Nimepewa siri nashindwa kuitunza (roho inauma)

Hizi changamoto za hivi vyama muda mwingine ni ngumu kutatuliwa,

Sema hii ni tetesi...
 
Ili uweze kumsaidia huyo rafiki yako jaribu kwanza kuivaa nafsi yake. Fikiria ungekuwa ndio ww umetendewa hivo na unaendelea kusalitiwa.
 
Mwanzo nilihisi labda anataka tuanzishe mahusiano nikataka kumpa namba ya uongo anyway kwa sababu mimi ni mwanaume nikasema ngoja nimpe ya ukweli.

Siku ya pili tangu nichukue ile namba nikapokea namba mpya kumbe ni ya yule....

Ulimpa namba yako au ‘ulichukua’ yake..? Nimeishia hapo tu.
 
kwanza tafuta maana halisi ya neno rafiki,
Kwanza tafuta maana halisi ya neno Rafiki,kisha angalia nguvu na udhaifu wa urafiki wenu,naamini utapata jibu nini ufanye. Ila naamini rafiki wa kweli hawezi kukaa kimya kwa jambo kubwa kama hilo lazima atafikisha taarifa kwa mhusika tu.
 
Tafuta mtu yeyote ambaye humjui omba msaada akusaidie simu yake, copy namba zake then mwanandikie ujumbe uliokamilika na futa text. Mwenye simu asijue endelea na mambo yako! wao watajuana huko ila ujumbe atakuwa kashapata na akiwa na akili ataufanyia kazi tena utakuwa wa kwanza kushirikishwa then unakazia hapo hapo mchezo umeisha.
 
Aisee! Lazi unayo. Ushauri wangu ni kama ifuatavyo; kama jamaa ni rafiki yako kweli basi mshitue.

Sababu ya kukuambia hivyo ni kwamba hiyo Story sio siri tena, kwani inaonekana wengi hapo mitaani wanazijua ila yeye tu ndiyo hajui.

Pili huwezi kwema majukumu kwani tayari umesha ingiza kwenye hiyo issue, kilicho baki ni wewe kumweka rafiki yako sawa.

Zingatia kuwa mpaka wewe umeipata na kuingizwa kwenye hiyo kesi, ni kwa sababu inaonekana kuwa wengi wanatumia na kitendo hicho, ila wanaogopa kuchukua majukumu. Kitu kinacho wasumbua katika hili ni kama ulivyo sema kuwa jamaa ni mmpole sana na kwa hali hiyo wanahofia Reaktion yake itakuwaje kipindi atakapo pata hiyo taarifa.

Kwa tabia yake, kama ulivyo characterize, ana weza akachukua uamuzi wa kuondoa maisha yake. Kwa hali hiyo ndiyo maana wamekutupia game wewe uimalize. Usipofanya sasa hivi iko siku atatokea jasiri atamwambia ukweli na hapo huwezi jua, inawezakana wakakusukumia wewe kwa kumwambia kuwa rafiki yako anajua hiyo issue lakini hakuna kukueleza. Na hapo utakuwa umesha makosa rafiki yako na kuvunja uhusiano pengine.

Huna choice bali ni kufunga goli tu. Huyo mke wake, kama ambavyo nimedokeza hapo awali, inaelekea ana maadui wengi mitaani kwake. Watu wana donge naye kubwa. Na wewe usipocuheza huo mpira itakula kwako. Kuwa na ujasiri na mweleze rafiki yako.

Katika ufunguzi wa maelezo yako tumia kauli za kumfanya yeye ajitafakari, kwa mfano; unaweza ukamwambia "amwangalie sana mke wake". Akikuuliza kwa nini? Mwambie kuna fununu kuwa mke wake anafanya mambo yanamwondelea heshina yake mtaani. Akiendelea kuuliza, mwambie "awa consult jirani zake kuhusu hiyo issue wata.msaidia."
 
Nina Campaign naianzisha soon kuhakikisha watoto wote kabla hawajaandikwa kwenye card za clinics hatimaye Birth Certificates wazazi wao( Baba + Mama) wawe wamefanyiwa DNA testing kuthibitisha kama ni watoto wao au laa
Na hii itabidi ifanyike kwa watoto wote wanaozaliwa hapa nchini
 
Sio lazima umwambie kila kitu mdau wako,ila unaweza kumpa njia za kuujua ukweli ukawa umemsaidi pakubwa sana,ila fanya hivyo baada ya wewe kuwa na ushahidi juu ya hilo. Ila kujua jambo hilo kama ni la kweli kwa huyo mdau wako ni jambo la dharura yaani anatakiwa ajue,tena haraka iwezekanavyo.
 
K Aiseee Mimi katika masuala ya usaliti sinaga subira kabisa Ila chamuhimu ni jamaa apewe taarifa Kwa njia ambayo haitamuumiza ili achunguze Hilo suala majiran ndio wanajua maisha yetu sisi wananchi ambao hatukai mtaani tulioacha wake zetu nyumban mana mambo ni mengi na wanawake Wana Siri Sana Ila majiran akiingia mwizi usiku wanaweza wasimuone lkn akiingia mchepuko wa mkeo au mumeo wanajua so ninachoomba hapo jamaa apewe habari hakuna cha kuharibu ndoa wala kusingiziwa hapo kitaa kuna watu wangapi mbn hawajasingiziwa kasingiziwa huyo mtu hapo.????? Hakuna kitu kibaya katika hii dunia kama kupigiwa mkeo
 
Wewe tulia tu mkuu. Au mpe namba ya mhusika huyo aliyekupa hizo habari. Usikubali kuuvaa huo mkenge.
 
Usimuache mwana aangamie, tafuta njia nzuri ya kumuabarisha asije akalea watoto wa mwenzie bila kujua mwisho wa siku wakaja kumwaga
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…