KERO Nimepiga simu Tanesco kuhusu makato kodi ya Jengo, hata wenyewe hawajui kwanini wamenikata. Huu wizi!

KERO Nimepiga simu Tanesco kuhusu makato kodi ya Jengo, hata wenyewe hawajui kwanini wamenikata. Huu wizi!

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

Magazetini

JF-Expert Member
Joined
Aug 16, 2014
Posts
593
Reaction score
1,712
Nimepiga simu Tanesco, wamesema mita yangu ilikuwa inadaiwa 18,000 kwa mwaka wa fedha ulioisha(2023/24) hivyo wamekata pesa hiyo niliponunua umeme leo.

Nikawauliza mbona wamekuwa wakinikata kila mwezi, hili deni wanalosema sijalipa mwaka mzima limetokea wapi?

Majibu(TANESCO ): Hizi taarifa zake ziko TRA za kodi za majengo, anaeshugulika na kodi za majengo ni TRA na sio Tanesco, Tanesco tunatumika pale kipindi mteja ananunua umeme kodi ya majengo inalipwa kupitia manunuzi yake ya umeme lakini kutokana na kumbukumbu za TRA bado huyu mteja anadaiwa hiki kiasi.

Kwahiyo kama kutakuwa na changamoto nyingine yoyote, kama yeye ana uhakika alikuwa akilipia kila mwezi anaweza akaonana na maafsa wa TRA ofisini wakamuangalizia deni lake kodi za majengo na watampa ufafanuzi zaidi kwasababu wao wana rekodi yake ya kodi za majengo kwa kipindi chote.

Nilipohoji mimi siwajui TRA kwasababu aliyechukua hela yangu ni Tanesco, akajibu wao hawana jukumu la kukata mtu bali ni TRA na ninaponunua umeme moja kwa moja TRA wanachukua hela husika. Nikamwambia mimi siwezi kwenda TRA kwasababu hizi hela huwa sizipeleki TRA na hili jambo TRA wameshwahi kuliruka simu ikaanza kupiga makolrokocho na mwisho ikakatwa.

Pia, soma=> TRA: Hatuhusiki na ukusanyaji wa Kodi kupitia LUKU


Kwanini hizi mamlaka mbili zimeamua kutuibia watanzania, kwanza kodi yenyewe tangu mwanzo imekaa kiunyonyaji, baadae wakaamua kuiongeza kwa 50%, nusu nzima waliongeza na sasa wameona haijatosha wameamua kututoza mara mbili mbili
 
Mbona ikowazi kodi ya majengo inakatwa wakati wa kukunua umeme
 
Tujitahidi punguza matumizi ya umeme, Ili kulipa Kodi ya pango.
Ka kwa mwezi watumia unit 100, jitahidi zishuke hadi unit 50.
TANESCO wanaupiga mwingiii sana
 
Nimepiga simu Tanesco, wamesema mita yangu ilikuwa inadaiwa 18,000 kwa mwaka wa fedha ulioisha(2023/24) hivyo wamekata pesa hiyo niliponunua umeme leo.

Nikawauliza mbona wamekuwa wakinikata kila mwezi, hili deni wanalosema sijalipa mwaka mzima limetokea wapi?

Majibu(TANESCO ): Hizi taarifa zake ziko TRA za kodi za majengo, anaeshugulika na kodi za majengo ni TRA na sio Tanesco, Tanesco tunatumika pale kipindi mteja ananunua umeme kodi ya majengo inalipwa kupitia manunuzi yake ya umeme lakini kutokana na kumbukumbu za TRA bado huyu mteja anadaiwa hiki kiasi.

Kwahiyo kama kutakuwa na changamoto nyingine yoyote, kama yeye ana uhakika alikuwa akilipia kila mwezi anaweza akaonana na maafsa wa TRA ofisini wakamuangalizia deni lake kodi za majengo na watampa ufafanuzi zaidi kwasababu wao wana rekodi yake ya kodi za majengo kwa kipindi chote.

Nilipohoji mimi siwajui TRA kwasababu aliyechukua hela yangu ni Tanesco, akajibu wao hawana jukumu la kukata mtu bali ni TRA na ninaponunua umeme moja kwa moja TRA wanachukua hela husika. Nikamwambia mimi siwezi kwenda TRA kwasababu hizi hela huwa sizipeleki TRA na hili jambo TRA wameshwahi kuliruka simu ikaanza kupiga makolrokocho na mwisho ikakatwa.

Pia, soma=> TRA: Hatuhusiki na ukusanyaji wa Kodi kupitia LUKU

Kwanini hizi mamlaka mbili zimeamua kutuibia watanzania, kwanza kodi yenyewe tangu mwanzo imekaa kiunyonyaji, baadae wakaamua kuiongeza kwa 50%, nusu nzima waliongeza na sasa wameona haijatosha wameamua kututoza mara mbili mbili
TUKANA SERIKALI NDIO WATAJUA WAJE KUKUJIBU HARAKA NDIO WANAFAHAMU
 
Back
Top Bottom