Nimetapeliwa hela na rafiki wa karibu

Nimetapeliwa hela na rafiki wa karibu

KING ASSENGA

JF-Expert Member
Joined
Oct 8, 2016
Posts
928
Reaction score
1,478
Ndugu zangu, jihadharini sana na marafiki wa karibu hasa kwenye maswala yanayohusu hela. Nimekutwa na utapeli wa aina ambayo yeyote mwenye rafiki anayemwamini hawezi kutoboa kwenye utapeli huo.

Huyu rafiki nilimkuta mwaka 2021 huko Iringa kwenye mazingira ya kilimo cha nyanya. Alikuwa muungwana kabisa, tena church boy kweli kweli. Tulikaa sehemu moja geto, tulikuwa watu watatu mpaka nilipohama Iringa, na sikuwahi kuona tabia yake mbovu yoyote.

Baada ya mwaka 2021, mimi niliondoka na kuendelea na harakati zangu Dar es Salaam mpaka leo hii. Baada ya muda mfupi, alidai alipoteza simu na hivyo kupoteza namba zangu, na mimi pia nilipoteza namba zake. Niliporudia namba zangu nilizokuwa natumia kabla ya kuikimbia Dar kwa ajili ya kukwepa depression na anguko zaidi la kibiashara, basi tulikutana tena Dar kwenye mwezi wa Januari, tarehe 4.

Aliniona kwenye biashara yangu ya magodoro na electronics mitaa ya wilaya ya Ubungo. Ilikuwa kama surprise. Baada ya kama wiki mbili, tukiwa karibu sana, aliniambia kuna fursa ya hela kama ningekuwa na mtaji wa milioni tano au zaidi anishirikishe hiyo fursa. Nikamjibu kwamba kwa sasa nipo vibaya sana, huwezi kuamini sina hata milioni moja kwenye akaunti ya benki ya nje ya biashara nilizonazo.

Basi akaniambia tarehe 21 nitafute milioni mbili na nusu tu ya kuanzia anishirikishe dili lenyewe. Nikamjibu sawa kwa alivyokuwa mpambanaji, niliamini kabisa itakuwa fursa maana uvaaji wake na kuwa na gari juu ndani ya miaka mitatu tu tuliyopotezana, bila shaka itakuwa ishu ya maana. Basi siku hiyo akaja na gari fresh, nikazama ndani. Walikuwa wawili, yeye na jamaa mmoja bonge kinoma, na akaenda hewani. Basi tukawa tunapiga stori, tukitoka nilipokuwa kufika mahali, rafiki yangu akaniambia umebeba hela hiyo milioni mbili na nusu. Nikamjibu ndio, basi akaanza kuongelea fursa yenyewe.

Wanaita utakatishaji fedha. Wanaambatanisha noti za elfu kumi original na karatasi flani nyeusi wanaita "nega" au "black money" ambazo wanadai hela hazitolewi nje zikiwa kamili. Zinakuja kama hayo makaratasi meusi na yanakuwa ni hela ila hayana baadhi ya nembo, na ukiziambatanisha hizo karatasi na noti ya elfu kumi na kumwagia chemical, zote zinakuwa nyeusi. Ukisafisha na chemical tofauti, zote zinakuwa noti kamili za elfu 10. Sijawahi kukutana na utapeli wa namna hii, ila nilipinga baada ya kuelezwa na kuoneshwa mfano.

Basi, baada ya kuweka msimamo sana, rafiki yangu ananijua vizuri nikishapinga jambo, basi akasimamisha gari sehemu flani. Alibaki kwenye gari akawa anapiga simu. Tayari hisia zangu zilinipeleka kuwa nipo kwenye hatari. Basi rafiki yangu akaniambia, "Unajua nini hapa? Ushajua siri ya kundi hatari na hawawezi kukuacha salama. Wewe toa hizo milioni mbili zifanyiwe utakatishaji upate hela zako nao wapate chao, alafu utaangalia namna ya kuja kujitoa bila tatizo zaidi. Unaona gari ya nyuma Alphard? Wapo watu watano na silaha, hivyo upo hatarini." Muda uleule kuna Alphard iliingia, plate namba ilifunikwa.

Nakuja kutuweka kati, basi nikaingia kwenye gari tukaenda hotel flani, wakafanya yao. Mwisho wakasingizia chemical imeganda, wakaniacha na yale makaratasi meusi, wakatoweka, na mimi sikukaa, nikatoweka zangu pia. Nikiwa na maumivu ya milioni mbili, lakini niliendelea kuwapigia simu kujifanya sijashtuka nishatapeliwa. Waliendelea kusema watarudi, ila hawakurudi na hawakujua nishatoka pale.

Basi baada ya kuendelea kumtafuta rafiki yangu, akanijulisha chemical ya kusafishia mzigo chini ya milioni 10 umekwisha, hivyo nijitahidi nipate 4M naye atafute 4M ili mzigo usafishwe. Basi nikawa mkali sana kwa kujifanya kwanini wamemwagia chemical kama kuwa hawana uhakika wa chemical ya kusafishia hela zingine. Wakijua sijashtuka, walichoniachia ni makaratasi meusi. Basi niliwatamanisha kupata hiyo 4M na wakaingia mkenge kwa akili sana. Nikamkamatisha rafiki yangu kwa polisi, akakaa ndani, wenzie walikimbia.

Alikuja kudhaminiwa baada ya wiki moja na kujaribu kuomba alipe ili kesi isiende mahakamani. Alidai hana uwezo kwani fedha zilibebwa na kundi, hivyo anaomba nimpe muda wa mwezi na atatoa ushirikiano wa kuwakamata wengine. Basi nikaacha kama lilivyo, nasubiri kulipwa au akishindwa, kesi iende mahakamani japokuwa sina uzoefu wa huko.

Mnalipi la kunishauri ili nipate fedha zangu? Na sina uzoefu na mambo ya sheria, hata polisi sina nako mazoea.
 

Attachments

  • PXL_20250223_101555630.jpg
    PXL_20250223_101555630.jpg
    443.8 KB · Views: 2
Kubali matokeo. Hao matapeli hawana pesa za kukulipa, zaidi ukisema uende mahakamani utaendelea kutumia pesa ambazo hujui zitarudi vipi.
 
Hiyo mzee inaitwa WASH WASH, michezo hiyo ilifanyika sana Nigeria enzi hizo.

Unapewa makaratasi meusi, ukiyaosha kwa chemicals ule weusi unatoka inabaki noti kamili.

Michezo wanayofanya, wanazipaka noti chache za elfu kumi huo weusi, kisha mengine yanakua makaratasi tupu nayo wanayapaka rangi nyeusi, hivyo unakua mzigo mzigo mwingiiii kumbe unaeza kukuta hela halali haizidi elfu 50.

Ukija wewe wanachukua karatasi moja kwenye mfuko (ambayo ni noti halali,) wanamwagia chemicals ule weusi unatoka unaliona teni halisi.

Kisha wanakuonyesha mfuko uliojaa makaratasi na kukwambia zote ni noti, unachotakiwa kuwa nacho ni chemicals tu, kwa hiyo unajikuta unatoa hela wanakuuzia chemicals kisha haoooo.

Wewe sasa unajifungia ndani kuanza kuosha, unakuta umeachiwa shangazi kaja limejaa makaratasi basi unapagawa unajiona milionea tayari ukiosha unashangaa noti halali ni chache, mengine ni makaratasi tu


View: https://youtu.be/n7_jlp1_MLg?si=HvFTZNRhQyWoaDvY

Utapeli wa hivi kuna mjamaa aliufanya kwenye meli miaka ya nyuma huko, alitengeneza kimashine kinatoa hela, akawadanganya watu, hiyo mashine ina uwezo wa ku print hela kila baada ya lisaa inaprint noti moja ya dola mia.

Watu walivyoona wakapagawa, akawauzia kimashine, mpaka meli inatia nanga bado kina print
 
Ndugu zangu, jihadharini sana na marafiki wa karibu hasa kwenye maswala yanayohusu hela. Nimekutwa na utapeli wa aina ambayo yeyote mwenye rafiki anayemwamini hawezi kutoboa kwenye utapeli huo.

Huyu rafiki nilimkuta mwaka 2021 huko Iringa kwenye mazingira ya kilimo cha nyanya. Alikuwa muungwana kabisa, tena church boy kweli kweli. Tulikaa sehemu moja geto, tulikuwa watu watatu mpaka nilipohama Iringa, na sikuwahi kuona tabia yake mbovu yoyote.

Baada ya mwaka 2021, mimi niliondoka na kuendelea na harakati zangu Dar es Salaam mpaka leo hii. Baada ya muda mfupi, alidai alipoteza simu na hivyo kupoteza namba zangu, na mimi pia nilipoteza namba zake. Niliporudia namba zangu nilizokuwa natumia kabla ya kuikimbia Dar kwa ajili ya kukwepa depression na anguko zaidi la kibiashara, basi tulikutana tena Dar kwenye mwezi wa Januari, tarehe 4.

Aliniona kwenye biashara yangu ya magodoro na electronics mitaa ya wilaya ya Ubungo. Ilikuwa kama surprise. Baada ya kama wiki mbili, tukiwa karibu sana, aliniambia kuna fursa ya hela kama ningekuwa na mtaji wa milioni tano au zaidi anishirikishe hiyo fursa. Nikamjibu kwamba kwa sasa nipo vibaya sana, huwezi kuamini sina hata milioni moja kwenye akaunti ya benki ya nje ya biashara nilizonazo.

Basi akaniambia tarehe 21 nitafute milioni mbili na nusu tu ya kuanzia anishirikishe dili lenyewe. Nikamjibu sawa kwa alivyokuwa mpambanaji, niliamini kabisa itakuwa fursa maana uvaaji wake na kuwa na gari juu ndani ya miaka mitatu tu tuliyopotezana, bila shaka itakuwa ishu ya maana. Basi siku hiyo akaja na gari fresh, nikazama ndani. Walikuwa wawili, yeye na jamaa mmoja bonge kinoma, na akaenda hewani. Basi tukawa tunapiga stori, tukitoka nilipokuwa kufika mahali, rafiki yangu akaniambia umebeba hela hiyo milioni mbili na nusu. Nikamjibu ndio, basi akaanza kuongelea fursa yenyewe.

Wanaita utakatishaji fedha. Wanaambatanisha noti za elfu kumi original na karatasi flani nyeusi wanaita "nega" au "black money" ambazo wanadai hela hazitolewi nje zikiwa kamili. Zinakuja kama hayo makaratasi meusi na yanakuwa ni hela ila hayana baadhi ya nembo, na ukiziambatanisha hizo karatasi na noti ya elfu kumi na kumwagia chemical, zote zinakuwa nyeusi. Ukisafisha na chemical tofauti, zote zinakuwa noti kamili za elfu 10. Sijawahi kukutana na utapeli wa namna hii, ila nilipinga baada ya kuelezwa na kuoneshwa mfano.

Basi, baada ya kuweka msimamo sana, rafiki yangu ananijua vizuri nikishapinga jambo, basi akasimamisha gari sehemu flani. Alibaki kwenye gari akawa anapiga simu. Tayari hisia zangu zilinipeleka kuwa nipo kwenye hatari. Basi rafiki yangu akaniambia, "Unajua nini hapa? Ushajua siri ya kundi hatari na hawawezi kukuacha salama. Wewe toa hizo milioni mbili zifanyiwe utakatishaji upate hela zako nao wapate chao, alafu utaangalia namna ya kuja kujitoa bila tatizo zaidi. Unaona gari ya nyuma Alphard? Wapo watu watano na silaha, hivyo upo hatarini." Muda uleule kuna Alphard iliingia, plate namba ilifunikwa.

Nakuja kutuweka kati, basi nikaingia kwenye gari tukaenda hotel flani, wakafanya yao. Mwisho wakasingizia chemical imeganda, wakaniacha na yale makaratasi meusi, wakatoweka, na mimi sikukaa, nikatoweka zangu pia. Nikiwa na maumivu ya milioni mbili, lakini niliendelea kuwapigia simu kujifanya sijashtuka nishatapeliwa. Waliendelea kusema watarudi, ila hawakurudi na hawakujua nishatoka pale.

Basi baada ya kuendelea kumtafuta rafiki yangu, akanijulisha chemical ya kusafishia mzigo chini ya milioni 10 umekwisha, hivyo nijitahidi nipate 4M naye atafute 4M ili mzigo usafishwe. Basi nikawa mkali sana kwa kujifanya kwanini wamemwagia chemical kama kuwa hawana uhakika wa chemical ya kusafishia hela zingine. Wakijua sijashtuka, walichoniachia ni makaratasi meusi. Basi niliwatamanisha kupata hiyo 4M na wakaingia mkenge kwa akili sana. Nikamkamatisha rafiki yangu kwa polisi, akakaa ndani, wenzie walikimbia.

Alikuja kudhaminiwa baada ya wiki moja na kujaribu kuomba alipe ili kesi isiende mahakamani. Alidai hana uwezo kwani fedha zilibebwa na kundi, hivyo anaomba nimpe muda wa mwezi na atatoa ushirikiano wa kuwakamata wengine. Basi nikaacha kama lilivyo, nasubiri kulipwa au akishindwa, kesi iende mahakamani japokuwa sina uzoefu wa huko.

Mnalipi la kunishauri ili nipate fedha zangu? Na sina uzoefu na mambo ya sheria, hata polisi sina nako mazoea.
Bore utoe kuliko kukopesha utaumia
 
Ilibidi umkatae ili first day anakuletea pigo za kishamba.
Komaa akulipe chako mchezo uishe hvyo kama vipi acha akaolewe na kaka nyapala
 
Duh pole sana mkuu. Watu wanasema ukipotezana na mtu kwa zaidi ya miaka miwili ukija kukutana nae anakuwa sio Yule uliekuwa unamjua
Looh, pole sana maana utapeli umetamalaki
 
Ndugu zangu, jihadharini sana na marafiki wa karibu hasa kwenye maswala yanayohusu hela. Nimekutwa na utapeli wa aina ambayo yeyote mwenye rafiki anayemwamini hawezi kutoboa kwenye utapeli huo.

Huyu rafiki nilimkuta mwaka 2021 huko Iringa kwenye mazingira ya kilimo cha nyanya. Alikuwa muungwana kabisa, tena church boy kweli kweli. Tulikaa sehemu moja geto, tulikuwa watu watatu mpaka nilipohama Iringa, na sikuwahi kuona tabia yake mbovu yoyote.

Baada ya mwaka 2021, mimi niliondoka na kuendelea na harakati zangu Dar es Salaam mpaka leo hii. Baada ya muda mfupi, alidai alipoteza simu na hivyo kupoteza namba zangu, na mimi pia nilipoteza namba zake. Niliporudia namba zangu nilizokuwa natumia kabla ya kuikimbia Dar kwa ajili ya kukwepa depression na anguko zaidi la kibiashara, basi tulikutana tena Dar kwenye mwezi wa Januari, tarehe 4.

Aliniona kwenye biashara yangu ya magodoro na electronics mitaa ya wilaya ya Ubungo. Ilikuwa kama surprise. Baada ya kama wiki mbili, tukiwa karibu sana, aliniambia kuna fursa ya hela kama ningekuwa na mtaji wa milioni tano au zaidi anishirikishe hiyo fursa. Nikamjibu kwamba kwa sasa nipo vibaya sana, huwezi kuamini sina hata milioni moja kwenye akaunti ya benki ya nje ya biashara nilizonazo.

Basi akaniambia tarehe 21 nitafute milioni mbili na nusu tu ya kuanzia anishirikishe dili lenyewe. Nikamjibu sawa kwa alivyokuwa mpambanaji, niliamini kabisa itakuwa fursa maana uvaaji wake na kuwa na gari juu ndani ya miaka mitatu tu tuliyopotezana, bila shaka itakuwa ishu ya maana. Basi siku hiyo akaja na gari fresh, nikazama ndani. Walikuwa wawili, yeye na jamaa mmoja bonge kinoma, na akaenda hewani. Basi tukawa tunapiga stori, tukitoka nilipokuwa kufika mahali, rafiki yangu akaniambia umebeba hela hiyo milioni mbili na nusu. Nikamjibu ndio, basi akaanza kuongelea fursa yenyewe.

Wanaita utakatishaji fedha. Wanaambatanisha noti za elfu kumi original na karatasi flani nyeusi wanaita "nega" au "black money" ambazo wanadai hela hazitolewi nje zikiwa kamili. Zinakuja kama hayo makaratasi meusi na yanakuwa ni hela ila hayana baadhi ya nembo, na ukiziambatanisha hizo karatasi na noti ya elfu kumi na kumwagia chemical, zote zinakuwa nyeusi. Ukisafisha na chemical tofauti, zote zinakuwa noti kamili za elfu 10. Sijawahi kukutana na utapeli wa namna hii, ila nilipinga baada ya kuelezwa na kuoneshwa mfano.

Basi, baada ya kuweka msimamo sana, rafiki yangu ananijua vizuri nikishapinga jambo, basi akasimamisha gari sehemu flani. Alibaki kwenye gari akawa anapiga simu. Tayari hisia zangu zilinipeleka kuwa nipo kwenye hatari. Basi rafiki yangu akaniambia, "Unajua nini hapa? Ushajua siri ya kundi hatari na hawawezi kukuacha salama. Wewe toa hizo milioni mbili zifanyiwe utakatishaji upate hela zako nao wapate chao, alafu utaangalia namna ya kuja kujitoa bila tatizo zaidi. Unaona gari ya nyuma Alphard? Wapo watu watano na silaha, hivyo upo hatarini." Muda uleule kuna Alphard iliingia, plate namba ilifunikwa.

Nakuja kutuweka kati, basi nikaingia kwenye gari tukaenda hotel flani, wakafanya yao. Mwisho wakasingizia chemical imeganda, wakaniacha na yale makaratasi meusi, wakatoweka, na mimi sikukaa, nikatoweka zangu pia. Nikiwa na maumivu ya milioni mbili, lakini niliendelea kuwapigia simu kujifanya sijashtuka nishatapeliwa. Waliendelea kusema watarudi, ila hawakurudi na hawakujua nishatoka pale.

Basi baada ya kuendelea kumtafuta rafiki yangu, akanijulisha chemical ya kusafishia mzigo chini ya milioni 10 umekwisha, hivyo nijitahidi nipate 4M naye atafute 4M ili mzigo usafishwe. Basi nikawa mkali sana kwa kujifanya kwanini wamemwagia chemical kama kuwa hawana uhakika wa chemical ya kusafishia hela zingine. Wakijua sijashtuka, walichoniachia ni makaratasi meusi. Basi niliwatamanisha kupata hiyo 4M na wakaingia mkenge kwa akili sana. Nikamkamatisha rafiki yangu kwa polisi, akakaa ndani, wenzie walikimbia.

Alikuja kudhaminiwa baada ya wiki moja na kujaribu kuomba alipe ili kesi isiende mahakamani. Alidai hana uwezo kwani fedha zilibebwa na kundi, hivyo anaomba nimpe muda wa mwezi na atatoa ushirikiano wa kuwakamata wengine. Basi nikaacha kama lilivyo, nasubiri kulipwa au akishindwa, kesi iende mahakamani japokuwa sina uzoefu wa huko.

Mnalipi la kunishauri ili nipate fedha zangu? Na sina uzoefu na mambo ya sheria, hata polisi sina nako mazoea.
Ccm ni wapumbavu sana
 
Wazee wa Kolongwee hao.Ebwana pole sana mkuu sema liwe somo kwako.Michezo hiyo mara ya kwanza niliiona Jhb.
 
Back
Top Bottom