Nimevamiwa na kuibiwa mali zangu na wezi, nawezaje kuwakomesha?

Kuna mafundi wa kazi hiyo! Pengine watajitokeza humu lakini usiwalipe mpaka hapo watakapomaliza kazı!
Kungekuwa na mafundi basi tungekuwa tunaona matokeo. Mbona mafundi wa magari wapo na kila siku tunaona magari mabovu yakitengemaa?
 
Najua unataka watu wakufurahishe kwa kukuambia ''nenda kwa mganga'' ili tu kitu ambacho umekwisha kiwaza kiungwe mkono. Warning: Utapote fedha na mali zaidi.
asante kwa ushauri, nimeupokea
 
Waliokuibia wamejiibia wao wenyewe , hivyo usiende kwa mganga bali mshukuru MUNGU kwa kila kitu.
 
Ungeacha simu yeyote smart ya bei rahisi nyumbani, tena sebuleni uwe unaiweka kwenye charger.
Kwa Tanzania utaweza kumpata mmojawapo.
 
Ungeacha simu yeyote smart ya bei rahisi nyumbani, tena sebuleni uwe unaiweka kwenye charger.
Kwa Tanzania utaweza kumpata mmojawapo.
Bado sijaelewa vizuri mkuu, kwamba ningeiacha smartphone moja nyumbani ndyo ingekuwaje au ingesaidia nini?
 
Nenda karipoti Polisi , ndio kazi yao , wanaweza kukusaidia ukapata vitu vyako na wahusika kupelekwa mahakamani ili wahukumiwe Kwa mujibu wa sheria
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…