Bujibuji Simba Nyamaume
JF-Expert Member
- Feb 4, 2009
- 76,107
- 160,001
Muda huu nikiwa nangoja basi ili nirudi nyumbani kutoka kazini mara nikamuona mke wa jirani yangu akija huku akiwa amenuna na kukunja sura.
Alikuwa anatembea kwa mwendo wa kasi kuelekea upande nilioko.
Aliponifikia, akanikunja shati na kuanza kunipiga vibao, nikiwa katika hali ya mshangao, watu waliokuwepo kituoni wakamshika, ndipo alipoanza kuporomosha matusi "mwacheni nimshikishe adabu, anampeleka mume wangu kunywa pombe na kumtafutia wanawake".
Watu wakamkokota, na mi nikawa naondoka kiunyonge tena kwa aibu, nyuma nilisikia watu wakisema umemkomesha nguruwe akome.
Dah... Kumbe unaweza kusingiziwa hivihivi kwa makosa ambayo hujafanya.
Lakini tunaambiwa shukuruni kwa kila jambo
Alikuwa anatembea kwa mwendo wa kasi kuelekea upande nilioko.
Aliponifikia, akanikunja shati na kuanza kunipiga vibao, nikiwa katika hali ya mshangao, watu waliokuwepo kituoni wakamshika, ndipo alipoanza kuporomosha matusi "mwacheni nimshikishe adabu, anampeleka mume wangu kunywa pombe na kumtafutia wanawake".
Watu wakamkokota, na mi nikawa naondoka kiunyonge tena kwa aibu, nyuma nilisikia watu wakisema umemkomesha nguruwe akome.
Dah... Kumbe unaweza kusingiziwa hivihivi kwa makosa ambayo hujafanya.
Lakini tunaambiwa shukuruni kwa kila jambo