Nimepata kazi ambayo inaniruhusu kuhamia USA nikitaka, lakini mshahara ni ule ule popote nitakapoamua kufanyia kazi

Hamia tu USA kaka hapa USA kilo ya sukari ni tsh 1500 na utelezi ni bure kabisa. Kaka amka usingizini usije ukajinyea.
 
ni KAZI ya IT, NGO au ipi?vyovyote iwavyo kama mshahara ni huohuo basi Kaa bongo ila utakuwa jnapelekwa US maramojamoja kusoma au expusre training
Sasa nimpige nani na kwa lipi?
Pitia thread yote, umeona popote nimesema mtu anifuate PM au kiashiria chochote cha upigaji? In fact, hata PM yangu tu its inaccessib
 
ni KAZI ya IT, NGO au ipi?vyovyote iwavyo kama mshahara ni huohuo basi Kaa bongo ila utakuwa jnapelekwa US maramojamoja kusoma au expusre training
Ni NGO mkuu. Asante kwa ushauri.
 
UPDATE: Napenda kuwapatia update kuwa nimefanya uamuzi kuhusiana na hili suala.
Nimeamua kuwa nitabakia hapa hapa BONGO, baada ya kuchakata ushauri wenu, pamoja na insights kutoka sehemu mbalimbali. Nimeonelea kuwa itakua na faida zaidi kwangu nikiendelea kubaki hapa hapa, mpango ni kuweza ku save as much as possible, na kufanya investiments za long term na short term hapa hapa nchini. Hivyo, nimeshasaini mkataba wa mwaka mmoja ambao utawezesha hilo. Nawashukuruni nyote kwa mawazo yenu.
 
Hata bongo hiyo hela haitoshi
 

Maamuzi mazuri
 
1) Bongo una nyumba yako hulipii kodi
2) Houston rent ya mwezi town area $2,000 mpaka $3,000.
3) Matumizi bongo familia nzima $1,500 mnaishi vizuri tu.
Kama mimi wewe nabaki bongo kwa mshahara huo, ukijua kujipanga miaka 5 upo mbali sana lakini USA huo mshahara ujibane kweli uweze kuishi vizuri na kuwa na akiba kwa mtu mwenye familia ya watu 4.
 
Asante sana. Nimeshaamua kubaki hapa hapa, kama ulivyochambua vizuri, nimeona nikienda kule nitaishi kwa shida sana, maana ni kweli, nilikua naangalia family house nyingi za huko, rent ni around dola 2,000 had 3,000 kwa mwezi. Hapo bado matumizi mengine; hapo hapo usave na kufanya investiment.
 
Kila la Kheri, ikitokea huko mbele kuna kuhuisha mkataba, nenda kafanye kazi hukohuko, una watoto, wanahitaji elimu bora ambayo sidhani kama Tz inatosheleza hilo hitaji.

Sent from my moto g 5G (2022) using JamiiForums mobile app
Asante, nimeamua kubaki bongo kwa sasa. Huu mradi ni wa miaka mitano, kwa hiyo kwa sasa hivi nimesaini mkataba wa mwaka mmoja ambao nitakua hapa hapa bongo, then I will see in the coming years, uzuri afte mkataba huu kuisha nikisaini mwingine, chance ya kwenda kule bado inakwepo.
 
Hakuna shirika lenye kujielewa wakatoa same salary scale kwa mtu anakaa bongo na mwingine Texas us ukizingatia tofauti kubwa ya gharama za maisha
Una akili sana mkuu. Hata serikalini tu kunatofauti ya Per Dm ya city na wilayani.

Mke wako alisemaje before all? Huyo ndo ulitakiwa umsikilize.

Kama una mke na kuja kuomba ushauri huku tayari ushaonyesha kuna kitu hakipo sawa.
 
Watanzania wengi wanao ishi USA wakipata hio $7,500 kwa mwezi kwa kuja kuishi huku Tanzania 80% yao watarudi bongo.

Hio hela unaishi kama mfalme bongo mkuu hapo ukienda kuishi Houston lazima utalipa federal tax, State tax na city tax kwenye hio $7,500 kwa mwezi itaishia kuwa $6,300. Rent tufanye $2,500 + umeme,Maji,taka na cable+internet itafika $3,000. Umebakisha $3,300 ukiweka usafiri+simu fanya $500. Imebaki $2,800 mkopo wa gari+ bima yake $500 imebaki $2,300 matumizi ya chakula familia ya 4 $600 imebaki $1,700 nguo+viatu+ watoto shule + mtoko na mengine. Halafu huku bongo mfanyakazi unae ndani huko wife akianza kazi hata kula hutoijua schedule yake😂
 
Una akili sana mkuu. Hata serikalini tu kunatofauti ya Per Dm ya city na wilayani.

Mke wako alisemaje before all? Huyo ndo ulitakiwa umsikilize.

Kama una mke na kuja kuomba ushauri huku tayari ushaonyesha kuna kitu hakipo sawa.
Kuna mshkaji alitokea Boston,MA alikuja dar alikuwa analipwa mshahara uleule wa Boston tena hajapewa hata hela ya kumove zaidi ya kununuliwa ticket tu. Kila company ina policies zake
 
Una akili sana mkuu. Hata serikalini tu kunatofauti ya Per Dm ya city na wilayani.

Mke wako alisemaje before all? Huyo ndo ulitakiwa umsikilize.

Kama una mke na kuja kuomba ushauri huku tayari ushaonyesha kuna kitu hakipo sawa.
Kila shirika lina policy zake mkuu. Mfano, serikali hiyo hiyo per diem dereva analipwa sijui 60,000 au 80,000 kwa siku, wakati boss anaemuendesha kwa siku analipwa hadi 250,000; Ila mashirika ya kimataifa per diem ni flat rate, uwe mkurugenzi au uwe dereva. Hivyo kila organization na policy yake haya mambo hayako fixed.
Hata hivyo, nimetoa update kuwa nimeamua kubaki hapa hapa bongo baada ya kuchakata katika halmashauri ya ubongo wangu.
 
Na hii ndo imenifanya mimi kuchagua kubaki hapa Bongo mkuu after thorough consideration.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…