Nimesikiliza mahojiano ya Prof. Assad na Kikeke, huyu Prof. ana ujuaji mwingi. Unafukuzaje mfanyakazi akikataa kufanya majukumu ambayo sio yake?

Nimesikiliza mahojiano ya Prof. Assad na Kikeke, huyu Prof. ana ujuaji mwingi. Unafukuzaje mfanyakazi akikataa kufanya majukumu ambayo sio yake?

Wakati akihojiwa na Salim Kikeke,

Aliyewahi kuwa CAG na kuondolewa kwa aibu kuu Prof. Assad anadai kuna mtumishi huko Morogoro aliajiriwa kama Dereva.

Lakini kwakuwa hakuwa na mtu wa kumuendesha basi wakaamua wawe wanampa kazi ya kupanga mafaili.

Jamaa baada ya kuona anafanya kazi ambazo sio zake akaamua kuandika barua akidai alipwe kwa kufanya kazi ambazo sio zake.

Huyu Prof msomi na mshika dini akamuamuru HR amfukuze kazi huyo dereva.

Hapa tunasikiliza mahojiano ya Prof. Akilalamika kufutwa kazi bila utaratibu lakini wakati huo huo anatueleza bila aibu kitendo chake cha kinyama cha kumfuta mtumishi kazi kwa kudai haki zake.

Kwa elimu yake hiyo anaona ni sahihi kwa dereva kufanya kazi za kupanga file badala ya kuendesha gari kulingana na mkataba wa ajira yake??

Je yeye huyo Prof. Angeambiwa akadeki korido pale UDSm badala ya kufundisha wanafunzi kukariri madesa angefanya hivyo.

Ama kweli binadamu ni wasahaulifu sana na wanafiki mno.

Huyu keshasahau namna alivyomtenda mwenzake anaona ni haki yake kuonea wengine kwa kuwa kasoma sana ila wenzake hawana haki ya kumfuta yeye kazi.

Such an arrogant and a very useless academician.


View: https://youtu.be/eE2JoDEd43Q?si=vgPL1ihKxMpsLtel

Na yeye mwenyewe alivyotemwa mpaka Leo analalamika
 
Hata mimi nilimshangaa ,

Unajisifiaje kumuachisha mtu kazi kwa kukataa kufanya majukumu ambayo sio yake kimkataba??

Wangemwambia wanapunguza madereva kazini kumpa mafao yake yote na kutangaza na kuajiri office admistrator angetaka angeomba hiyo kazi akijua anaomba kazi gani. Alichofanya ni dharau kubwa kwa madereva na proffessional yao.
 
Back
Top Bottom