Elections 2010 Nimeshinda Kura za maoni Kuipepersuha Bendera ya CHADEMA

Elections 2010 Nimeshinda Kura za maoni Kuipepersuha Bendera ya CHADEMA

Status
Not open for further replies.
Mkuu hata mimi nilijiuliza hilo lakini nimefikiria kwa undani na hakika hana sababu ya kujitambulisha hapa kwani kura hazipigwi JF.

Sasa kwa nini kajitambulisha kama mgombea mtarajiwa hapa JF ? Wagombea wanapofanya kampeni kwenye TV, kwani kura zinapigwa kwenye TV? JF ni sawa na TV, ni media, na kama mgombea yuko hapa JF na ana access ya kujitambulisha na kufanya campaign hapa, lakini haitumii, mimi namuona hajiamini na hayuko serious katika campaign yake.Ni kama anaona privacy yake ni muhimu kuliko campaign na zaidi ya hapo anaonekana kama hajiamini kwamba atashinda, na hivyo anaogopa kuji expose for nothing.

Pili kama hukujiandikisha jimbo lake huwezi kumsaidia kwa kura ila kama anahitaji msaada ataandikia watu barua pepe.

Anajuaje kwamba wana JF hawajajiandikisha jimboni kwake ? Siku hizi mtandao upo kila kona TZ. Anajuaje kwamba hawezi ku spark cheche moja itakayoanzisha wildfire katika campaign yake ? Anajuaje anahitaji msaada wa aina gani na wa aina gani hahitaji ? Mpiga kampeni makini ni yule aliye tayari kusikiliza mawazo tofauti ya watu tofauti kuhusu kampeni yake, sasa watu watampa input gani ya maana wakati hata hawajui jimbo gani anagombea ?

Au kaja kutuambia anagombea ubunge kama showoff tu ?

Tatu, kama wewe upo jimboni kwake sidhani kama utampigia kura kwa sababu yupo JF isipokuwa kutokana na kujiuza kwa chama na YEYE hata kama akiwa ni Malaria_Sugu.

Right, lakini kama akitumia platform ya JF kutueleza mipango yake, atawapa nafasi watu kupata mambo fulani ambayo hawawezi kuyapata kirahisi kwa njia nyingine yoyote, mfano interactivity. Zaidi ya hayo, haki ya kupiga kura ni ya wananchi wa jimboni kwake, lakini hii haimaanishi mjadala wa mchakato wa ubunge unaishia kwa wananchi wa jimboni kwake, ingekuwa hivyo magazeti national yasingecover mbio za ubunge.Jf ni kama gazeti na watu wa JF wana haki ya kuuliza hata kama hawana haki ya kupiga kura. Sasa kama hataki kujitambulisha wengine watasema anaogopa maswali na hana skills za uongozi.

Haya ndiyo mabadiliko tunayotaka ? Wabunge waoga hata kufanya kampeni ? Kweli wanaweza kwenda kupingana na status quo ya ufisadi kwenye mjengo ?
 
Hongera sana rafiki! Umeanza vizuri, endelea kuweka mikakati zaidi hadi uifikie azma yako kuu. Hakuna kulala na ukitaka mawazo yetu zaidi usisite kutu PM maana mengine hayasemekani hapa bayana.
 
Hongera GS....Another bad news kwa mafisadi.
 
safi sana GS na nakutakia kila la kheriufanikiwe kushinda kwenye uchaguzi.Mungu akuepushe na mabaya yoyote, akujalie ufanikiwe kushinda na akupe moyo wa kutumikia jimbo lako kwa uaminifu.

kila la kheri mkuu.
 
Mgombea ubunge tayari kashaonyesha kukosa umakini katika maamuzi.

Kwa upande mmoja, anataka kufanya ugombea wake ubunge kuwa siri hapa JF, hivyo hataki kutuambia jimbo wala jina lake.

Kwa upande mwingine hawezi kuwa msetiri wa habari zake, baada ya kutaka kutoanika jina na jimbo lake, anakuja JF na kutumwagia mpunga, mpaka na vidokezo vya "wilaya yenye jimbo moja" kuturahisishia kazi.

Mgombea ubunge inaonekana anashindwa mtihani mdogo tu wa maamuzi, akifika njia panda anashindwa kuchagua njia ya kwenda, akitaka kuwa msiri anaishia kutoa siri, ataweza ku deal na classified documents za vita dhidi ya ufisadi ?

Strategy iko wapi? Solid decision making iko wapi? Huu ndio uongozi mbadala tunaousubiri? Uongozi unaoogopa kivuli chake wenyewe unawezaje kusimama against the CCM apparatus of Stalinistic machinations ?
 
Hongera sana ndugu yangu. Muda huu si wa kufanya siri ya jimbo, weka wazi wadau tukuongezee mbinu za kuishinda CCM maana kila jimbo lina mbinu yake.
 
naheshimu maamuzi yako na nakutakia kila la heri
 
Hongera sana ndugu yangu. Muda huu si wa kufanya siri ya jimbo, weka wazi wadau tukuongezee mbinu za kuishinda CCM maana kila jimbo lina mbinu yake.

Sema wewe labda watakuelewa.

Huwezi kufanya campaign ya public office kwa usiri, public does not go with usiri wa aina yoyote ile.You will be sending the wrong message, kwamba huna transparency na labda una kitu cha kuficha.
 
Wakuu,


Nimeandika historia kwa kuwa kijana wa kwanza kugombea kwenye jimbo hili tangu kurudi kwa mfumo wa vyama vingi kwa vyama vyote vilivyowahi kusimamisha wagombea ubunge kwenye jimbo hili. Ni mtaji kwangu..
Vizuri....
 
Tafadhali naomba msiniulize nagombea jimbo gani. Ni jimbo moja la Mkoani, Wilaya yenye jimbo moja.. Zaidi ya hapo usiniulize.

Alunta continua

Hii ni jeuri sasa. Kama hutaki kuulizwa yote hayo kwa nini umekuja kutuambia hapa kuwa umeshinda kura za maoni kwenye chama chako? Unachoogopa kuulizwa ni nini au kwa nini hutaki tusikuulize? Mantiki zingine bana...yaani hazina mbele wala nyuma.

Eti tusikuulize....tusikuulize kwani wewe ni nani? Ebo! Watu kama nyinyi hamfai kabisa kushika public office kwa sababu hamuelewi maana yake. Kama hutaki watu wakuulize maswali basi jitoe.

Mbunge gani mtarajiwa una jeuri hivyo.....Halafu kwani ukiulizwa unagombea jimbo gani nini kitaharibika? Kwa sababu siyo kwamba unamwaga mbinu na mikakati yako hadharani.....

Umeshanitibua na kwenye uchaguzi mkuu na ushindwe kwa sababu hustahili kuwatumikia watu wa jimbo lako.
 
Hii ni jeuri sasa. Kama hutaki kuulizwa yote hayo kwa nini umekuja kutuambia hapa? Unachoogopa ni nini? Mantiki zingine bana...yaani hazina mbele wala nyuma.

Eti tusikuulize....tusikuulize kwani wewe ni nani? Ebo! Watu kama nyinyi hamfai kabisa kushika public office kwa sababu hamuelewi maana yake. Kama hutaki watu wakuulize maswali basi jitoe.

Mbunge gani mtarajiwa una jeuri hivyo.....Halafu kwani ukiulizwa unagombea jimbo gani nini kitaharibika? Kwa sababu siyo kwamba unamwaga mbinu na mikakati yako hadharani.....

Umeshanitibua na kwenye uchaguzi mkuu na ushindwe kwa sababu hustahili kuwatumikia watu wa jimbo lako.

Yaani huyu jamaa kabla hata hatujafika katika kuchambua policies na strategies, yeye hata ile concept nzima ya public service haielewi.

Hapa mtu unapata mashaka kama kuna chochot kitafanyika, mtu ambaye hata kabla hajapata kuchaguliwa - yuko katika courtship na wananchi- anadiriki kuwaambia wananchi msiniulize ulize maswali, je mtu huyu akipata ubunge atakuwa na jeuri gani ?

I am sorry, mtu kama huyu kwangu anashindwa hata kabla hajaanza.Na kwa sababu hajatutajia jimbo sasa kawafanya wagombea ubunge wote wa CHADEMA kuwa suspect, kwa sababu kama mtu wa type hii ameshinda kura za maoni jimbo moja anaweza kushinda jimbo lolote.

Chama twawala visa vitupu, hawa wanaotaka kutushawishi kuwa mbadala nao visa vitupu. Basi nakonda tu.
 
.....Hongera natumaini utachukua jimbo tu, mjengo ule unakusubiri.
 
haaaaa haaaa haaaa! nimeipenda sentensi hiyo hapo juu! Loh!

Aaah Kibs, what gives? You've been missing in action for a minute. Is everything hunky dory? I heard it through the grapevine that you had matriculated at the London School of Oriental and African Studies to brush up on your English language proficiency. Is there any truth to that?
 
Aaah Kibs, what gives? You've been missing in action for a minute. Is everything hunky dory? I heard it through the grapevine that you had matriculated at the London School of Oriental and African Studies to brush up your English language your proficiency. Is there any truth to that?

Kibs ana bonge la gig BAKITA ndiyo maana ung'eng'e anakuwa hafagilii.
 
Hii ni jeuri sasa. Kama hutaki kuulizwa yote hayo kwa nini umekuja kutuambia hapa kuwa umeshinda kura maoni kwenye chama chako? Unachoogopa kuulizwa ni nini au kwa nini hutaki tusikuulize? Mantiki zingine bana...yaani hazina mbele wala nyuma.

Eti tusikuulize....tusikuulize kwani wewe ni nani? Ebo! Watu kama nyinyi hamfai kabisa kushika public office kwa sababu hamuelewi maana yake. Kama hutaki watu wakuulize maswali basi jitoe.

Mbunge gani mtarajiwa una jeuri hivyo.....Halafu kwani ukiulizwa unagombea jimbo gani nini kitaharibika? Kwa sababu siyo kwamba unamwaga mbinu na mikakati yako hadharani.....

Umeshanitibua na kwenye uchaguzi mkuu na ushindwe kwa sababu hustahili kuwatumikia watu wa jimbo lako.
..........Nyani Ngabu mbona unauaaaaaa :shock:
 
..........Nyani Ngabu mbona unauaaaaaa :shock:

Siui pasipo na sababu mtu wangu. Yeye mwenyewe kaja kututangazia hapa kuwa kashinda kura za maoni za chama chake kuwa mpeperusha bendera yao ya kiti cha ubunge ktk uchaguzi mkuu. Halafu kwa wakati huo huo hataki watu wamwulize maswali. Alaaaa.....kwa nini sasa hataki watu wamwulize maswali?

Kaanza vibaya. Sijui ndio u'rookie wenyewe huo au ni kukosa busara....I can't call it.

Ubunge ni utumishi wa umma (public service). Ukishaamua kujitolea kuingia ktk utumishi huo basi kuna baadhi ya mambo ya msingi wa mwanzo (elementary principles) ambayo unatakiwa kuyaelewa. Mojawapo ni kuwa tayari kujibu maswali kutoka kwa wananchi maana ndio hao utakaokuwa unawatumikia.

Sasa huyu anaanza na jeuri ya msiniulize maswali ya nagombea wapi? Kwani kusema unagombea sijui Kilombero au Ifakara huko kuna ubaya gani? Nini kitakachoharibika hapo?
 
Natumaini kampeni zenu zilikuwa za kimyakimya na hata hujazunguka ukajua ukubwa wa jimbo lako na wapiga kura wako wakakufahamu. CCM are very clever, kampeni zao wanazunguka jimbo zima hivyo kabla hata kampeni hazijaanza mgombea wao anafahamika jimboni na anafahamu kila uchochoro wa jimbo lake. Wewe wakati utakuwa unatumia muda mwingi ili watu wakufahamu, wenzio watakuwa kwenye hatua ya kueleza sera na kuomba kura. You need to work very hard to win
Mijitu mingine bwana halijui hata GS ni nani linafanya utabiri wa Yahya, ulitaka kila wanapoenda kufanya kampeni GS aku PM au akupigie simu LOL!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom