Nimeziba jino zaidi ya mwezi nyuma, sasa hivi nikitafuna kama lina ganzi, nikibonyeza juu ya shavu kuna maumivu kwa mbali nayasikia, nini tatizo?


Ahsante mkuu. Nitaitafuta
 
Hiyo inaitwa dabur red.

Dawa yenyewe kama ina rangi nyekundu flani dawa kama pilipili,ndo dawa yangi saivi baada ya kuachana na sensodyne.

Mkuu iko vizuri hiyo dawa? Je inatibu meno yanayouma?
 
Yani umebambikia uzi mkuu[emoji2][emoji2][emoji2].

Mkuu wake zetu wahanga wa meno nao.

Meno yake yametoboka au ?

Jino moja gengo ndo limetoboka katikati limeweka kama shimo, na mengine yanauma mno.
 
Jamani wacheni kuhangaisha meno,

Niko na dawa ya kienyeji uhakika 98% isipofanya kazi pesa inarudishwa
Unaifuata ofisini kabisa.
 
Kama ana mimba jitahidi amuone mganga wa meno. Kipindi cha uja uzito mtoto anachangia calcium na mama na inapelekea meno ya mama kukosa u imara. Anywe maziwa fresh na dagaa kupata calcium ya ziada.

Hapana sio mjamzito
 
Mkuu nisaidie for free then hela itafata.
Nitaongea na muhusika Ni Dr mmoja hivi akikubali ni sawa.

Ila binadamu hamuaminiki tena, bora hiyo nachukua dhamana mtu anakuwa anajua pa kukutana.
 
Bora toa bure kwanza

Dawa ya jino lilotoboka eidha ang'oe ama azibe baas
Siyo zangu, ni kazi ya Dr mmoja hivi nimetumia nikiwa nategemea kung"oa jino la pili hivi Nikapona na sisikii chochote.

Ndo maana nikarecomend,

Yeye binafsi ni biashara yake ameifanyia research na majaribio hawezi toa bure,

Ila siyo bei kubwa kulinganisha na matokeo.
 
Inatibu vipi meno yaliyotoboka?
 
Majibu ya jino ni mengi kuliko maswali yenyewe..
Binafsi nina meno 9 yaliyokwisha pandikizwa na yaliyobaki yote yako kama spare tu mdomoni
1. Kutoa jino ni bora zaidi kuliko njia yoyote ile utakayoshauriwa
2. Kuziba zino ni sawa lakini kwa tza ni kama mchezo kuigiza miezi 6 ni mingi nilikwisha rudi katika khari ile ya awali tofauti na wenzetu niliziba jino sasa ni mwaka wa 10 bado niko nalo..
3. Kakata mizizi ya jino,hii njia hiko sawa lakini ni gharama na maumivu yake ni makali sana na sio hospital wanaweza kufanya hii huduma..
4. Kupandikiza jino hii njia ni ni maumivu makali jino la asili linasuguliwa hadi inabaki kijino kidogo kisha wanaweka jino fake juu ya jino la asili..hapa pia maumivu ni makali sana na inadumu kwa mda mchache sijajua mpaka sasa mda gani maana mpaka sasa niko nalo
5. Mwisho jaribu kutumia dawa za asili kama karafuu na dawa za miti shamba wengi ni waogo nimetapeliwa pesa nyingi kwa sababu ya meno.
6. Jaribu kutumia Sensondayne kupiga msawaki kila mara na hiwe sehemu ya maisha yako ..na ile dawa usiwe unaitema unabaki nayo kinywani mwako mpaka inakauka.
7. Achana kutumia dawa za meno za whitedend,colgate na nyingine zote ni feki hakuna kitu hapo..Colgate walikuwa wazuri zamani sasa hivi copy ndio nyingi madukani kwetu

MWISHO:
Kama meno yako bado yako mengi bora kuliondoa utasikia maumivu mwanzoni lakini baada ya hapo utasahau nakisha endelea kutumia sensodyane utasahau matatizo ya meno
 
Si unapigwa ganzi mzee.

Au wewe hukuoigwa ganzi ?
Mkuu kuna ile pressure wakati koleo likiwa linasogezwa sogezwa ili jino lilegee liweze kuvutwa , japo hautasikia maumivu ila ile pressure pamoja na sauti ya mifupa ya fuvu iliyoshika jino iliwa inaachana na jino lenyewe ni adhabu tosha.

Miezi mitano nyuma nilienda kungo'a gego la pili la juu upande wa kulia lilikuwa halifai kuziba.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…