Nimependa jinsi kijiji cha Namalembo walivyopanga mji wao pamoja na kutokuwa na rasimali fedha na wasomi kama mijini

Nimependa jinsi kijiji cha Namalembo walivyopanga mji wao pamoja na kutokuwa na rasimali fedha na wasomi kama mijini

Umeharibu kabisa sasa, wazee wa mipangomiji watatua na ramani zao uchwara, watajidai kurekebisha matumizi na kuanza kuuza viwanja, watakatakata kama viazi vya chips viwe vingi.
Hawa jamaa wa mipango miji nyambaff kabisa sijui hata huko vyuoni huwa wanafundishana nini. wananzengo wakitulia wenyewe wanaweza kufanya la maana sana ila sio hawa jamaa.
 
Kasulu wamepanga mji wao vizuri. Huku Songwe kuna kijiji kinaitwa Ifumbo. Kimepangwa vizuri sana. Watu hawana shida kupanga miji, shida ni serikali na wanaosimamia mipango miji. Hakuna anayejali iwapo miji imepangika, pumbavu kabisa.
 
Yaani mipango miji hapa Tanzania ni kizungkuti aisee. Miji yote ni uwanja wa fujo. Mimi huwa najiuliza hizo DC huwa wanafanya nini huku kwenye miji midogo inayokuwa kwa kasi?

Angalia pale mafinga, mji unakuwa ila sasa, shaghala bhaghala. Ona pale Iringa hapo stand ya zamani pogolo wamejenga hovyo. Yaani aaaa hata mitaa hakuna vurugu tu. Ona Makambako mji unajiendea tu, hamna mipango yoyote mji mbovu kama nini. Yaani tufike mahali hawa watendaji wawe ndio wasimamizi wa miji hii maana mmm. Angalia Mbeya napo hovyo kabisa.

Makambako kwa kupanga mji wamejitahidi Kuna mitaa mitatu ndo ilikuwa ovyo wamesharekebisha na eneo kubwa kwa Sasa makambako limepimwa ni vizur kulijua vizuri eneo sio kubashiri
FB_IMG_16811889713114200.jpg
 
Back
Top Bottom