Nimetoka ukweni Kigoma, ila kama hii ndiyo aina ya wazee acha wabaki na watoto wao!

Vitu vidogo Sana hivyo sema u bado mdogo
Mahari hata iwe milioni 100 Huwa hakuna anaemaliza mahari,hizo ni figure tu.
We zaa tu,ishaisha hio
 
Pole best. Mke anakupenda Kwa dhati nadhani mpende pia. Wazazi wake fanya kuwasamehe lakini usiende tena kigoma. Mwisho funga ndoa harali ikibidi bila hata wazazi wake kuwepo ili likitokea la kutokea uwe on safe place

Engineer, afunge ndoa bila ridhaa ya wazazi kwa tamaduni zetu? Hiyo ni a time bomb! Balaa kubwa!
 
Kujitia umwamba kwa vitu vya namna hii haifai n'a ni tabia mbaya kabisa, sasa akibaki na mtoto wake atamuoa yeye???
Mlikutana/walikutana chuo ,kutoka kigoma nani alifanikisha mtia mimba au mzazi ,kama ndivyo ilipwe

Swala la kumtukana mkwe ,haisaidii ukigoma ,nakushauri kakomboe mtoto fasta
 
Nimetafakari sanaaa, nampenda sana mama wa mtoto wangu lakini sina namna zaidi ya kumuacha aendeee kuepusha Shari za baadaye!
Kosa kubwa Sana endapo atafanya hvo au kama ameshafanya. Ikumbukwe mama mkwe alimuelewa mwamba kasoro bamkwe.

Laana ya Baba hua haifanyi kazi coz wakat mungine pombe ndio hua zinaongea
 
Mkuu kabla hujaachana na huyo dada hemu nitumie namba yake pm na jina lako ili nijitambulishe kama shemeji yake [emoji4]
 
Ushaambiwa hao watu hawana huruma na huyo mjukuu wao.
Jamaa akizingua wanamdedisha ili binti yao aolewe.

Sasa we endelea kumpa ushujaa uchwara.
Jamaa ni mbinafsi.
 
We fala Nini unaoa mama yake au baba yake,nyie ndo mnatualibia watoto mnawazalisha na kuwaacha buladifakini Sasa ukitaka tukutoe kafara mrudishie mtoto wetu Kijijini uone.utakufa mchana kweupe

Komaa na Binti muoe Wewe Cha kufanya mpige mimba nyingine wakifka watoto watatu tu wazazi wataookea hata Laki moja.
 

dah!

Pole sana Mkuu!
 
Ushaambiwa hao watu hawana huruma na huyo mjukuu wao.
Jamaa akizingua wanamdedisha ili binti yao aolewe.

Sasa we endelea kumpa ushujaa uchwara.
Jamaa ni mbinafsi.
Hivi vitisho vya kipuuzi sana, sasa wamuue mtoto kwa sababu ya wao kutaka pesa nyingi?
Kwani kuoana ni miradi mpaka ihusishe mauaji?
Kama ndivyo walivyo inaniongezea sababu ya kuwakataa tena na kutojenga undugu na watu wa aina hii!
 
Huo sio Uanaume Kiongozi huwezi kumhukumu mpenz wako kwa tabia za Baba ake..Be a gentleman
Nakuelewa sana, lakini ndoa ni zaidi ya mke na mume! Ukiwa na wakwe wenye hulka za kishari shari utajikuta umejitwisha gunia la misumari
 
Vitisho vya kuua na kujivunia uchawi ni ujinga uliopitiliza, mkiua nyie mnaishi milele? Au pumzi yangu mnapeea nyie?

Acheni tabia za kishenzi bhana, yaani mnaanzisha ugomvi makusudi ili mupate mwanya wa kuroga? Haya rogeni sasa nipo hapa!
 
Kwa upande wangu mimi naona wewe ndio tatizo huwez kwenda kwenye mkoa mwingine bila kuja taratibu zao hasa kama waha kwa ufahamu wangu mimi na hili ni kabila langu wewe kwenda ukwen kijipatanishia mahari ya mkeo ni kosa na dharau kwa ile kwamba unaona wote ni watoto na sidhani kama kuna mkoa wenye mahari ndogo kama kigoma vijijini walikutajia mahari ili ushindwe uende ukae ujitafakari ka una wazazi uwashirikishe wewe ulivyo mpuuz na huyo mshenga wenu akajifanya anayaweza ili apate chochote tu kigoma hayo mambo ya mkaja wa mama hayana nguvu sana hata 30k wanachukua afu kwa taratibu za kiha mzazi anaozesha binti kwa mzazi mwenzie yaan ingekua ndio wameenda wazazi wa kiume wa upande wako baba zako wakubwa kwa wadogo au mababu hata kaka zako wakubwa na baadhi ya viongozi wa iman yako ya dini kwa upande wako na uko unakoenda kuoa huko ukwen kwako ndio wangewaandaa afu na uyo mshenga hakua sawa hawezi kukuambia kwamba ukimuacho mtoto atakufa anakujengea nini akilini mwako kwa unaenda kuoa familia ya wachawi wakat uyo mwanamke wako hujawahi kuyaona umuamini mshenga kwa maneno yake wakat umekaa na binti yao muda kama ni washirikina ungeaanza kuona kwa binti yao
Ndugu umri wako ila kwa jambo kubwa kama hilo la kutaka achana na fikra za ujana na huu mji wetu wa dar fanya maamuzi ya kiutu uzima hata kama wewe unapesa huwezi kujiozesha wape pesa wazazi wako waende wakatoe mahari we baki dar utapewa taarifa wakisha kamilisha kama ukiwa na baada ya muda kama miezi kadhaa nenda kaombe msamaha kwa baba mkwe wako ulimuabisha sana kwenye jamii yake hata huo mkaja wa lak 5 walikutajia ili ushindwe ujiongeze ili mlivyokua wote mapumba mkasema huku ni mbali acha tukomae liishe hatuwez kurudi kumbe ndo mnaharibu kabisaa hakuna mshenga aliewahi kupatanisha mali kama watoto mmeridhiana ikashindikana we bint kaishakuambia milioni na ndo kawambia wazazi wake waje wakuambie m5 tena kigoma vijijini mkashindwa kushtuka kwamba kuna kitu tumekosea
 
Aiseew wachangiaji ni wengi na comments zao interesting,ila kwa upande wangu mie nisingeacha mke kisa baba yake kazingua abadan asilan.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…