Nimesikiliza mahojiano ya Prof. Assad na Kikeke, huyu Prof. ana ujuaji mwingi. Unafukuzaje mfanyakazi akikataa kufanya majukumu ambayo sio yake?

Unafanya kazi gani? mkataba wako unasemaje?
 
Mwenye Hekima Suleimani aliandika

"Hata mpumbavu akinyamaza, huhesabiwa hekima; Akifumba midomo yake, huhesabiwa ufahamu.
Mithali 17:28
 
Nauza kitimoto, sina mkataba.
Una mfanyakazi nyumbani kusaidia kulea watoto una mpa kazi ya uhasibu? Anayekusaidia kuuza kiti moto unamwambia pia awe dereva wako au utamfukuza kazi akikataa?
 
Ila mikataba ya kazi pia inampa room kumpangia mtumishi majukumu mengine na mtumishi anapaswa kuyafanya provided that hayamdhalilishi.
Hii ndo nilikuwa naitafuta.

Huwenda mkataba ulikuwa unamruhusu kupangiwa kazi nyingine lakini mhusika hakujua kama mkataba unamruhusu hivyo akawa anakataa,najaribu kuwaza.
 
Una mfanyakazi nyumbani kusaidia kulea watoto una mpa kazi ya uhasibu? Anayekusaidia kuuza kiti moto unamwambia pia awe dereva wako au utamfukuza kazi akikataa?
Uhasibu ni kazi ya kitaaluma, kazi za nyumbani kwangu hazihusiani na biashara yangu ya kitimoto, anayeuza kitimoto kwangu anaweza pia kuwa dereva wangu au nikamtuma sokoni kuleta ndizi mzuzu za kuuzia na kitimoto pamoja na viungo vya kutengenezea rosti ya kitimoto.
 
Kupanga files unahitaji taaluma?, tuwe serious na maisha. Watoto wangu weekend huja ofisini na husaidia kupanga files, kwani aliambiwa aandike references?
Sana tu, tena mafaili ya serikali. Uhasibu, ukiuza siri, faili, watu wanapiga bilioni, lazima kuwe na system ya ku- record, ku-trace, ku- verify every file. Comprising systems, vitu viwekwe kwa mpangilio.
 
Sana tu, tena mafaili ya serikali. Uhasibu, ukiuza siri, faili, watu wanapiga bilioni, lazima kuwe na system ya ku- record, ku-trace, ku- verify every file. Comprising systems, vitu viwekwe kwa mpangilio.
Watumishi wa serikali wanaajirwa na utumishi na hawawezi kufukuzwa kazi na CAG.
 
Tatizo ni dharau yenu kwa dereva. Kuna tofauti gani kati ya dereva anayemwendesha CAG, Rais, basi la watu 80, pilot au dereva,wa treni? Akiamua kuwapoteza ni dakika sifuri ajali kwa upande wako. Hata dada anakusaidia kupika unahitaji kumuheshimu na mkataba wake, anaangalia afya yako, watoto wako. Huko Ulaya analipwa vizuri sana na haki zake zinaheshimiwa vizuri.
 
Prof. Assad ana uchu wa madaraka sana na anajifanya anajua kuliko wote, na mbaya zaidi ni mbishi sana, sio mtu wa kupewa maelekezo na kupokea
 
Tatizo ni dharau yenu kwa dereva. Kuna tofauti gani kati ya dereva anayemwendesha CAG, Rais, basi la watu 80, pilot au dereva,wa treni? Akiamua kuwapoteza ni dakika sifuri ajali kwa upande wako.
Udereva ni mojawapo ya life skills, ila sio taaluma kama pilot au dereva wa treni.
Kama hana matatizo ya akili dereva hawezi tu kuamua kuwapoteza watu kwa sababu na yeye anaweza kujipoteza atakapojaribu kufanya hivyo.
 
Udereva ni mojawapo ya life skills, ila sio taaluma kama pilot au dereva wa treni.
Kama hana matatizo ya akili dereva hawezi tu kuamua kuwapoteza watu kwa sababu na yeye anaweza kujipoteza atakapojaribu kufanya hivyo.

Kila kitu ni life skills. Kwako life skills ni nini? Unafikiri tulifanyaje biashara kwa maelfu ya miaka bila hiko cheti chako cha uhasibu, kabla ya University of Dar (UDSM) haijaundwa?
 
Kila kitu ni life skills. Kwako life skills ni nini? Unafikiri tulifanyaje biashara kwa maelfu ya miaka bila hiko cheti chako cha uhasibu, kabla ya University of Dar (UDSM) haijaundwa?
Umepaniki,
 
Mhasibu hasomei manunuzi, hr na uhasibu?. Zote hizi ni sehemu ya kozi yake.
Kwa hiyo Hr anaweza fanya kazi za sheria kisa kasoma labour laws? Political scientist kuwa mchumi kisa kasoma political economy? Huko uliko baki hukohuko
 
Ukiona mtu muoga jua kuwa ni mjinga bado maana uoga ni ishara ya ujinga. Pro anajiwelewa na kujiamini ndiyo maana hana uoga. Huwezi kutolewa kwenye nafasi yake kiuni na yeye akae kimya tu. Waafrika tuna shida sana kifra
Sasa kulia Lia ndiyo suluhisho? Kila akihojiwa lazima alilie u CAG? Hizo akili za kulilia nafasi kama mtoto wa kambo aachane nazo... Yeye sio wa kwanza kupigwa chini
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…