Nimepata milioni 50, nifanyie biashara gani niwe milionea?

Nimepata milioni 50, nifanyie biashara gani niwe milionea?

Endelea na unachokifanya huko na hizo daladala nimefanya. Fuso mpaka scania miaka 20 sasa. Sio kihivyo.
Kiwanja cha kujenga ni maporini. Kununua hiyo hela haitoshi nyumba prime areas kama sinza.
Sikukatishi tamaa ila jitahidi uwe na japo 200m kama unataka kutoka fasta hapa bongo.
mkuu changamoto kubwa kwenye biashara ya daladala ni ipi,, na je ww ulifanyia wap hyo biashara..kama ni dar njia hipi inalipa sana,,,na malengo kwa siku ni shingap,,, sorry kwa usumbufu kaka
 
mkuu changamoto kubwa kwenye biashara ya daladala ni ipi,, na je ww ulifanyia wap hyo biashara..kama ni dar njia hipi inalipa sana,,,na malengo kwa siku ni shingap,,, sorry kwa usumbufu kaka
Nilianza mikoani nikaja dar kwa daladala ila ugumu wake madereva wengi mateja. Hawatunzi chombo. Siku moja nilipanda gari langu sikukuta dereva wala konda ila mateja wawili na chombo kinalelekwa 'kimperampera' ligi kwelikweli. Nauli nikatoa na chenji sikupewa.
Siku nyingine dereva anakartisha ruti huku anakuambia gari ni bovu au limekamatwa.
Kibaya zaidi sasa ruti zenye pesa zinakatwa sababu ya mwendo kasi.
Car hire nayo wateja walikuwa serikali naao waamechacha.
Hata bureu de change wanalia sababu safari za nje na dili vimepigwa ambavyo ndo wahitaji wakubwa wa dola.
Biashara sasa inaahitaji ubunifu na utulivu.
 
bab zilete mwendokasi huku .. utapiga hela kishenzi .. utazalisha kuliko huko ufaransa
 
Endelea na unachokifanya huko na hizo daladala nimefanya. Fuso mpaka scania miaka 20 sasa. Sio kihivyo.
Kiwanja cha kujenga ni maporini. Kununua hiyo hela haitoshi nyumba prime areas kama sinza.
Sikukatishi tamaa ila jitahidi uwe na japo 200m kama unataka kutoka fasta hapa bongo.
Nataka kujua unayetoa ushauri huu una kiasi gani mpaka sasa maana unaongea kama mtu ambaye hata laki ya akiba kwenye akaunti huna.
 
Heshima zenu wakuu.
Mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 25,ni Mtanzania nnae ishi nchini ufaransa
Nimebahatika kupata shillingi mil 50 za kitanzania na nahitaji kuwekeza nchini Tanzania.
Je ni fursa zipi nnazo weza kuzipata Tanzania kuweza ili kuimaximize hii pesa ili niweze kuwa Millionaire ndani ya miaka 10 kutoka sasa.?
Asanteni.
Nimeku pm mkuu
 
Nataka kujua unayetoa ushauri huu una kiasi gani mpaka sasa maana unaongea kama mtu ambaye hata laki ya akiba kwenye akaunti huna.
Njoo chemba utashangaa. Pesa ninazo.kazi nzuri kubwa na cheo kikubwa na kampuni kubwa vinafanya kazi.
Hofu ya Mungu ndo mpango mzima.
 
Back
Top Bottom