Nimepokea mzigo kutoka Ali Express kupitia Posta

Nimepokea mzigo kutoka Ali Express kupitia Posta

Uzi mzuri mkuu umenimotivate na Mimi kuagiza hebu nielezee vizuri hapo kwenye sanduku la posta, ulikua na anuani yako yaposta personally (p.o box) au vipi? Sijaelewa hapo uliposema uliweka anuani ya posta ya morogoro.
Kila Mkoa hua una postal code zao au zip code, sasa uliingia hata google andika postal code/zipcode ya mkoa wako watakuletea, ndo uijaze hapo kwenye adress yako na namba ya simu ambyo unaitumia, means mzigo utakuja kwenye posta ya mkoa wako then wao watapiga simu kwa namba iloandikwa wakat wa shipment ya mzigo
 
Usije kujaribu kulipia maana mara nyingi huko Ali au ebay au popote watakutumia mzigo wako kweli tatizo ukishaingizwa bongo wanaopokea ili kukufikishia (posta, dhl n.k) wao wakishajua ni mzigo wa thamani lazima waupige maana wanajua kabisa hauna namna ya kuwajua au ukifuatilia utachoka tu mwenyewe na kuachana nao.

Mimi nina experience na eBay. Nilikuwa naagiza vitu vya hovyo hovyo napata siku nilikuja jichanganya nikaagiza power tool set. Hapo ndio nikaja kujua kuwa sijui.
Kwanini hukufungua desipute? Ukiibiwa kitu ni msala kwa posta wao wenyew...na mzigo usipo upata utarudishiwa hela yako kweny refund...haya mambo unatakiwa ujifunze kwanza ,hakuna kitu utaibiwa au kupoteza pesa yako..hii ni system
 
Hongera,hata mimi nimewahi kuagiza mzigo maramoja kupitia Aliexpress,sikupata usumbufu wowote na ulikuja mpaka posta wakanipigia simu nikaupata ukiwa kamili,ilikuwa ni bluetooth speaker...
Asant mkuu [emoji120][emoji120][emoji120]
 
Nadhani kwa vitu vyenye thaman kubwa ni safe kutumia hawa agents wa kuagiza mizigo wenye ofis zao hapa tanzania unaongea nae bei wanakuletea mzigo na wao ndo wanasimamia kila kitu mpaka mzigo ukufikie
Akina nani?
 
Kila Mkoa hua una postal code zao au zip code, sasa uliingia hata google andika postal code/zipcode ya mkoa wako watakuletea, ndo uijaze hapo kwenye adress yako na namba ya simu ambyo unaitumia, means mzigo utakuja kwenye posta ya mkoa wako then wao watapiga simu kwa namba iloandikwa wakat wa shipment ya mzigo
Okay nimeelewa Asante.
 
Kila Mkoa hua una postal code zao au zip code, sasa uliingia hata google andika postal code/zipcode ya mkoa wako watakuletea, ndo uijaze hapo kwenye adress yako na namba ya simu ambyo unaitumia, means mzigo utakuja kwenye posta ya mkoa wako then wao watapiga simu kwa namba iloandikwa wakat wa shipment ya mzigo
postal code zinaenda mpaka levo ya kata.
 
Habari wana Jamvi, nilikua nina mashaka sana na kuagiza mizigo Ali Express kwamba ntapokeaje mzigo wangu.

Nikafanya majaribio nilinunua bidhaa mbili Moja ni flash ambayo ipo kama kadi ya master card (GB16) na nyingine ni Case ya external hard disk.

Niliingia kwenye aliexpress nikatengeneza profile yangu na kwenye adress niliweka morogoro na nkaweka postal code ya morogoro ambyo ni 67000. Basi nkaenda kwenye kulipia bidhaa.

Malipo niliyafanya kwa kuingiza namba za Visa Card yangu ya CRDB then nkaweka security code (namba 3, zilizopo nyuma ya kadi yako) nilipomaliza basi wao wakakata kiasi cha pesa kinachohitajika moja kwa moja kutoka CRDB.

Bidhaa zangu zote nilizonunua zilikua hazizid elf 10 bei yake kwa pesa ya kitanzania na zote nilichagua za free shipping. Baada ya kuweka order ilikua mwez wa 12 mwishon nkatulia kusubiri na kila siku nlikua naingia kwenye shipped items naona progress mzigo umefika wapi.

Nmesubiria sana mpaka mwez wa kwanza ukaisha kwenye track ya mzigo wangu naona zmeshafika destination country, nikawa nasubiria.

Mpaka mwanzon mwa mwezi wa 2 kama tar 4 ivi nkapigiwa simu na Posta Mkoa Morogoro naambiwa kuna package zako 2 hapa, nkaenda pale nkapewa control number. Kila mzigo pale posta nmelipia 2350. Jumla nkalipa 4700. Nkapewa package zangu.

Bidhaa ni nzuri na hazina shida yoyote nmekua confident kuagiza mizigo kwa hawa jamaa.View attachment 2116927
Kumbe ata wamatombo nao wanaweza agiza mzigo ukapokea posta....hongereni waluguru
 
Umezunguka mnoo, ukihitaji msaada tafuta tukusaidie. Flash sio ya kuchukua miezi miwili njiani na unakuja kuandikia uzi. Na hiyo njia yako ya ulipaji wa pesa sio nzuri, hapo kuna makato hujatwambia.
Njia nzuri ya kulipia bidhaa mtandaoni ni ipi?
 
Nmejaribu kuangalia kwenye laptop shipping fee zao kubwa sana yaani, kwa mfano pia nmetafuta HeatPress ya 5 in 1, machine ambayo wao wanauza $120 tu ila Shipping fee naambia $250 ukijumlasha hapo $350

Heat press huwa hatupakii kwa shippers wa li express.. tunapakia kwa 3rd party hasa hasa dhl
 
Inategemea na supplier uliponunua. Baadhi sio waaminifu. Ali Express ni kiunganishi tu kati yako na muuzaji. Eg. Mwaka jana August Nilinunua bidhaa mbili totauti kutoka wauzaji wawili tofauti kupitia Ali Express. Bidhaa moia ilifika Dec/2021, sababu aliyotoa supplier ni kuwa Logistic company aliyotumia kuutuma mzigo kwangu ilipoteza mzigo, hivyo nilipofuatilia sana ndio akatuma tena!!! (Ina maana nisingefuatilia ungepotea). Bidhaa ya pili mpaka leo Feb/2022 haijafika. Supplier hana jibu la kuridhisha. (Ina maana umepotea).

Hii ni shida inawapata wengi pia. Ni MUHIMU sana kusoma Reviews za Seller/Supplier wako Kabla haujaamua kununua kwake.
Hizi platforms eBay/AliExpress zinaonesha pia huyu seller amekua akifanya biashara kwa hiyo platform tangu lini pamoja na rating ambazo buyers wamempatia. Hii inakusaidia kujua kama ni legit Au ana magumashi.

Nakumbuka 2014, niliwahi kununua laptop. Jamaa wa Dhl wakaniletea na makaratasi ya kodi za TRA. Tangu hapo nikawa discouraged kununua vitu vya thamani kubwa.
 
Back
Top Bottom