Uchaguzi 2020 Nimeshangaa Magufuli kusema ameongeza mishahara kwa watumishi wa Serikali kimya kimya miaka yote mitano

Uchaguzi 2020 Nimeshangaa Magufuli kusema ameongeza mishahara kwa watumishi wa Serikali kimya kimya miaka yote mitano

Akiwa mkoani Mara Mgombea wa CCM Dkt John Magufuli kwenye uzinduzi wa kampeni katika mkoa huo Mgombea amesema kuwa "naskia kuna mtu anasema sijaongeza mshahara watumishi wa umma ,Watumishi wa umma nimewaongezea mshahara kimya kimya "
Aliendelea na kusema kuwa ukipandisha madaraja huongezi mishahara ,ukipunguza PAYE sio kuongeza mishahara...
Lord have mercy 🤐
 
Hapo hapo anasema atawaongezea mishahara wafanyakazi akikaribia kumaliza muda wake, nafikiri huu uchaguzi kwa namna yoyote ile ata shinda so tusubiri danganya toto

Hapo hapo anasema siwezi ongeza mshahara sababu najenga sgr na bwawa la umeme dadek
 
Mkuu inaonekana wewe hujasoma hesabu na hujui hesabu. Kitendo Cha kushusha thamani ya "PAYE" Kutoka 15% mpaka 9% lazima pesa itapanda na ukipandisha na mshahara utashukwa pia.

Mathematically; Makato ya mshahara (PAYE) is inversely proportional to the salary. So the decrease the paye the increase the salary.
Mkuu umechanganya vitu viwili mshahara (Basic Salary). Kushuka kwa PAYE hakuongezi mshahara, Bali inaongeza kiasi kinachobaki baada ya makato (take home). Hicho ndicho Rais alichosema.

Tunaendeleanamagufuli202-2025
 
Mkuu umechanganya vitu viwili mshahara(Basic Salary). Kushuka kwa PAYE hakuongezi mshahara, Bali inaongeza kiasi kinachobaki baada ya makato(take home). Hicho ndicho Rais alichosema.

Tunaendeleanamagufuli202-2025
Nakushasha PAYE nakupandisha makato ya loan board kunaongeza nini?.

Nini tofauti ya muajiriwa wa 2015 na muajiriwa wa 2020 katika kima Cha mshahara?.
 
Wafanya kazi japokuwa ni wachache ukilinganisha na Wapiga kura wengine lakini wanaweza kumfanya mbaya Magufuli tarehe 28 Octoba
Nasikia aliongeza shs 3000/= iweje mseme hajaongeza hiyo Kwan si nyongeza
 
Mkuu umechanganya vitu viwili mshahara(Basic Salary). Kushuka kwa PAYE hakuongezi mshahara, Bali inaongeza kiasi kinachobaki baada ya makato(take home). Hicho ndicho Rais alichosema.

Tunaendeleanamagufuli202-2025
Duuu
 
Naona chama kongwe hakiongelei hili jambo kwa kina katika kampeni zake.

Je, watumishi wajipange kufunga mkanda kwa miaka mitano mingine? Mshahara alioacha JK una nguvu ya kuhimili miaka kumi bila nyongeza?
 
Watumishi nchi hii wanajielewa bila shaka. Nitashangaa Sana kama hawatamuangusha John.

Yaani jitu limewaburuza miaka 5 halafu kwenye kamapeni linatamba siongezi mishahara lkn linaongeza ndege 5 halafu wasiliangushe?

Wanashindwaje wakati wao ndiyo wanahusika ktk zoezi la uchaguzi?
 
Back
Top Bottom