Nimepata kazi serikalini, je niondoke vipi huku private?

Aga tu kistarabu uondoke usije ukawakama staff mwenzetu aliepata ajira akaondoka kwa mbwembwe alipofika kule akaambiwa amedanganya masomo yakufundisha so anaona aibu kurudi kazini, ilanasikia anashida mno.
 
Hapo tulikua group km mtu 10 hivi kuna mwenzetu tunashinda nae bar ila ni dokta wa meno e bana watu waling'olewa meno kipindi hiyo mpaka basi anaaga kabisa" naondoka na jino la mtu "
Akienda akirudi ana buku 30 anazungulusha.
Tapeli mwingine akisema anaenda town akirudi mtakula monde usiku wote na kilinda mfuko mnapewa.
Zikiisha ni nyagi tu
 
Mcheki boss umueleze dhamira yako baada ya hapo utaandika barua kulingana na mkataba mliokubaliana


usitoroke; la lesho hulijui. Usije ukashindwa kurudi yakikukuta huko uendako
 
Fanya calculations je wapi unapata faida.usidhani serikalini ndio peponi.
 
Mimi nilipata kazi serikali wakati huo shule moja ya private ilikuwa inanihitaji sana kwa MATHS na PHYSICS. Niliaga kwa amani nikavunja mkataba kwa mujibu wa vifungu vyake bila shida. Sasa nipo serikalini. Mkuu wangu wa pale private school hata nikimwambia MKUU NIKOPESHE million moja ananiambia nenda benki nakutumia saa hivi bila riba. Kwa kweli nafurahi jinsi tulivyoagana
 
kwani hiyo ajira ya serikalini umepewa tu au uliomba...na kama uliomba ulikua hujui kama upo private......fanya maamuzi
 
Mlambe makofi bosi wako
 

Huwa mnapendea nini serikalini? Marupurupu ama?
 
Omba likizo, ukaripoti na ukiwa likizo toa notisi ya kujiuzulu.
 
Hakuna za akiba au uwekezaji? Ukipata ni za kula, zikiisha unarudi kuanza upya.
 
Hakuna za akiba au uwekezaji? Ukipata ni za kula, zikiisha unarudi kuanza upya.
Nilikua kazi yenyewe siitaki vilevile, ila sometime tukifulia na demu wangu ndio nafanya, ye ndo alikua kinara kwenye madeal. Nikiona tumefubaa naenda mzigo ili tusikose ya kula na issue ndogo ndogo
Akibatua ni mzigo wa haja atakodi Hotel tutalala wiki hukobaadae ni starehe tu. Na alikua anajua kutumia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…