidi maana mwili unakuwa hauna nguvu sana. Kwasababu kirusi cha corona kimekaa zaidi ya mwaka kinabadilika ili kiweze kuingia kirahisi kwenye miili yetu hii kitaalamu wanaita variant. Hivyo mpaka sasa kuna variant ya South Africa, England, Brazil na ili ya China. Ya South Africa ndiyo kali kuliko zote na ndiyo imeingia Tanzania kwa sasa na kusababisha watu kufa na kuumwa sana kulinganisha na ile ya mwanzo.

Kwenye kinga kuna kinga nyingi sana cha maana ni upatikanaji, usalama na chanjo kufanya kazi. Kuna vipimo vikubwa viwili vya kuzingatia cha kwanza ni kinga ya chanjo yaani ambayo inazuia mtu kupata Corona lakini cha pili je mtu akipata corona ambaye ana chanjo ataumwa kiasi cha kulazwa au kuzidiwa?. Hii ya south Africa inaonyesha kinga haifanyi kazi vizuri hasa kwa hii chanjo ambayo nchi za Africa inauziwa za Oxford Astrazenica au AZD1222. Hawajatoa data kuonyesha je mtu akiumwa inakuwaje au kinga inakuwaje. Lakini chanjo ya Johnson and Johnson imeonyesha inakinga ya corona ya south Africa kwa asilimia 57% lakini hata ukipata corona ni karibu 100% hautazidiwa. Lakini mpaka sasa HAKUNA MTU ALIYEPATA CHANJO YEYOTE POPOTE NA KUUMWA NA KUZIDIWA KIASI CHA KULAZWA. Hii ina maana gani ni kwamba inawezekana kinga ikawa ndogo lakini watu nhawatapoteza maisha ambao wana chanjo

Tanzania wanaogopa chanjo kama hii niliyopewa kwasababu inatumia technologia ya mRNA ambayo ni ya DNA na wanaogopa eti DNA zetu wazungu watabadilisha. Wakati nimeenda kupata chanjo kulikuwa na wazungu wengi wamepewa chanjo kama yangu sasa sijui hizi habari ni za wapi?!!!. Lakini kuna chanjo ambazo zina technologia kama chanjo za zamani mfano Sputnik V ambayo ni ya Urusi inatumia technologia ya zamani ya chanjo na sasa wamefanya utafiti unaonyesha inakinga aslimia 90%. Lakini hii ina order nyingi hasa huko South America itachukua muda kuipata.

Hivyo ushauri wangu ni kwa serikali kutumia chanjo yeyote kasoro ile ya China ambayo haina data ambazo watu wamezionana kusema zipo sawa. Lakini hii wenzetu wa Kenya, Nigeria, Ghana wamepata chanjo yenyewe inawezekana kinga ni ndogo kwa hii ya south Africa lakini ukipata chanjo corona itakuwa kama mafua ya kawaida haitakuuwa kama sasa hivi. Hivyo nashauri bado ni bora sana kuliko kukaa na kutokufanya maamuzi yeyote. Tukiweza kuweka order hii ya J&J ni zuri kwasababu ni sindano mmoja na inahitaji jokofu la kawaidia kuifadhi.

Tatizo serikali inaweza kusema wataalamu wanachukungaza lakini mpaka sasa hakuna habari yeyote uchunguzi umefika wapi, nani yupo kwenye hiyo team inawezekana ni maneno tu.
Wewe hujui chochote Tz maana upo Marekani na hajawahi ingia maabara yoyote ya Tz ili kujua kuna Corona gani.Wewe usutufananishe Waafrika na Wamarekani maana wao mfumo wao wa maisha haufanani na wetu.huko mnakula Bisi mnalala huku wali maharage, kwetu jua kali kwenu mnalichungulia .Acha upuuzi Mtu mweusi hana undugu na mzungu.
 
Wewe hujui chochote Tz maana upo Marekani na hajawahi ingia maabara yoyote ya Tz ili kujua kuna Corona gani.Wewe usutufananishe Waafrika na Wamarekani maana wao mfumo wao wa maisha haufanani na wetu.huko mnakula Bisi mnalala huku wali maharage, kwetu jua kali kwenu mnalichungulia .Acha upuuzi Mtu mweusi hana undugu na mzungu.

Hebu angalia bega lako kama huna chanjo😂. Usidanganye na rangi yako kijana Afya sio rangi . Tofauti ya aina ya damu kiafya ni kitu kikubwa kuliko hata rangi kama una type A haijali rangi! Hivi hizi shule za kata zinatutolea vijana wa type gani siku hizi!
 
Endelea kusema uzushi
20210315_093431.jpg
 
Si mbaya kujulishana WAPENDWA. Kwa aliepitia hii chanjo anajisikiaje?

Na ikoje, unachomwa sindano ama?

Wengine tukisikia tutashawishika kusisitiza ifanyiwe haraka kuja nchini mwetu.
 
Unachomwa sindano, binafsi kwa masaa kama nane baada ya kuchomwa mkono uliuma na kuwa mzito. Baada ya hapo sikuhisi chochote. Nimemaliza sindano zote mbili tangu mwezi wa March mwaka huu.
Congratulations dia aina gani hioo inabidi ukatoe na sadaka kanisan MAANA ninavyoziwaza loh
 
Can I get Covid after being fully vaccinated?
The U.S. Centers for Disease Control and Prevention also continues to recommend vaccinated people with symptoms get tested for COVID. Cases of fully vaccinated individuals contracting coronavirus are rare, but possible
 
Si mbaya kujulishana WAPENDWA. Kwa aliepitia hii chanjo anajisikiaje?

Na ikoje, unachomwa sindano ama?

Wengine tukisikia tutashawishika kusisitiza ifanyiwe haraka kuja nchini mwetu.
Akili kubwa 👍
Nilidungwa ya kwanza 03/2021 na ya pili 04/2021.

Ukishadungwa unawekwa checkpoint ukae kwa dakika 15 kuangalia kama una adverse reaction.

Ukipita hizo dakika 15, unapotea zako.

Next day maumivu yana kuja kwenye mkono uliodungwa, kwa mimi hii ni kawaida sababu nikisafiri lazima nikamilishe yellow card(kadi ya chanjo) kwenda dunia ya tatu,

kwahiyo haya maumivu ni kitu cha kawaida kwa yeyeto aliewahi kupitia chanjo hizi. Pitia mtu anaitwa David Attenborough, huyu inasemekana anarekodi ya dunia yakuchanjwa🤣(joking).

Binafsi sijaona mabadiliko yeyeto ya kiafya baada ya chanjo lakini mke wangu anasema;
"Pfizer did it again" kama Via......a
 
Kwasasa binaadamu hatuna tofauti na kuku wa kizungu (Broiler), kila kukicha ni kudungana machanjo kwenda mbele. Yani "Mguu upande, Mguu sawa, Kaburini elekea", muda wowote.

Maradhi kila kukicha yanazuka mapya, mpaka utamu wa maisha umekwisha. Tofauti na maisha ya enzi za mababu zetu ambao hata ukimwi kulikua hakuna.

Siku hizi ukimwi ukikukosa, kuna Hepatitis, na yenyewe ikikukosa basi kuna homa ya manjano, ukikoswa na homa ya manjano kuna Covid inakuwinda kwa spidi ya 4G.

Tunaishi kama nyani porini, kila kukicha ni kukwepa mishale kwenda mbele. Yani tafrani tupu walahi.
 
Mimi nilichomwa vaccine ya MODERNA ; hakuna matatizo kabisa . In fact vaccine ya SHINGLES inauma zaidi kuliko ile ya COVID!!!
 
Akili kubwa 👍
Nilidungwa ya kwanza 03/2021 na ya pili 04/2021
Ukishadungwa unawekwa checkpoint ukae kwa dakika 15 kuangalia kama una adverse reaction...
Mkuu nimeelewa sahihi? Kuwa ukisafiri lazima upate chanjo ya manjano, una maana kila ukisafiri unaenda kuchomwa chanjo ya "manjano"?
 
Back
Top Bottom