Nimepata uzoefu kuzuia wizi wa mtandaoni

Nimepata uzoefu kuzuia wizi wa mtandaoni

Usitukane mamba kabla hujavuka mto mkuu, binafsi sikua nawaelewa wanaotapeliwa mtandaoni mpaka pale yaliponikuta siku moja

Na mpaka sasa najilaumu kwa kuibiwa kizembe, walinilamba 750k hiyo hela mpaka leo inaniuma, laiti ningewakazia kama nnavowakaziaga sikuzote

Najiuliza yule sijui alikua ana dawa gani mpaka kuniingiza chaka kiasi kile.
Elezea ulivyotapeliwa ili tujuwe mbinu wanazotumia.
 
Elezea ulivyotapeliwa ili tujuwe mbinu wanazotumia.
Nahisi aibu hata kuelezea aise

Walinipigia wakijidai ni kampuni ya simu kwamba wanataka waniboreshee line yangu

Kuna namba wakawa wananitajia kumbe kule kufata maelekezo yao nawahamishia pesa bila kujua

Nilijionea hasira mwenyewe kwaku waendekeza na ni hela ambayo nilikua nikiitegemea
 
Usitukane mamba kabla hujavuka mto mkuu, binafsi sikua nawaelewa wanaotapeliwa mtandaoni mpaka pale yaliponikuta siku moja

Na mpaka sasa najilaumu kwa kuibiwa kizembe, walinilamba 750k hiyo hela mpaka leo inaniuma, laiti ningewakazia kama nnavowakaziaga sikuzote

Najiuliza yule sijui alikua ana dawa gani mpaka kuniingiza chaka kiasi kile.
Naelewa mlivyo pigwa wewe na mleta mada hata kabla hamja sema. Ndo maana mesema hivyo

Kila siku mnaambiwa huduma kwa wateja ni 100 tu hamuelewi

Anyway vp uko pm kuna seat nije nipumnzkie kidogo bibie
 
Kwanza nitafurahi nikipokea pole baada ya kuibiwa mara 2 kwa njia ya mtandao.Vile vile wanaoibiwa na serikali itafaidika ikinisikiliza namna wizi huo unavyoweza kama si kuzuilika basi kupunguzwa kwa kiasi kikubwa..
Wezi daima watakuwepo isipokuwa kama kuna nia safi ya kuwashughulikia basi huwa wanashindwa kuendelea na uovu wao.
Wizi wa mtandao upo wa kimataifa na upo wa kitaifa.Ule wa kimataifa ukikupata inakuwa ni ngumu zaidi kupata msaada.Huu wa kitaifa tumeambiwa pamoja na kuwepo kwa vikosi vya kipolisi vya kuushughulikia bado wezi hao wanaendelea kuwaibia watu mabilioni ya pesa na hawajaweza kupunguzwa. Hili linashangaza sana kiasi kwamba tunaoibiwa huwa tunapata dhana kuwa wezi hao si wa kawaida.Huwa wanasaidiana na hao hao ambao wanatakiwa wazuie wizi huo.
Kwanza wale wanaopiga simu ili wakuibie huwa wanakuwa na takwimu karibu zote zinazokuhusu wewe.Kinachobaki huwa ni namba yako ya siri tu.Huwa wanakuongoza hatua kwa hatua na kwa kujiamini mpaka unatoa namba yako ya siri ukidhani unazungumza na mtu wa karibu au mhudumu wa shirika la simu.Mtu wa kawaida hawezi kujiamini kufanya hivyo lazima anakuwa ana uzoefu kutoka mashirika ya simu.
Mapendekezo
1.Unapogundua umeibiwa ukipiga simu kwa shirika la simu inatakiwa hatua yoyote wanayochukua iwapo ni kuzuia muamala basi kuwe na mawasiliano ya kimtandao na kitengo cha polisi cha kuzuia wizi wa mtandao kama ilivyo taarifa ya matukio ya moto.Haitoshi wahudumu wa simu kusema ukaripoti polisi.Umuhimu wa polisi kusikia malalamiko na kuona namba ni kuwa watakuwa pengine wameshaona namba hiyo hiyo ikilalalamikiwa kwenye makampuni mengine ya simu muda si mrefu kabla.Hapo wao kimy kimya wamfuate mhusika kwa kutumia GPS ya simu ya mwizi.Wakati mwengine inatia aibu kwani wezi wa mtandao wanabaki hewani zaidi ya siku moja na ukiwapigia wanakutukana vibaya sana.
2.Namba iliyoripotiwa kufanya wizi baada ya dakika chache iwe imezimwa ili mwizi asiendelee kuibia watu kwa siku nzima.Kwa kufanya hivyo mwizi hatopata nafasi ya kuendeleza wizi na pesa inaweza kurudishwa kwa mwenyewe bila kupiga simu kuzidai kwa mwizi katika kipindi cha saa 24.
3.Masuala ya usajili wa laini za simu usifanyike mitaani. Wale wanaopita na spika za matangazo ya kusajili na kurudisha laini wapuuzwe moja kwa moja.Wengi wao wanafanya kazi mbili mbili.Na ukichunguza wana vifaa vya kuchukulia alama za vidole zaidi ya kimoja.Mwananchi usitoe vidole vyako kwa wapita njia.Huwa unawapa nafasi ya kusajili laini nyengine usizozijua kwa jina lako ambazo huzitumia kuibia watu.
4.Mwanachi ukipigiwa simu na mtu anayetaka takwimu kwenye simu akisema anatoka popote basi bora uwe na simu ya kurekodi mazungumzo yenu.Hizi sauti kama zina shaka au ukipata tatizo zipelekwe kwenye ofisi za mashirika ya simu wachunguze iwapo si watu wao wanaofanya kazi hizo baada ya muda wa kazi.
5.Laini iliyolalamikiwa kuiba pesa ambayo watu wa kampuni watakuwa wameiona baada ya kuripotiwa na kufungiwa ndani ya dakika mbili.Mwenye laini hiyo akiwa na hoja kwamba si yeye basi apige simu kampuni kwa simu nyengine yenye wasap hata ya kuazima ili aonekane sura yake bila kuona sura ya mhudumu.Pamoja na sura atakiwe kutaja vitambulisho vyake kama inavyofanyika kawaida.Pamoja na hivyo atoe maelezo kwanini imetokea hivyo.Iwapo hakuhusika arudishiwe pesa hapo hapo bila kuingiza masuala ya polisi.Akishindwa kufanya hivyo baada ya masaa 24 pesa arudishiwe aliyelalamika na namba iliyotumika kuiba iwe imefungwa moja kwa moja.Mara nyingi wezi hawatopiga simu.Itakuwa ni uthibitisho wa mwanzo wa madai ya mlalamikaji kuwa kweli ameibiwa.
Kwa hauta hizo pesa nyingi zitaokolewa na wezi watapungua sana na upande mwengine wateja watafurahia huduma za pesa mtandaoni.Kinyume cha hivyo tutafikiria kurudia enza za ujima.
Mkuu vipi huko Iran na Palestine?
 
Mkuu usitoe nywila hata ukiombwa na Waziri mkuu sembuse Meneja wa tawi la Benki.

Hawa wezi primitive ambao wanatuma random messages hao huwa wanawapata Wazee,Washamba,na Low IQ wenzao.
Kwa "wazee" unatudhalilisha bure, tuombe radhi.

Kuna "wazee" na wazee buana, haiingii akilini kuibiwa kizembe zembe namna hiyo eti kisa maelezo na maelekezo ya mtoa huduma za mitandao.

Kwanini nisimlambe authentications za kufa mtu hata kabla sijansikiliza?

Tena niwepesi kukimbia kama mbwa!

Wenye low Iq na wenye pupa za tamaa ndiyo wahanga wakubwa wa kwanza.

Mzee mjanja kama mimi utaanzia wapi kuntapeli mie?

Utapeli si kwa njia za mitandao pekee, hata kavu kavu mtu anakuja kwa njia ya kuazima, kukopa ama kukushawishi soko ili ukijaa tu, ndiyo iwe kantolee!

Sasa njia zote haramu za dhulmati ninazijua, hata aje vipi kwangu siyo rahisi hata kidogo.

Anayeniweza mie ni mwizi aliyejizatiti kwa kutumia nguvu lakini siyo tapeli.
 
Kwanza nitafurahi nikipokea pole baada ya kuibiwa mara 2 kwa njia ya mtandao.Vile vile wanaoibiwa na serikali itafaidika ikinisikiliza namna wizi huo unavyoweza kama si kuzuilika basi kupunguzwa kwa kiasi kikubwa..
Wezi daima watakuwepo isipokuwa kama kuna nia safi ya kuwashughulikia basi huwa wanashindwa kuendelea na uovu wao.
Wizi wa mtandao upo wa kimataifa na upo wa kitaifa.Ule wa kimataifa ukikupata inakuwa ni ngumu zaidi kupata msaada.Huu wa kitaifa tumeambiwa pamoja na kuwepo kwa vikosi vya kipolisi vya kuushughulikia bado wezi hao wanaendelea kuwaibia watu mabilioni ya pesa na hawajaweza kupunguzwa. Hili linashangaza sana kiasi kwamba tunaoibiwa huwa tunapata dhana kuwa wezi hao si wa kawaida.Huwa wanasaidiana na hao hao ambao wanatakiwa wazuie wizi huo.
Kwanza wale wanaopiga simu ili wakuibie huwa wanakuwa na takwimu karibu zote zinazokuhusu wewe.Kinachobaki huwa ni namba yako ya siri tu.Huwa wanakuongoza hatua kwa hatua na kwa kujiamini mpaka unatoa namba yako ya siri ukidhani unazungumza na mtu wa karibu au mhudumu wa shirika la simu.Mtu wa kawaida hawezi kujiamini kufanya hivyo lazima anakuwa ana uzoefu kutoka mashirika ya simu.
Mapendekezo
1.Unapogundua umeibiwa ukipiga simu kwa shirika la simu inatakiwa hatua yoyote wanayochukua iwapo ni kuzuia muamala basi kuwe na mawasiliano ya kimtandao na kitengo cha polisi cha kuzuia wizi wa mtandao kama ilivyo taarifa ya matukio ya moto.Haitoshi wahudumu wa simu kusema ukaripoti polisi.Umuhimu wa polisi kusikia malalamiko na kuona namba ni kuwa watakuwa pengine wameshaona namba hiyo hiyo ikilalalamikiwa kwenye makampuni mengine ya simu muda si mrefu kabla.Hapo wao kimy kimya wamfuate mhusika kwa kutumia GPS ya simu ya mwizi.Wakati mwengine inatia aibu kwani wezi wa mtandao wanabaki hewani zaidi ya siku moja na ukiwapigia wanakutukana vibaya sana.
2.Namba iliyoripotiwa kufanya wizi baada ya dakika chache iwe imezimwa ili mwizi asiendelee kuibia watu kwa siku nzima.Kwa kufanya hivyo mwizi hatopata nafasi ya kuendeleza wizi na pesa inaweza kurudishwa kwa mwenyewe bila kupiga simu kuzidai kwa mwizi katika kipindi cha saa 24.
3.Masuala ya usajili wa laini za simu usifanyike mitaani. Wale wanaopita na spika za matangazo ya kusajili na kurudisha laini wapuuzwe moja kwa moja.Wengi wao wanafanya kazi mbili mbili.Na ukichunguza wana vifaa vya kuchukulia alama za vidole zaidi ya kimoja.Mwananchi usitoe vidole vyako kwa wapita njia.Huwa unawapa nafasi ya kusajili laini nyengine usizozijua kwa jina lako ambazo huzitumia kuibia watu.
4.Mwanachi ukipigiwa simu na mtu anayetaka takwimu kwenye simu akisema anatoka popote basi bora uwe na simu ya kurekodi mazungumzo yenu.Hizi sauti kama zina shaka au ukipata tatizo zipelekwe kwenye ofisi za mashirika ya simu wachunguze iwapo si watu wao wanaofanya kazi hizo baada ya muda wa kazi.
5.Laini iliyolalamikiwa kuiba pesa ambayo watu wa kampuni watakuwa wameiona baada ya kuripotiwa na kufungiwa ndani ya dakika mbili.Mwenye laini hiyo akiwa na hoja kwamba si yeye basi apige simu kampuni kwa simu nyengine yenye wasap hata ya kuazima ili aonekane sura yake bila kuona sura ya mhudumu.Pamoja na sura atakiwe kutaja vitambulisho vyake kama inavyofanyika kawaida.Pamoja na hivyo atoe maelezo kwanini imetokea hivyo.Iwapo hakuhusika arudishiwe pesa hapo hapo bila kuingiza masuala ya polisi.Akishindwa kufanya hivyo baada ya masaa 24 pesa arudishiwe aliyelalamika na namba iliyotumika kuiba iwe imefungwa moja kwa moja.Mara nyingi wezi hawatopiga simu.Itakuwa ni uthibitisho wa mwanzo wa madai ya mlalamikaji kuwa kweli ameibiwa.
Kwa hauta hizo pesa nyingi zitaokolewa na wezi watapungua sana na upande mwengine wateja watafurahia huduma za pesa mtandaoni.Kinyume cha hivyo tutafikiria kurudia enza za ujima.
Matapeli wanakuja na njia mpya kila siku kwa hiyo katika hilo hakuna uzoefu
 
Inawezekana vipi mtu mwenye akili zako timamu ukaibiwa kizembe zembe kwa kutumia simu?

Eti, mtu usiyemjua anakupigia simu na kukuuliza taarifa zako za siri na wewe unampatia. Hiyo ni akili au makamasi?

Hata kama mtu huyo unamfahamu bado ni uzembe kumpatia taarifa zako za siri ikiwepo password na taarifa zingine muhimu.

Mtu yeyote anayeibiwa kwa njia ya mtandao ni uzembe wake mwenyewe.
 
Kwa "wazee" unatudhalilisha bure, tuombe radhi.

Kuna "wazee" na wazee buana, haiingii akilini kuibiwa kizembe zembe namna hiyo eti kisa maelezo na maelekezo ya mtoa huduma za mitandao.

Kwanini nisimlambe authentications za kufa mtu hata kabla sijansikiliza?

Tena niwepesi kukimbia kama mbwa!

Wenye low Iq na wenye pupa za tamaa ndiyo wahanga wakubwa wa kwanza.

Mzee mjanja kama mimi utaanzia wapi kuntapeli mie?

Utapeli si kwa njia za mitandao pekee, hata kavu kavu mtu anakuja kwa njia ya kuazima, kukopa ama kukushawishi soko ili ukijaa tu, ndiyo iwe kantolee!

Sasa njia zote haramu za dhulmati ninazijua, hata aje vipi kwangu siyo rahisi hata kidogo.

Anayeniweza mie ni mwizi aliyejizatiti kwa kutumia nguvu lakini siyo tapeli.
Tuko watu wapole na wema pia wanatupata sana.Mtu huwezi hata kutoa sauti ya ukali au unaona shida usijeukaambiwa huna ushirikiano.
 
Matapeli wanakuja na njia mpya kila siku kwa hiyo katika hilo hakuna uzoefu
Inawezekana vipi mtu mwenye akili zako timamu ukaibiwa kizembe zembe kwa kutumia simu?

Eti, mtu usiyemjua anakupigia simu na kukuuliza taarifa zako za siri na wewe unampatia. Hiyo ni akili au makamasi?

Hata kama mtu huyo unamfahamu bado ni uzembe kumpatia taarifa zako za siri ikiwepo password na taarifa zingine muhimu.

Mtu yeyote anayeibiwa kwa njia ya mtandao ni uzembe wake mwenyewe.
Baada ya kutulaumu tunaoibiwa lawama kubwa ziwaendee mashirika ya simu na vitengo vya polisi vya wizi wa mtandao. Inatakiwa kuwe na update kila baada ya muda kutahadharisha njia mpya.Sio kila siku maneno ni hayo hayo usitoe namba yako ya siri kwa mtu usiyemjua.Haitoshi hiyo. Unajua kwa nini anti virus za mtandao kila siku ikifika jioni wanatengeneza kinga za hali ya juu baada kuona wapi virus wamepenya kutwa nzima.
Kwanza kauli ya shirika la simu Inabidi uende polisi.Sisi hapo hatutoweza kukusaidia. Ni kauli za kutoa ushirikiano kwa wezi kabla ya kumsaidia aliyeibiwa
 
Kwenye mitandao ya benki
Matapeli wanakuja na njia mpya kila siku kwa hiyo katika hilo hakuna uzoefu
Mashirika ya simu yachukue uzoefu wa huduma za mabenki.Kadi ya nida ya mteja ikitumika kusajili laini nyengine kwenye mtandao wao papo hapo itoke ujumbe kwenda kwa mwenye kadi hiyo.Mwenyewe atajuwa iwapo ni yeye au ni mwizi.
 
Back
Top Bottom