NIMR ni kimeo, haina faida kwa nchi, ifutwe tu

NIMR ni kimeo, haina faida kwa nchi, ifutwe tu

Ralph Tyler

JF-Expert Member
Joined
Jul 31, 2015
Posts
2,828
Reaction score
3,579
1. Miaka yote zaidi ya 40 ya uwepo wa NIMR, wameongeza nini katika ufahamu wa mambo ya tiba Tanzania? Ni utafiti gani waliowahi kuufanya ukaleta tija katika kupunguza au kuondoa tatizo lolote la kiafya? Jibu ni zero.

2. Hivi kuna dawa yoyote sokoni (dawa ya maana yenye viwango stahiki, na siyo ile michanganyiko ya pilipili kichaa na tangawizi waliyoiga kutoka kwa waganga wa kienyeji) au vifaatiba hospitalini au maarifa mapya yoyote ya tiba yaliyowahi kugunduliwa na NIMR? Jibu ni hakuna.

3. Nina jamaa zangu nimesoma nao History na English pale Mlimani, eti nao wanafanya kazi NIMR wananiambia wanaitwa "Research Scientist". Hiki ni kituko! Scientist wa history, English, Kiswahili, sociology na Political Science anafanya nini kwenye MEDICAL research? Ingekuwa HEALTH research ningewaelewa kwa kuwa afya ni suala mtambuka lenye mambo ya kisiasa, kiuchumi na kijamii yanayoathiri afya, lakini medical research ni mambo ya maabara, madawa, mawodini huko wanakotibiwa wagonjwa, operations mpya mpya kama hizi za moyo na figo nk. Tunasikia huko Jakaya Kikwete institute, Benjamin Mkapa Hospital na hata MOI wakifanya innovations mpya mpya, lakini mchango wa NIMR kwenye hizi innovations uko wapi?

4. Mkurugenzi wa NIMR ni profesa wa Marine Biology. Hii ndiyo medical research? Hakuna medical researcher nchi hii mwenye sifa ya kuwa mkurugenzi wa NIMR? Sasa marine biologist na medical research wapi na wapi? Ndio chanzo cha kwenda kudesa michanganyiko ya waganga wa kienyeji na kutuambia ni dawa za korona!

5. Kwa ujumla NIMR ni kimeo, haina faida kwa nchi, ifutwe tu.
 
Samhani nndugu Ralph Tyler kwa faida yangu na wengine NIMR kirefu chake nini?
anniversary-website-1024x134.png
 
Hiyo number 3. Usipuuze mkuu, wanaweza kuwa kitengo maalum tiss, hawa jamaa kila mahali wanaingia hata kama wamesomea linguistic!
Hiyo number 3. Usipuuze mkuu, wanaweza kuwa kitengo maalum tiss, hawa jamaa kila mahali wanaingia hata kama wamesomea linguistic!
Sasa kama ni hivyo wajitafutie jina muafaka, wawaache mabingwa wa tiba waendelee kufanya medical research huko mahospitalini.
NIMR limekuwa chaka la kufuja fedha za umma kwa research za kudesa zisizo na tija.
 
Nakubaliana na wewe mkuu100%.Niliwahi kusema humu siku moja .kuna taasisi za serikali sizionagi kazi ya kim kakati.Mfano,naona hata taasis za elimu ya juu ni kama tuition centres tuu. Sionagi ile segment ya research inafanyaga nini hasa.

Hebu tuangalie Muhimbili, SUA, UDSM. haya ni mataasisi makubwa lakini sijawahi kusikia wamefanya utafiti wa kutatua changamoto zilizopo. Na wenyewe wameingia katika mtego wa kuazimia kuongeza mapato yatokanayo na karo,ila siyo kushughulikia tafiti ya kutafuta majibu ya changamoto.Angalia watu wanaoitwa Taasisi ya lishe Tanzania.

Sioni wanafanya nini hasa.Taasis zote zimewachia wanasiasa wanatuchanganya na milishe ambayo haijahata hata patiwa approval na TMDA.

Yaani kipindi hiki tunalishwa kila kitu kwa kweli.Nimeona hata UDSM nao walikuja na mchanganyiko wa tiba mbadala.Sasa sayansi waliyosomea imepotelea wapi.ni kweli kwamba wote walisomea tiba mbadala.Kuna Taasisi inaitwa Ifakara Health Institute ,kidogo sana hii imejaribu jaribu kwenye malaria,lakini nayo imejifia yenyewe.

WANASANSI WETU MKO WAPI? MMEISHIA KUTUTISHA KUHUSU CHANJO YA CORONA ILA HAMJABAINISHA KAMA NI KWELI MLIFANYIA UTAFITI HIYO CHANJO AU NA NYINYI MNASIKILIZA HABARI ZA MITANDAONI KAMA SIYE WA HUKU NANJILINJI MTWARA VIJIJINI
 
... ni kakichaka ka maprofesa kupiga hela za tafiti zisizo na matokeo.
Exactly. Nimeona mahojiano kwenye TV na mkurugenzi mmojawapo (siyo mkurugenzi mkuu Prof Mgaya), akasema wanafanya research kwa kutegemea grants ambazo watoaji wa grants hizo ambao ni mataifa ya nje ndio wanaoamua research agenda. Kwa hiyo tuna taasisi ya utafiti wa tiba (ndiyo tafsiri ya institute of medical research, ingawa wenyewe wanaita taasisi ya utafiti wa magonjwa ya binadamu) ambayo haina uwezo wa kuendesha research agenda zake. Matokeo yake imejaza "scientists" wasiokuwa wa tiba kwenye ranks zake: sociologists, politicians, linguists, historians, marine biologists na wengine wa hivyo, eti hawa ndiyo waendeshe agenda za medical research! Hii siyo dharau?

Ndiyo maana tafiti zake ni kichefuchefu kitupu, hata sisi tuliosoma "ungwini" tunawashangaa.
 
Mnaweza kuiga kwetu mangwini kama mnavyotuita. Katika Taasisi ya Taaluma za Kiswahili pale Mlimani, kuna wataalamu wa lugha tu, hatuna biologists, sociologists na vitu vingine vya aina hiyo. Hata TAWIRI ile ya wanyamapori inaongozwa na wataalam wa wanyama pori. Pia kuna TARI ya kilimo, ina wataalamu wa kilimo kila siku tunasikia tafiti zao za mbegu bora na kwenye maonesho ya kilimo nanenane tunaziona.
Hao medical research ndio wamedharauliwa au wamejidharau?
 
Nakubaliana na wewe mkuu100%.Niliwahi kusema humu siku moja .kuna taasisi za serikali sizionagi kazi ya kim kakati.Mfano,naona hata taasis za elimu ya juu ni kama tuition centres tuu. sionagi ile segment ya research inafanyaga nini hasa.Hebu tuangalie Muhimbili,SUA,UDSM. haya ni mataasis makubwa lakini sijawahi kusikia wamefanya utafiti wa kutatua changamoto zilizopo.Na wenyewe wameingia katika mtego wa kuazimia kuongeza mapato yatokanayo na karo,ila siyo kushughulikia tafiti ya kutafuta majibu ya changamoto.Angalia watu wanaoitwa Taasisi ya lishe Tanzania.sioni wanafanya nini hasa.Taasis zote zimewachia wanasiasa wanatuchanganya na milishe ambayo haijahata hata patiwa approval na TMDA.

Yaani kipindi hiki tunalishwa kila kitu kwa kweli.Nimeona hata UDSM nao walikuja na mchanganyiko wa tiba mbadala.Sasa sayansi waliyosomea imepotelea wapi.ni kweli kwamba wote walisomea tiba mbadala.Kuna Taasisi inaitwa Ifakara Health Institute ,kidogo sana hii imejaribu jaribu kwenye malaria,lakini nayo imejifia yenyewe.

WANASANSI WETU MKO WAPI? MMEISHIA KUTUTISHA KUHUSU CHANJO YA CORONA ILA HAMJABAINISHA KAMA NI KWELI MLIFANYIA UTAFITI HIYO CHANJO AU NA NYINYI MNASIKILIZA HABARI ZA MITANDAONI KAMA SIYE WA HUKU NANJILINJI MTWARA VIJIJINI
... afadhali kidogo taasisi za utafiti za kilimo na mifugo; angalau hawa wameweza kuja na mbegu mbadala za mazao mbalimbali - mahindi, mtama, korosho, n.k. Pia wakulima wanapata mitamba na madume bora ya ng'ombe na mbuzi wa maziwa.

Naanza kukubaliana thread moja ililetwa humu jana kwamba SUA ndio chuo kinachoongoza Tanzana kwa tafiti zake kuwa cited. Wataalamu wengi wa kilimo na mifugo nchini walipitia SUA.
 
Ni usenge mtupu ,na hapa ndo tatizo lilipo ,kama Raisi anadoubt chanjo from abroad , kule ambako wenzetu hawalali they are fighting to the bitter end kuhakikisha wanakabiliana na Korona ,...Sisi kama nchi tunafanya juhudi gani scientifically, NIMRI wako wapi ??? Wanafanya nini pale ?? Fukuza wote , they are useless, kuweka doubt kwenye chanjo ya Korona huku wewe ukiwa na zero effort hamna kitu unakifanya..... unapopinga silaha ya mwenzako inabidi na wewe uwe na silaha inayokupa jeuri au ndo ujinga wa kujifukiza na kupiga ramli , na kujificha kwenye kichaka cha Mungu anaponya , Muujiza hauji mahali pa wajibu ....Kwa style hii tutaendelea kuzika mizoga ya wazee wetu wapendwa .... Na hata JPM mwenyewe yupo kwenye extremely danger kama mtu wake wa ofisi anaenda na Korona .... Yeye usalama wake uko wapi ..na itakuwa aibu ya Karne
 
Exactly. Nimeona mahojiano kwenye TV na mkurugenzi mmojawapo (siyo mkurugenzi mkuu Prof Mgaya), akasema wanafanya research kwa kutegemea grants ambazo watoaji wa grants hizo ambao ni mataifa ya nje ndio wanaoamua research agenda. Kwa hiyo tuna taasisi ya utafiti wa tiba (ndiyo tafsiri ya institute of medical research, ingawa wenyewe wanaita taasisi ya utafiti wa magonjwa ya binadamu) ambayo haina uwezo wa kuendesha research agenda zake. Matokeo yake imejaza "scientists" wasiokuwa wa tiba kwenye ranks zake: sociologists, politicians, linguists, historians, marine biologists na wengine wa hivyo, eti hawa ndiyo waendeshe agenda za medical research! Hii siyo dharau?
Ndiyo maana tafiti zake ni kichefuchefu kitupu, hata sisi tuliosoma "ungwini" tunawashangaa.
... wanasiasa watakuambia hujuma za mabeberu hizo; wanatoa grants halafu wanaelekeza ni tafiti zipi za kufanya ili kuvuruga malengo ya NIMR. Tuko vitani; ha ha ha!
 
... afadhali kidogo taasisi za utafiti za kilimo na mifugo; angalau hawa wameweza kuja na mbegu mbadala za mazao mbalimbali - mahindi, mtama, korosho, n.k. Pia wakulima wanapata mitamba na madume bora ya ng'ombe na mbuzi wa maziwa.

Naanza kukubaliana thread moja ililetwa humu jana kwamba SUA ndio chuo kinachoongoza Tanzana kwa tafiti zake kuwa cited. Wataalamu wengi wa kilimo na mifugo nchini walipitia SUA.
Yesi ni kweli vyuo vya kati ndiyo vinavyopeform.Naliendele mtwara,TARI uyole na kwingineko.lakini ukiangalia kwa kina utakuta kuna mkono wa mabeberu kwa nyuma yake umewezesha mafanikio.
 
Mnaweza kuiga kwetu mangwini kama mnavyotuita. Katika Taasisi ya Taaluma za Kiswahili pale Mlimani, kuna wataalamu wa lugha tu, hatuna biologists, sociologists na vitu vingine vya aina hiyo. Hata TAWIRI ile ya wanyamapori inaongozwa na wataalam wa wanyama pori. Pia kuna TARI ya kilimo, ina wataalamu wa kilimo kila siku tunasikia tafiti zao za mbegu bora na kwenye maonesho ya kilimo nanenane tunaziona.
Hao medical research ndio wamedharauliwa au wamejidharau?
... wanapewa grants na mabeberu halafu wanaelekezwa maeneo ya kufanya tafiti based on beberu's interests! Tunapigana vita vikali sana, sio vya kiuchumi tu Mkuu.
 
Back
Top Bottom