Nimetukaniwa Mzazi wangu kwa SMS, Naombeni Muongozo!

Mfuate ukamwambie hupendi hiyo tabia yake. . . . . . . .umbali kitu gani kwa heshima ya mzazi wako kama kweli umeamua kuwatunzia heshima??!!!
 

Na hii itategemea na mambo matatu pia... Mwenye matusi ana mahela kumzidi aliyetukanwa.... atachemka

Mwenye mitusi kama ni mtoto wa mujini aka pedeshee kumzidi aliyetukanwa.... atachemka

Mwenye mitusi akiamua pia kukaa kimya baada ya mitusi... kama mgomvi ni aliyetukanwa... atachemka (kama tayari kishaanza kuchemka kwa kuja kulialia hapa wakati labda jamaa huko halina hata habari)
 
Raha ya watu wa aina hiyo ni kumu ignore.Mie huwa ukinitusi naumia nakuacha.
Na matusi huwa hayana ukweli BALI ni mtukanaji anaufurahisha moyo wake.
Ukiyaweka moyoni unampa credits
 


Wazazi wengine wanastahili Mitusi!

 

Sasa ikiwa hivi ndo inabidi ukubali unyonge tuu.. kama una asili ya kabila la wanyukololo unajimaliza mwenyewe basi..
 
Ahsanteni wakuu, kwa mawazo, maoni na ushauri wenu!

Angalau nimefahamu kwanini nchi yetu ipo hivi (kutokana na maoni yenu). Acha nikapumzike sasa!
 
Anyway ninavyojua mtu mpaka amporomoshee mtu mwingine matusi ya nguoni huyo anayetukanwa anakuwa kafanya jambo fulani baya mno.Pamoja na kuwa hutaki kusema kwa nini kakuporomoshea matusi mazito siri unaijua wewe.
Hujawahi kutana na waporomoshaji matusi wa JF.....
Kuna watu kutukana kwao ni kama kunywa maji.
 

Nakushauri USAMEHE Mkuu! Ili kumpalia mkaa!
 
Ahsanteni wakuu, kwa mawazo, maoni na ushauri wenu!

Angalau nimefahamu kwanini nchi yetu ipo hivi (kutokana na maoni yenu). Acha nikapumzike sasa!

Kapumzike mkuu. Hata sisi tumefurahi kujua kwanini nchi yetu iko hivi (kutokana na thread yako)
 
Si amelianzisha...... usimkopeshe.... mpe maneno yake kama alivyokuambia ili kesho asirudie
 
Watoto wasome msg kwenye simu yako ,wewe wa wapi wewe .Bora ukae huko huko kijijini
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…