Tetesi: Nimetonywa, kuwa anayefuata nyayo za Hayati analiwa kichwa kwa alichokifanya Longido

Tetesi: Nimetonywa, kuwa anayefuata nyayo za Hayati analiwa kichwa kwa alichokifanya Longido

Hakuna hekima kwenye ujinga.

Mtu mjinga unapasuka nae jumla jumla.

Hekima kanisani huko na kwenye jumuia za mtakatifu petro.
Ukiidharau silaha hizi muhimu (hekima & busara) katika maisha ya kawaida na ya kila siku na hususani ukiwa kiongozi wa watu, basi hufiki popote hata uwe mjanja kiasi gani.

Kinyume cha "hekima" ni "ujinga". Unaikataa hekima, basi wewe ndiye hasaaaa mjinga...

Baba yenu Magufuli yuko wapi? Kama unafikiri ni "mapenzi ya Mungu", umechanganyikiwa, huna akili ya kupambana mambo.

Huyo alijiua mwenyewe kwa ujinga wake. Huyu naye atafuata nyayo za baba yake kwa kufa kifo cha kijinga tu kabla ya wakati wake.
 
Ukiidharau silaha hizi muhimu (hekima & busara) katika maisha ya kawaida na ya kila siku na hususani ukiwa kiongozi wa watu, basi hufiki popote hata uwe mjanja kiasi gani.

Kinyume cha "hekima" ni "ujinga". Unaikataa hekima, basi wewe ndiye hasaaaa mjinga...

Baba yenu Magufuli yuko wapi? Kama unafikiri ni "mapenzi ya Mungu", umechanganyukiwa. Huyo alijiua mwenyewe kwa ujinga wake..
Wewe umefika wapi zaidi ya kutetea majizi na upumbafu?
 
Screenshot_20240524_234216_WhatsApp.jpg
 
Kabla ya kuambiwa utumbo huyo dada alikuwa anajibu kwa dharau ndio yakamkuta makubwa. Sijui nini kilimfanya huyo dada ajiamini kutoa majibu kwa nyodo kiasi kile, on the spot akapewa shombo za uso bila chenga. Kwa kusilibwa vile na makonda haileweki makonda naye anajiamini nini kumtolea maneno ya shombo dada yule, ina maana hataki ukuu wa mkoa, anataka kurudi benchi?
 
You can easily tell she was lying.
Unajua inabidi tufike mahali watanzania tuondokane na hii tabia ya ubabaishaji. Ingawa ni kweli hicho kichombezo cha 'kuongea na mchumba wako' siyo appropriate, lakini kwa kusikiliza tu maelezo ya mhojiwa unaona kabisa alikuwa anatafuta njia ya kudanganya ili kuficha uzembe wa kutokamilisha kazi kwa muda! Hiyo ndiyo imekuwa culture yetu watanzania; uzembe, uongo, uvivu, ubabaishaji, ufisadi, nk. Tusipofika mahali tukabadilika, kamwe tusahau kuhusu kuleta mabadiliko ktk jamii na taifa letu.
 
Binasfi nimesikitika mno!
Kwa nini asijifunze hata kwa biteko!
Safari yake naamini kabisa sio ndefu upande wa siasa na uongozi.
Biteko ndio wa kutolea mfano? Nini ameachivu biteko toka awe waziri, tofautisha hulka ya mtu anayefaa kuongoza kanisani au msikitini na kiongozi anayefaa kuongoza jamii inayolia kwa wizi na ukandamizaji..kuna tabia mbaya kabisa inaendelea kuota mizizi ya kuteua na kuwapa madaraka watu wasio na uwezo wa kuamua..kwa sifa eti ni wanyenyekevu..ujinga usio kifani! Lengo hasa ni kutopenda watu independent kwenye maamuzi, tukiwaacha hawa wajinga waliolewa madaraka, kuendelea kuteua watu aina ya biteko, bashungwa, ndumbaro mongella, mchengerwa...nchi hii itaishia kuwa watumwa wa mataifa mengine..!
Makonda alishasema yuko tayari kuwa mkuu wa mkoa wa hata siku moja then akaondolewa..lkn tu amefanya kile anasikia amani kufanya kutoka Moyoni..hakuna haja ya kuongea kike kike, alishasema yuko tayari wakati wowote kwa lolote, hizo kelele za kusema km mnamtisha ni punguani wa akili tu ndie anaweza kudhani Makonda ataumia akiondolewa hicho cheo..
 
Serious gani wewe, majitu majizi na mazembe lazima yacharazwe viboko.

Hapo makonda aendelee kushikilia gia na kuwapelekea moto mpaka washike adabu.

Mmezoea uvivu na kudekezwa.
Kwa hizi akili zako hustahili hata kuwa mwenyekiti wa mtaa.
Umewahi kumuona namna Mh.Kassim Majaliwa anavyowajibisha watumishi wazembe!?
Huwa anawawajibisha kihekima na kihaki sio kwa kauli za kipuuzi na kitoto kama Makonda.
Huna hekima wewe hufai kuwa kiongozi.
 
Wekeni uzi huu kwenye kumbukumbu zenu, mrithi wa hulka za marehemu amekalia kuti kavu.

Aliyemteua hajaitazama mara mbili clip ya udhalilishaji aliofanyiwa yule mtumishi wa kike wa Longido. Amekwazika sana.

Amehurumiwa mara nyingi sana ktk kauli zake, lkn Not This Time.
Moderator rekebisheni heading hapo pasomke NImetonywa


Kwa hiyo Zuhura leo usiku au kesho atarusha barua ya utenguzi na uteuzi mpya hewani?
 
Dada wa watu kajibu kistaarabu kabisa..... Konda boy akawa anamuingilia kabla hajamaliza ili tu amchanganye..
Hakuna binadamu mwenye utu anaeweza kuangalia hii clip hadi mwisho.
Lazima tu hisia za huruma na utu zitamsukuma ku skip.
Haya sasa hawa ndio mama aliwaambia kuwa wanajua anachokitaka.
 
Back
Top Bottom