Nimerejea kutazama 'Video' mbalimbali za Hayati Rais Dkt. Magufuli niseme tu Samahani kwa 'Kumkosoa' ila Asante Mungu kwa 'Kutuzawadia' Rais kama yeye

Nimerejea kutazama 'Video' mbalimbali za Hayati Rais Dkt. Magufuli niseme tu Samahani kwa 'Kumkosoa' ila Asante Mungu kwa 'Kutuzawadia' Rais kama yeye

Pole sana mkuu, Binafsi Magufuli naamini ndiye Rais bora ambae aliiwaza Tanzannia ya miaka 2050, Magufuli alikuwa kiongozi sema Watanzania wengi wanataka wanasiasa.

Hii picha hapa chini iko ndani kwangu tena chumbani kwangu!

View attachment 1991351
Mazuzu mpo wengi nchi hiyo. Haya madhila yote yanayoonekana leo ni matokeo ya utawala wake muovu. Unapoharibu mfumo wa sekta binafsi ulio rasmi na kuwadanganya kwa ujinga wa machinga ndio sababu ya nchi nzima kugeuka gulio.
 
Hakika
Kwangu mimi JPM JPM alikuwa rais muuaji, mwenye chuki kali sana kwa wanamkosoa na kumpinga, mbinafsi aliyepitiliza kiwango cha kawaida na mungu mtu aliyependa kusujudiwa mpaka na nzi. MUNGU AMEWATENDEA HAKI WATANZANIA.
 
Hayati Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli Asante kwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa Kipindi chako chote na leo GENTAMYCINE bila Unafiki nasema Tanzania tarehe 17 March, 2021 tumempoteza "Malaika Maalum' aliyeletwa na Mwenyezi Mungu kuja Kutuamsha Watanzania, Kututhaminisha, Kutuheshimisha, Kutuaminisha na kutuletea Maendeleo ya haraka.

Kutoka Mwezi March 2021 hadi leo hii (Mwezi Oktoba 2021) nimeanza Kuiona Tanzania ya tofauti kabisa ambayo imeanza kurudi nyuma na 'Kusuasua' katika Sekta nyingi na Maeneo mengi hali ambayo imeanza Kunitisha huku Machozi ya Kumbukumbu ya Kuondokewa nae Hayati Rais Dkt. Magufuli yakianza 'Kunibubujika' tena.

Nisamehe Hayati Rais Dkt. Magufuli kwa Kukukosoa Kimihemko, nakukumbuka, nakulilia sana na namuomba Mwenyezi Mungu ailaze Roho yako mahala pema Peponi ila huko Chato ulikolala sasa jua kuwa Viatu vyako bado ni Vikubwa na Vinawapwaya wale waliodhani kuwa aina ya Uongozi wako ulikuwa ni rahisi wakisahau kuwa Umahiri wako wa Kiuongozi uliongozwa ma kutawaliwa zaidi na Kumtanguliza Kwako Mwenyezi Mungu na Malaika wake.

Ninatamani 2025 aje tu Magufuli mpya.
Kwa hiyo Mungu huyo huyo unamshukuru na bado unamlilia kwa kumwita kwake mtu mwema.Familia nyingi ikimo Mimi tumeondokewa na Baba pengine tukiwa bado akili zetu hazijwa na uwezo wa kujipambania lakini hatukai tulia bali tumeamua kutumia Pengo hili kuyaishi maisha yasiyo na utegemezi au kulia lia.Ukimaliza kulia joto atakua ameshawika amka kapambane.
 
Tanzania tumeondokewa na Mkombozi.
Kwa upeo lakini sio wote wanafikra Kama zako.Kinachotofautisha kiongozi mmoja na mwingine ni vipaumbele na style.Ni mkombozi kwenye angle ipi? Fafanua Mimi naona alikua rais Kama mwinyi,Mkapa,Jk nk..ambao wote lengo ni kuendeleza gurumu.
 
Magufuli alianza siasa akiwa na miaka kama 35 hivi sina uhakika na akafariki akiwa na miaka 61. Kwa nini Mungu alimwacha Magufuli miaka hiyo yote na akamchukua yesu mapema kama kifo ni adhabu itokanayo na kilio cha wanachi?
Kihalisia kila mtu kuwepo kwake duniani kwa muda ambao Mwenyezi Mungu anampa kuna kuwa na kusudi maalumu(specific purpose),na hii ndio sababu kati ya millions of sperms heading to the egg is only one sperm produce a humain,hii ni sayansi ya ajabu sana
Issue kubwa ni pale muda wa kusudi unapoisha na kupimwa,swali linabaki tutakuwa tumetimiza kwa kiwango kile ambacho ilikusudiwa,kiwango cha kati,Cha chini kabisa,au hatujatimiza kabisa kusudi.
 
Kumbe!!!nadhn utoto unakusumbua
Kwangu Mimi Marais wazuri, makini, werevu na Wachapakazi niliowahi kuwapenda na nawalilia sana na 24/7 ni Watatu tu Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere, Hayati Mkapa na Hayati Dkt. Magufuli wengine walijitahidi / wanajitahidi ila waliharibu na wanaharibu zaidi.
 
Mbona hautaji wezi aliowashughulikia accordingly,wauza madawa ya kulevya,wapora rasilimali za nchi na waonevu wa wanyonge.Au umesahau wahuni kama wakina Papaa Msofe,Ndama na wahuni wengine ambao jela iligeuka kuwa mapumziko yao
Angeweza kuwashighulikia hao wahuni bila Kuunda Genge la Majangili akina Sabaya.
Kitendo chake cha kufadhili Genge la Majangili kinafuta Credibility yake yote
 
Hutokaa ufute kumbukumbu nzuri za magu kwa hizo hoja nyepesi, watu tulikuwa tunaona matokeo, sio porojo porojo
Mbele ya Ndugu wa Ben Saanane Mzee wenu alikuwa Ibili na Mumiani Mkubwa Sana
Mungu kaiondolea Dunia Balaa na Laana
 
Mazuzu mpo wengi nchi hiyo. Haya madhila yote yanayoonekana leo ni matokeo ya utawala wake muovu. Unapoharibu mfumo wa sekta binafsi ulio rasmi na kuwadanganya kwa ujinga wa machinga ndio sababu ya nchi nzima kugeuka gulio.
Kutaka nikuamini ww wakati kipindi cha utawala wake nilikuwepo nilishuhudia kwa macho yangu ni upumbavu! We endelea kuamini hivo unavyoamini acha nami niamini kile ambacho nilikiona.

I'm sorry brother tusipqngiane! Ijue mipaka yako.
 
nilikuchukia sana magufuli nisamehe bure, kupitia awamu hii nimejifunza ni bora kua na kiongozi mmoja mungu mtu kuliko kua na viongozi ambao kila mmoja ni mungu mtu katika eneo lake.
 
Kutaka nikuamini ww wakati kipindi cha utawala wake nilikuwepo nilishuhudia kwa macho yangu ni upumbavu! We endelea kuamini hivo unavyoamini acha nami niamini kile ambacho nilikiona.

I'm sorry brother tusipqngiane! Ijue mipaka yako.
Hakuna cha mipaka hapo, the man was good propagandist. Yes, he did something (as others did too), lakini baadhi ya maamuzi yake mengi yana negative repercussions for long term country progress. Na kubwa kuliko yote ni kusema uongo kwa yasihitaji kusemewa uongo.
 
Mbele ya Ndugu wa Ben Saanane Mzee wenu alikuwa Ibili na Mumiani Mkubwa Sana
Mungu kaiondolea Dunia Balaa na Laana
Accusations zisizo na vithibitisho zipo tokea enzi za kambarage, unfortunately hazijawahi kufuta kumbukumbu nzuri walonazo watu kwa viongozi majemedari.
So, itabidi mvumilie sifa watakazomwagiwa mpaka mtakapokufa.
 
Kwangu mimi JPM JPM alikuwa rais muuaji, mwenye chuki kali sana kwa wanamkosoa na kumpinga, mbinafsi aliyepitiliza kiwango cha kawaida na mungu mtu aliyependa kusujudiwa mpaka na nzi. MUNGU AMEWATENDEA HAKI WATANZANIA.
Usitusemee watanzania wote, sema shetwani amewatendea haki nyie majizi, mafisadi, vyeti feki, wauza ngada, wapiga dili na vibaraka wa mabeberu.

Sent from my itel W6004 using JamiiForums mobile app
 
Hakuna cha mipaka hapo, the man was good propagandist. Yes, he did something (as others did too), lakini baadhi ya maamuzi yake mengi yana negative repercussions for long term country progress. Na kubwa kuliko yote ni kusema uongo kwa yasihitaji kusemewa uongo.
Brother unahisi mimi kuto kukupinga naamini uko sahihi? Ila naheshimu mawazo yako cos mtazamo wangu sio wako!

Binafsi natamani mabadiliko kweli katika nchi yetu labda kama wakiosema mabadiliko 2015 hawakujua hayo mabadiliko yatakujaje.
 
Kutaka nikuamini ww wakati kipindi cha utawala wake nilikuwepo nilishuhudia kwa macho yangu ni upumbavu! We endelea kuamini hivo unavyoamini acha nami niamini kile ambacho nilikiona.

I'm sorry brother tusipqngiane! Ijue mipaka yako.
Ulishuhudia Kupotezwa Ben Saanane, Kutekwa Kwa Roma Mkatoliki, Kupigwa risasi Akwilina, uchaguzi Mkuu kuharibiwa kabisa, Kuibuka Kwa Magenge ya wahuni Kama vile Sabaya, Musiba, Bashite, Mashimo n.k
 
Angeweza kuwashighulikia hao wahuni bila Kuunda Genge la Majangili akina Sabaya.
Kitendo chake cha kufadhili Genge la Majangili kinafuta Credibility yake yote
punguza chuki mkuu, yesu pia alikua na wanafunzi waovu je, uovu wao ulifuta credibility yake?
 
Back
Top Bottom