Nimepooza kiuno hadi chini, msaada tafadhali

Nimepooza kiuno hadi chini, msaada tafadhali

Ndiyo nilimpeleka kwa huyo mkorea tatizo likaonekana kwenye pingili za shingo na mishipa ya fahamu ndo maana akawa kama anapooza upande mmoja wa kulia.

Vyote amepona shida sasa imebaki kichwani anasikia kelele kama za mtu anapiga manyanga,hiyo nayo imekuwa ngumu kutoka kila dogo akienda clinic anaambiwa itaisha though ni gharama nakomaa nae maana kidogo kwa hawa jamaa nimeona kuna mwanga wa kupona
Mkorea anapatikana wap
 
Tuwe na staha kidogo, vipo vya kufanyia dhihaka lakini si maradhi ya mtu.

Inawezekana ikawa umeuliza kwa nia ya kutaka kujua lakini hudhani si wakati muafaka kuuliza hilo swali.
Ni kama unaetia ndimu kidonda.

Anyways ni mtazamo wangu tu sina dhamira ya kujifanya nina maadili zaidi.
Wee una akili Sana ubarikiwe Sana mzee wa sumu kali

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Mafuta ya zaituni, habisouda na swaum kwa wingi changanya after grind, Chua kuanzia kichwani, kwenye uti wa mgongo malizia miguuni, ni inbox jina lako nikuweke kwenye maombi, for sure najiamini kwenye maombi and then baada ya wiki mbili utujuze maendeleo, pole sana mkuu!
Binafi mm nitakutafuta unanifanyie maombi nahitaji maombi mkuu Niko serious

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Back 2017 nilipata hili tatizo baada ya ajali. Nikalazwa bochi mwaka mzima. Nilitoka sikai wala kusimama. Muda mwingi nalala.
Nikahudhuria mazoezi ya physical na massgae pale bochi kwamsuguri. Sikuacha mazoezi. Nilitengenezewa nyumbani chuma la kilo 30 lile kama la gym. Asubuhi na jioni nikawa nanyanyua. Mimi nilikua napata maumivu kabisa ya uti wa mgongo.
Mwezi wa saba 2018 (mwaka na mwezi mmoja) baadae niliweza kusimama na Magongo. Mwezi mbele nilikua nadunda, naendesha gari, nakimbia, na hata mpenzi wangu aliyekua bega kwa bega na mimi alifurahi sasa.
POLE SANA UTAPONA.
JITAHIDI MAZOEZI
Kuna mashine ya massage inatikisa hivi ina kama kipira mbele zipo kwenye physiotherapy mahospitalini.
Kuna mafuta pia nilikua napakwa. Yalisaidis sana.
 
Pole sana mkuu kwa changamoto iliyokupata ,pia ITV kila Jumapili kuanzia 21:05-21:15 kuna jamaa anajitangaza anatibu hayo magonjwa unaweza mcheck.
 
MRI haikuonyesha tatizo lolote? Kwasababu kila aina ya Paralysis ina chanzo chako au sehemu yake kwenye UTI wa MGONGO ambapo panahusika...
Na ubongo kuwa na tatizo kunaweza kusababisha hili tatizo,achana na maombi kupitia dini/wachungaji/maasikofu/n.k muombe MUNGU moja kwa moja atakunyooshea,pakuponea ni hospitalini labda tatizo liwe fedha ila tunaweza kukuchangia kama jf mwenzetu iwapo itabidi kwa kidogo tutakachokuwa nacho.

Rudia vipimo Mungu ni wa ajabu sana utapata majibu ya tatizo lako,mimi nilisumbuka sana sana na kuharisha na kutapika damu nikiambiwa ni vidonda vya tumbo hospitali zote hadi muhi2mbili nilikata tamaa na nilidhohofika sana lakini niliomuomba Mungu nikaenda Mloganzila pima pima na wewe ghafla alitokea daktari mmoja mwanamke nakusema "rudieni vipimo" na kweli ktk vipimo vilevile ikagundulika tatizo na kielekezwa matibabu nikafanyiwa Muhimbili Upanga naendelea vzr na matibabu sjataoika damu tena na niko imara.

Mtumainie MUNGU!!
 
Duh pole sana aisee
MRI scan iko expensive… sorry vilianzaje anzaje? Ni kihosp au kidunia 🥹

Ulifanikiwa kufika Rabinnsia hosp?
Sijui kwanini uwa nina imani na kitengo cha mifupa Rabinnsia.

Mungu akuponye
Rabininsia kwa sasa hamna kitu nilitaka kufa pale kwa uzembe wao na kutanguliza fedha wako kimaslahi,nashauri aende muhimbili tu akiweza kupata mtu wa kumshika mkono atapona
 
Dawa zitakazo kusaidia wewe ni za kuchua Mama yangu alipata ugonjwa huo yaani ilikuwa ni kupokezana kuchua mpaka kapona
Ndiyo,na mazoezi ikibidi awekwe kwenye pipa la mchanga wa baridi wakianzia kiunoni kisha wamkande
 
Back 2017 nilipata hili tatizo baada ya ajali. Nikalazwa bochi mwaka mzima. Nilitoka sikai wala kusimama. Muda mwingi nalala.
Nikahudhuria mazoezi ya physical na massgae pale bochi kwamsuguri. Sikuacha mazoezi. Nilitengenezewa nyumbani chuma la kilo 30 lile kama la gym. Asubuhi na jioni nikawa nanyanyua. Mimi nilikua napata maumivu kabisa ya uti wa mgongo.
Mwezi wa saba 2018 (mwaka na mwezi mmoja) baadae niliweza kusimama na Magongo. Mwezi mbele nilikua nadunda, naendesha gari, nakimbia, na hata mpenzi wangu aliyekua bega kwa bega na mimi alifurahi sasa.
POLE SANA UTAPONA.
JITAHIDI MAZOEZI
Kuna mashine ya massage inatikisa hivi ina kama kipira mbele zipo kwenye physiotherapy mahospitalini.
Kuna mafuta pia nilikua napakwa. Yalisaidis sana.
Bochi kwa msuguri ndio hospital ya hao wakorea au
 
Hapana sikuikariri jina ila ni Msuguli barabara ya kuelekea Msingwa.

Ukisimama traffic lights za Msuguli jengo unaliona upande wa kushoto kama unaelekea Mbezi.
Mkuu madaktri nihao hao wakorea wawili mke na mume naje wanavipimo au
 
Hii si bochi ndo hospital peke iliyopo apo unapoelekeza ukiwa chini unaona matenk yake meusi
Hapana sikuikariri jina ila ni Msuguli barabara ya kuelekea Msingwa.

Ukisimama traffic lights za Msuguli jengo unaliona upande wa kushoto kama unaelekea Mbezi.
Hapana sikuikariri jina ila ni Msuguli barabara ya kuelekea Msingwa.

Ukisimama traffic lights za Msuguli jengo unaliona upande wa kushoto kama unaelekea Mbezi.
 
Back
Top Bottom