Nimetoa mahari ya Tsh. laki nane (8) nyumbani kwao na mzazi mwenzangu na wamenikabidhi binti yangu (mwanangu) ili nimsomeshe

Nimetoa mahari ya Tsh. laki nane (8) nyumbani kwao na mzazi mwenzangu na wamenikabidhi binti yangu (mwanangu) ili nimsomeshe

Kuna wapare wametaka kuniletea hii story.. nimeachana nao mtoto atakuja mwenyewe. Mwanamke mwenyewe Ana mabwana kibao mahari nilipe mie.. isitoshe Nina Mke niliyemlipia.. silipi mahari Mara mbili ni laana.
Hahahah wapare gani wenye akili za kijinga namna hio
 
Yaan unajua kbs mawasiliano yalipotea ukiwa safarini halafu akasafiri wewe unaumia nn? Eti msiri. Huoni kama wewe ndo una matatizo?

Halaf hiyo ni fine siyo mahari
 
Huwa naona kabisa huko mbeleni nitanyimwa Mke. Hizi habari za mahari ya milioni, pesa ndani ya barua ya posa, faini ya kumtia binti yao mimba, mkaja wa nani sijui, blanketi la nani, koti la nani, kuwafungua vinywa wazee.
Huna hela??
Mahari...1,000,000 (negotiable)
Posa...50,000 au 100,000
Faini ya uchafuzi...300,000
Mkaja ....300,000
Blanket 2....150,000
Jembe 2 na mipini....15,000
Kipanga(Kama ni Mbeya)...300,000
Mengine..(mbuzi/ndama)...400,000
Kumtoa kidogo mshenga......!!!
Usafiri wako, mshenga, wazazi wako, mashangazi zako, wasindikizaji n.k.....!
 
Una tamaa sana ndugu uliamua tu kumpotezea mda wake ili hali ukuwa tayari kumiliki ndoa
 
Ukimzalisha binti wa watu halafu bado hamjaoana, ikitokea mmeachana ili upate haki ya mtoto ni lazima umlipie mahali huyo mtoto ndio unakuwa na mamlaka nae.
Kwetu tunaita kumkomboa mtoto na hata kama unaishi na mwanamke haujamuoa itokee bahati mbaya amefariki unalipishwa mahari na unaruhusiwa kumzika mkeo sababu umeshamlipia mahari
 
Huna hela??
Mahari...1,000,000 (negotiable)
Posa...50,000 au 100,000
Faini ya uchafuzi...300,000
Mkaja ....300,000
Blanket 2....150,000
Jembe 2 na mipini....15,000
Kipanga(Kama ni Mbeya)...300,000
Mengine..(mbuzi/ndama)...400,000
Kumtoa kidogo mshenga......!!!
Usafiri wako, mshenga, wazazi wako, mashangazi zako, wasindikizaji n.k.....!
Ndugu, mimi siishi kwa mazoea na sio kwamba hiyo mahari muda ukifika siwezi ipata! Ni utaratibu wangu niliojiwekea, wakikataa basi wakae na binti yao. Mimi nilishasema, mabinti zangu sitowauza, nitawabariki yeye na mwenzie wakaanze maisha yao yenye raha na furaha katika ndoa yao.
 
Ndoa iko moja tu wewe hakuna ndoa zaidi ya hiyo. Ndiyo nyinyi mnaoharibu Kiswahili na madikteta kuwaita Wazalendo. Kulipa pesa kwa ME ili apewe mtoto wake kutoka kwa KE ambaye hakuwahi kuwa mke wake hiyo si ndoa, haijawahi kuitwa ndoa hata kwa sekunde moja. Acha kutuharibia kiswahili.

Ulianza vema kwa kukiri hujaelewa, nafikiri kiungwana ilitosha kabisa kuelekezwa…. sasa huku umeamua kupuyanga tena.

Ni wapi na nani kasema hii ni ndoa?
 
Ndugu, mimi siishi kwa mazoea na sio kwamba hiyo mahari muda ukifika siwezi ipata! Ni utaratibu wangu niliojiwekea, wakikataa basi wakae na binti yao. Mimi nilishasema, mabinti zangu sitowauza, nitawabariki yeye na mwenzie wakaanze maisha yao yenye raha na furaha katika ndoa yao.

Subiri ukue kwanza, utauvuka mto pale tu utapoufikia…. unaongelea mabinti ambao hata hujawapata!
 
Hiyo ni faini na siyo mahari, kila lakheri.

Iite faini au vyovyote, ila inatolewa kwa mfumo wa mapatano kama ilivyo mahari.

Bila hiyo:

1. Ikitokea mtoto huyo amefariki (God forbid) hatozikwa kwenye shamba lenu.

2. Ikitokea mtoto huyo (kama ni binti) akiolewa, mahari yake hutapokea wewe.

Ni mtoto wako sawa, ila huna mamlaka juu yake…. na kuna heshima nyingi utanyimwa.

Usishangae hata meza kuu siku ya harusi yake ukafukuzwa.[emoji1493][emoji1493][emoji1493][emoji28]
 
Huu ujinga wako wa mahari na ndoa eti ziko za aina nyingi kawadanganye wa shule za kata wenzio siyo humu. Mahari inatolewa na mume mtarajiwa kwa mke mtarajiwa na si kwa mtoto na mzazi wake na ndoa ni ni ya mke na mume tu hakuna ndoa ya mzazi na mwanae awe wa kike wala wa kiume. Shule za kata na walimu wa kuunga kwa gundi wametia tope kwenye kichwa chako. Kupotosha Kiswahili kafanye kwingine siyo humu.
Hata mana ya ndoa hujui..don't waste my energy rudi shule naona na poteza muda kumwelewesha layman.

#MaendeleoHayanaChama

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hiyo ndiyo maana halisi ya mahari si hizi wanakuja nazo wasiojua Kiswahili kutaka kupitosha.
Kwetu tunaita kumkomboa mtoto na hata kama unaishi na mwanamke haujamuoa itokee bahati mbaya amefariki unalipishwa mahari na unaruhusiwa kumzika mkeo sababu umeshamlipia mahari
 
Kuna wapare wametaka kuniletea hii story.. nimeachana nao mtoto atakuja mwenyewe. Mwanamke mwenyewe Ana mabwana kibao mahari nilipe mie.. isitoshe Nina Mke niliyemlipia.. silipi mahari Mara mbili ni laana.
Usiangaike mkuu mimi waliniletea za hivyo Bibi yangu akanambia Achana na habari za mtoto kama wamemkatalia watakutafuta wenyewe au mtoto atakuja mwenyewe, Baada ya mwaka wakapiga simu njoo uchukue mwanao, Ni baada ya mama mtoto kuanza kurukaruka na kuwaachia mzigo wa nyumbani kwao, nikamchukua kiulaini
 
Naona kuna wadau humu hawaelewi mila na desturi za makabila mengine. Wanataka kuleta uswahili na ujuaji. Chamsingi jifunze elewa mleta mada yuko sahihi, asisahihishwe.
Kwa kumzalisha mtoto wa watu unapaswa kuoa,ili uoe utatoa mahari. Lakini hata usipomuoa utatoa mahari na uamuzi ni wako umchukue mama yake au uondoke na mtoto tu. Labda mama mtoto akiwa ameolewa tyr bado utatoa mahari ili uondoke kihalali na mwanao.
 
Mkuu, Sijakuelewa. Ulibreak mahusiano halafu ukaenda kumlipia mahari huyo mzazi mwezio. Sasa tatizo lipo wapi?.

Tukio la wewe kupewa mtoto wako mbona ni haki yako au Ulinyimwa kupewa Mwanao hadi ulipe fedha za matunzo ya Mtoto?.
Wanaita kukomboa mtoto.

#YNWA
 
  • Thanks
Reactions: Auz
Back
Top Bottom