Nimfanyaje huyu house girl wangu

Nimfanyaje huyu house girl wangu

Ukiskija ujinga na ubwege ndio huo ulkioufanya! sasa angalia eti unasingizia pombe na angekubali uka-mduu ungesingizia nini. wewe sema ulikuwa tayari uko na matamanio yako juu ya huyo binti. sasa best out of all girls mtaani wewe unajitosa kwa Hg. huko ni kumdhalilisha mkeo mtu wangu. sasa ona anakudharau wewe na hata mkeo nae anadharaulika kwa kitendo ulichotaka kukifanya..... shamefull behaviour. Piga kote ila usijaribu kudu na Hg wako utaharibu familia yako pasipo na sababu za msingi. sasa cha muhimu ongeza mapenzi kwa mkeo na wala usihangaike na huyo binti wa kazi. kwanza wewe hutakiwi kabisa kuwa karibu na house girl. usifuate ushauri wa hao wazinzi wenzako (nisamehe kwa kutumia lugha kali)
 
Hapo hakuna kuombaq ushauri utavuna ulichopanda , na lazima atamwabia mkeo, inaonyesha akili yako ni kidogo sana hukustaili kupost humu aibu hii
 
Wandugu kwema?
Jamani mimi ni mdau wa humu siku nyingi sana ila nimekutwa na makubwa mwenzenu.

Siku tatu zilizopita mke wangu alikuwa amelala hospitali akimuuguza ndugu yake. Baada ya mimi kuwa huru basi nakaamua kutandika maji ile kisawasawa. Nilirudi majira ya saa tisa usiku nikiwa niko bati. Nilivyofika nyumbani dada akanifungulia mlango. Akili yangu ikanituma nimuombe dada penzi. Yule dada akawa mkali sana, nikajaribu kumlazimisha kwa kumshika akaning'ata mkono na kukimbilia chumbani kwake.

Basi nikaogopa watoto wasije wakaamka kwani walikuwa wamelala na bibi yao yaani mama yangu. Huyu dada sasa hivi namwona aibu na ninaogopa asije akamwambia wife. Shida ninayoipata nikamsalimia haitiki, nikimtuma kitu hafanyi kwa kweli ananidharau sana. Pia inabidi niwe karibu na wife mda wote kwani naogopa asije akamwambia.

Nimeomba ushauri kwa baadhi ya marafiki wengine wananiambia nikitaka niwe salama eti nihakikishe natembea nae na wengine wananiambia nimshawishi mama tumfukuze kazi.

CHONDE CHONDE ULEVI NOMA! Hivi ulimpa mkataba wa ajira?, unampelekea NSSF? Na je likizo anaenda kila mwaka siku 28? na je umri wake ni miaka mingapi? kama ni below 15 unamwendeleza kielimu na kwamba unampa haki zote za kucheza kama watoto wengine?
Ukinipa majibu nitafurahi na nita kupa ushauri wangu, basically ulevi usifagilie ndg yangu. Eti ukarudi home ukiwa 'bati' kunasiku utarudi ukiwa 'chuma' shauri yako!
 
Basi nikaogopa watoto wasije wakaamka kwani walikuwa wamelala na bibi yao yaani mama yangu..

Unaniangusha mdogo wangu, yaani umelewa kiasi cha kushindwa kujua unachofanya lakini ukabakiza akili kidogo za kuogopa kuwaaamsha watoto na mama yako, hii kwa lojiki inakataa kabisa.
 
Kwa nini usingechukua baa meidi huko ulikotoka ama wale machangu wa kununua? mambo mengine mnayaendekeza wenyewe.
 
Tafuta muda uongee na huyo hg wako na kumuomba msamaha, umwambie pombe ndio ilisababisha! Ukifanya hivyo utakuwa na amani!
 
Unaniangusha mdogo wangu, yaani umelewa kiasi cha kushindwa kujua unachofanya lakini ukabakiza akili kidogo za kuogopa kuwaaamsha watoto na mama yako, hii kwa lojiki inakataa kabisa.
Kumbe ni mdogo wako, mmefanana kila kitu....lol!
 
Tatizo lako ni ubosi kidogo ndio unataka kumaliza yote. Sasa kama angekubali ungetuomba ushauri au? Tabia hiyo sio nzuri kabisa kaa, umueleweshe huyo bint kuwa ilikuwa pombe tu na umuombe msamaha. Unaweza kumfukuza kwa kisa kingine ila kwa hili utakuwa umemuonea.
 
.....Pia inabidi niwe karibu na wife mda wote kwani naogopa asije akamwambia.

Nimeomba ushauri kwa baadhi ya marafiki wengine wananiambia nikitaka niwe salama eti nihakikishe natembea nae na wengine wananiambia nimshawishi mama tumfukuze kazi.





ndugu yangu wala usihangaike kukaa karibu na mkeo, kwani kama kumwambia anaweza kumwambia muda wowote kwa njia yoyote mfano anaweza kumwambia wakiwa jikoni, ama kwa sms nk.

lakini pia hakuna haja ya kuendelea kuwa na wazo la kutembea naye, maana keshaonesha kuwa anamsimamo na kuwa aproachi yako ilikuwa ya kilevikilevi mno na ndo maana alibumburuka, pia hakuna haja ya kumtemesha ngese (yaani kumwachisha kazi) kwani haitasaidia, zaidi zaidi utazidi kuyakoroga mambo na kuyaharibu zaidi..
 
Wandugu kwema?
Jamani mimi ni mdau wa humu siku nyingi sana ila nimekutwa na makubwa mwenzenu.

Siku tatu zilizopita mke wangu alikuwa amelala hospitali akimuuguza ndugu yake. Baada ya mimi kuwa huru basi nakaamua kutandika maji ile kisawasawa. Nilirudi majira ya saa tisa usiku nikiwa niko bati. Nilivyofika nyumbani dada akanifungulia mlango. Akili yangu ikanituma nimuombe dada penzi. Yule dada akawa mkali sana, nikajaribu kumlazimisha kwa kumshika akaning'ata mkono na kukimbilia chumbani kwake.

Basi nikaogopa watoto wasije wakaamka kwani walikuwa wamelala na bibi yao yaani mama yangu. Huyu dada sasa hivi namwona aibu na ninaogopa asije akamwambia wife. Shida ninayoipata nikamsalimia haitiki, nikimtuma kitu hafanyi kwa kweli ananidharau sana. Pia inabidi niwe karibu na wife mda wote kwani naogopa asije akamwambia.

Nimeomba ushauri kwa baadhi ya marafiki wengine wananiambia nikitaka niwe salama eti nihakikishe natembea nae na wengine wananiambia nimshawishi mama tumfukuze kazi.

Ndugu Nduka naona kama maelezo yako yanajikanganya vile. Kwa uzoefu wangu mtu aliyetandika maji kisawasawa hawezi kuwa na kumbukumbu nzuri kiasi hicho na pia hawezi kureason kama ulivyofanya. Inaonekana unakumbuka kila kitu tangu ulipofanya maamuzi ya kunywa, pombe, umuda ulioondoka bar na hali uliyokuwa nayo wakati unaondoka, muda uliofika nyumbani na mambo yaliyoendelea.

Mtu aliyelewa kisawasawa huwa akifanikiwa kufika maeneo ya nyumbani analala nje ya mlango kwani hata akili ya kubisha hodi huwa haipo au sebuleni kwenye kochi kwani nguvu ya kufika chumbani huwa imeisha. Wengine huishia kulala bar hukohuko. Na ukimuuliza kesho yake alifikaje na kulala pale mlangoni au kwenye kochi huwa hawezi kukumbuka details za jinsi alivyosafiri toka bar mpaka mlangoni kwake. Wengine hupata majeraha na huwa hawawezi kabisa kukumbuka waliyapataje au huibiwa pesa/simu wasijue labda wasaidiwe na walioshuhudia.

Kwa ufupi ni kuwa haukuwa umelewa kiasi cha kutokutambua mambo na hivyo sababu kuwa ulevi ndio uliokusukuma haina mashiko. Inaonekana ulishamtamani binti muda mrefu kabla ya tukio ila ulikuwa unatafuta tu wakati muafaka. Na ninahisi kuwa hata hizo pombe unazozisingizia ulikunywa ukiwa na malengo ya kumtokea binti mara utakaporudi kwani fursa ndiyo ilikwisha tokea.

Kuhusu suala la nini ufanye sijui unaishije na housegirl nyumbani kwako lakini cha muhimu ni ku "keep distance" na kuainisha mipaka ya mahusiano yako na huyo binti. Inawezekana kabisa kuwa binti keshamwambia mke wako na sasa hivi huyo mama anakufuatilia kwa karibu bila kukuonesha kuwa ameshafahamu. Hivyo hata ile tabia ya binti ya kugoma kukusalimu na kutelekeza maelekezo yako inaweza kuwa ni viashiria tu kwa huyo mwana mama.
 
Mshahara wa dhambi ni mauti tena mauti ya milele, kwa maneno mengine wanaseme nipotezeee.
 
Back
Top Bottom