Nimepata kazi serikalini, je niondoke vipi huku private?

Hichi kitu watu wengi wanasaau sana kujiuliza. Mimi nilimaliza chuo 2015 na sikupangiwa kazi na serekali na hadi sasa nipo secta binafsi nikweli kuna changamoto zake ila pia pesa ipo na ukiweka malengo vzr unajikuta umefika mbali na umejiajiri maana unakua huna uhakika na mkataba mwingine so unakua na mpangilio mzur wa pesa. Serekalini watu wanakimbilia assurance ya kazi ila ni ulemavu sana kujua siku zote upo kazini hufukuzwi kirahisi. Unakuta mtu ana staafu ndo anawaza kujenga au kujiajiri na mafao . Changamoto za secta binafsi zinatukomaza sana kufikiri na kutaka kuwa na vyetu
 
Ndio,walikua wanaweka
Ukiandika barua ya kujiuzulu unapoteza pesa zako.

Kama una nia ya kwenda serikalini, wewe nenda baadaye watakufuta kazi wenyewe.

Kampuni siyo yako, usiwaone wema sana kwakuwa sasa hivi una afya njema, unafanya kazi vizuri na wamekupa cheo.

Siku ukikosa uwezo wa kuzalisha ndio utajua hujui.
 
Nikikumbuka enzi zangu tukipiga hela ya dili na washkaji, mfuko una dola ya kula miezi kadhaa kuacha kazi ilikua jambo dogo sana.
Natimba tu na jamaa mda wa kuingia mzigoni, tunaagiza gambe tunalitwanga hapo boss akija kuuliza vp mbona huingii time late atapigwa mkwara mzito na kazi inaisha hapo nadai changu kibabe maana sina time kurudi kuchukua.
Boss inabidi azame ofisini anilipe then tunasepa.
We unauliza tena?
 
Nikweli kabisa mkuu,huku sekta binafsi unabanwa mno maslahi nafuu ila muda wakufanya mambo yako hasa ya kipato zaidi unakua mdogo.
 
Umeongea vizuri sana. Nipo private na mkataba wetu mfupi sana so kila mtu ameweka mguu ndani mguu nje. Amna aliye kaa kiboya
 
Acha ushamba aga kwa heshima kuna leo na kesho ... sisi kuna aliyepata akaondoka kwa kuaga akalipwa kila kitu hadi mshahara na aliondoka tarehe 4 ... akapewa mpka allowance za huo mwezi ... tumia ustaarabu usiondoke kama mhuni
 
Hongera kwa kupata nafas ya uwalimu serekalin

Sent from my SM-G9250 using JamiiForums mobile app
 
Omba ruhusa kuwa una matatizo ya kifamilia, then ka-report, sign mikataba malizana nao kbs kule nadhani siku 3 zitakutosha kisha omba ruhusa kule ofisi mpya kuwa unaenda kujifungasha (nadhani unapewa 14 days). Then sasa ndo urudi ofc yako ya zamani uage kuwa umepata kazi serikalini unaomba ufanye resignation. Ingawa nadhani utatakiwa kuacha mshahara wa mwezi mmoja hapo.
Kuaga ni ustaarabu mzuri......
 
Acha ushamba aga kwa heshima kuna leo na kesho ... sisi kuna aliyepata akaondoka kwa kuaga akalipwa kila kitu hadi mshahara na aliondoka tarehe 4 ... akapewa mpka allowance za huo mwezi ... tumia ustaarabu usiondoke kama mhuni
Sawa mkuu,ushauri mzuri
 
Zungumza na bosi wako,atakupatia ABC, baada ya hapo uandike barua ya kuacha kazi
 
Kwani hio kazi ni teuzi au kwamba hukujua kwamba ikitiki utaitaji uage?
 
Heheheh ofisi ya nani mlikuwa mnafanya huu uhuni?
 
Heheheh ofisi ya nani mlikuwa mnafanya huu uhuni?
Mahotelini huko kwa waitaliano na wahindi Masaki na O bay walitukoma enzi hizo,

siku zingine ukute tunakula monde mi time ya jobb imefika basi nawaambia jamaa ngoja niingie mzigoni,
aaah wapi utasikia kaache kazi wewe tule monde.
Sasa hapo ubwii umekolea nikifkiria manyanyaso ya boss nawaambia tu nisindikizeni nikaache kazi, aah gari inawashwa twende ukaache
πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ€£.
Nikikumbuka lile life
 
Ushauri wangu...

Kama huko uliko, ktk sekta binafsi unapata malisho mazuri... Na unafanya mambo yako vizuri yananyooka.. Na umewekeza vile unaona inafaa....

Hiyo kazi endelea nayo... Achana na huko unakokimbilia..
 
Pitia taratibu sahihi za kuresign kazi kiongozi.Pia tunaomba utuambie ulikuwa shule gani na masomo gani ili tuliokosa tutumbe maombi hapo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…