Yaani nashindwa nielezee vipi ili nieleweke.
Jana baada ya fainali ya kombe la dunia kumalizika nilipata maumivu makali sana ambayo sijawahi kuyapata kwenye masuala ya kimichezo yaani moyo ulikuwa unauma sana alafu nikawa sina raha kabisa. Nilijishangaa sana kutokana na hiyo hali, kwakwel niliumia sana na nikanyongonyea mithili ya mrenda.
Nilipenda sana Ufaransa atwae huo ubingwa lakini haikuwa hivyo, ilifika kipindi ukitizama kikosi cha Ufaransa chote ni Waafrika kasoro kipa wao tu, nilipenda sana hao wabaruya wachukue ubingwa. Pongezi sana kwa Mbappe
Mpaka sasa hivi bado nina maumivu makali sana, nimejaribu kutumia dawa za kutuliza maumivu lakini bado sijapata nafuu yoyote ile. Poor me