Kwa "wazee" unatudhalilisha bure, tuombe radhi.
Kuna "wazee" na wazee buana, haiingii akilini kuibiwa kizembe zembe namna hiyo eti kisa maelezo na maelekezo ya mtoa huduma za mitandao.
Kwanini nisimlambe authentications za kufa mtu hata kabla sijansikiliza?
Tena niwepesi kukimbia kama mbwa!
Wenye low Iq na wenye pupa za tamaa ndiyo wahanga wakubwa wa kwanza.
Mzee mjanja kama mimi utaanzia wapi kuntapeli mie?
Utapeli si kwa njia za mitandao pekee, hata kavu kavu mtu anakuja kwa njia ya kuazima, kukopa ama kukushawishi soko ili ukijaa tu, ndiyo iwe kantolee!
Sasa njia zote haramu za dhulmati ninazijua, hata aje vipi kwangu siyo rahisi hata kidogo.
Anayeniweza mie ni mwizi aliyejizatiti kwa kutumia nguvu lakini siyo tapeli.