NIMR ni kimeo, haina faida kwa nchi, ifutwe tu

NIMR ni kimeo, haina faida kwa nchi, ifutwe tu

Exactly. Nimeona mahojiano kwenye TV na mkurugenzi mmojawapo (siyo mkurugenzi mkuu Prof Mgaya), akasema wanafanya research kwa kutegemea grants ambazo watoaji wa grants hizo ambao ni mataifa ya nje ndio wanaoamua research agenda. Kwa hiyo tuna taasisi ya utafiti wa tiba (ndiyo tafsiri ya institute of medical research, ingawa wenyewe wanaita taasisi ya utafiti wa magonjwa ya binadamu) ambayo haina uwezo wa kuendesha research agenda zake. Matokeo yake imejaza "scientists" wasiokuwa wa tiba kwenye ranks zake: sociologists, politicians, linguists, historians, marine biologists na wengine wa hivyo, eti hawa ndiyo waendeshe agenda za medical research! Hii siyo dharau?
Ndiyo maana tafiti zake ni kichefuchefu kitupu, hata sisi tuliosoma "ungwini" tunawashangaa.
Hivi kwenye bajeti yetu umewahi kusikia walau serikali imetenga bajeti kwajili ya tafiti mbalimbali?

Kwenye wizara husika umeshawahi kusikia walau wizara kutenga bajeti kwajili ya tafiti mbali mbali zinazohusiana na wizara yenyewe ?

Kama hatuna bajeti ya tafiti hizo taasisi nitafanya tafiti kwa fungu gani?
 
Yesi ni kweli vyuo vya kati ndiyo vinavyopeform.Naliendele mtwara,TARI uyole na kwingineko. Lakini ukiangalia kwa kina utakuta kuna mkono wa mabeberu kwa nyuma yake umewezesha mafanikio.
Mbona NIMR hawafanikiwi kwa mkono huo huo wa mabeberu wakati ni PhD tupu zimejaa pale?
 
Wale jamaa hawako serious kabisa.

Ile kachumbari mtu yeyote anaweza kutengeneza badala ya kwenda kuinunua kwa hela kubwa namna ile.
Ndio maana fomula ilikuwa disclosed kuwasaidia wananchi wa kipato cha chini Mkuu! Hizi za mabeberu fomula ni top secret!
 
Ha ha ha haaaa! Mbona mnawafokea sana wakuu? I guess wenyewe wapo wanayasoma haya wajirekebishe. Kiukweli kama wamejaa sociologists kwenye taasisi ya utafiti wa madawa hapo kuna tatizo kubwa sana
ITEGAMATWI ni kijiji fulani kipo huko wilayani Urambo vipi unauhusiano wowote na kijiji husika?
 
1. Miaka yote zaidi ya 40 ya uwepo wa NIMR, wameongeza nini katika ufahamu wa mambo ya tiba Tanzania? Ni utafiti gani waliowahi kuufanya ukaleta tija katika kupunguza au kuondoa tatizo lolote la kiafya? Jibu ni zero.

2. Hivi kuna dawa yoyote sokoni (dawa ya maana yenye viwango stahiki, na siyo ile michanganyiko ya pilipili kichaa na tangawizi waliyoiga kutoka kwa waganga wa kienyeji) au vifaatiba hospitalini au maarifa mapya yoyote ya tiba yaliyowahi kugunduliwa na NIMR? Jibu ni hakuna.

3. Nina jamaa zangu nimesoma nao History na English pale Mlimani, eti nao wanafanya kazi NIMR wananiambia wanaitwa "Research Scientist". Hiki ni kituko! Scientist wa history, English, Kiswahili, sociology na Political Science anafanya nini kwenye MEDICAL research? Ingekuwa HEALTH research ningewaelewa kwa kuwa afya ni suala mtambuka lenye mambo ya kisiasa, kiuchumi na kijamii yanayoathiri afya, lakini medical research ni mambo ya maabara, madawa, mawodini huko wanakotibiwa wagonjwa, operations mpya mpya kama hizi za moyo na figo nk. Tunasikia huko Jakaya Kikwete institute, Benjamin Mkapa Hospital na hata MOI wakifanya innovations mpya mpya, lakini mchango wa NIMR kwenye hizi innovations uko wapi?

4. Mkurugenzi wa NIMR ni profesa wa Marine Biology. Hii ndiyo medical research? Hakuna medical researcher nchi hii mwenye sifa ya kuwa mkurugenzi wa NIMR? Sasa marine biologist na medical research wapi na wapi? Ndio chanzo cha kwenda kudesa michanganyiko ya waganga wa kienyeji na kutuambia ni dawa za korona!

5. Kwa ujumla NIMR ni kimeo, haina faida kwa nchi, ifutwe tu.
Mkuu kwemaaa?, una ushahidi na ubachokisema? NIMR kwa upande Wa suala ka kutokomeza malaria nchini naona kama wsmejitahidi sana,ni asilimia ndogo imebaki.
 
Hivi kwenye bajeti yetu umewahi kusikia walau serikali imetenga bajeti kwajili ya tafiti mbali mbali ?

Kwenye wizara husika umeshawahi kusikia walau wizara kutenga bajeti kwajili ya tafiti mbali mbali zinazohusiana na wizara yenyewe ?

Kama hatuna bajeti ya tafiti hizo taasisi nitafanya tafiti kwa fungu gani ?
Walishawahi kuomba bajeti wakazinguliwa ? ... Kwa tatizo lilivyo critical nilitegemea kumuona mkrugenzi akilisemea kwenye media na wao wamefanya nin na wamefikia wap na changamoto ni ipi.....wao wamelala tuu wameenda Madagascar kukopy formula ya tormato sauce na kuja kutuwekea et covidol ......kama mkrugenzi mwenyewe kasomea marine biology haishangazi kuona ukimya kama huu......ni moja ya vitengo vibovu kuwahi kutokea nchi hii
 
1. Miaka yote zaidi ya 40 ya uwepo wa NIMR, wameongeza nini katika ufahamu wa mambo ya tiba Tanzania? Ni utafiti gani waliowahi kuufanya ukaleta tija katika kupunguza au kuondoa tatizo lolote la kiafya? Jibu ni zero.

2. Hivi kuna dawa yoyote sokoni (dawa ya maana yenye viwango stahiki, na siyo ile michanganyiko ya pilipili kichaa na tangawizi waliyoiga kutoka kwa waganga wa kienyeji) au vifaatiba hospitalini au maarifa mapya yoyote ya tiba yaliyowahi kugunduliwa na NIMR? Jibu ni hakuna.

3. Nina jamaa zangu nimesoma nao History na English pale Mlimani, eti nao wanafanya kazi NIMR wananiambia wanaitwa "Research Scientist". Hiki ni kituko! Scientist wa history, English, Kiswahili, sociology na Political Science anafanya nini kwenye MEDICAL research? Ingekuwa HEALTH research ningewaelewa kwa kuwa afya ni suala mtambuka lenye mambo ya kisiasa, kiuchumi na kijamii yanayoathiri afya, lakini medical research ni mambo ya maabara, madawa, mawodini huko wanakotibiwa wagonjwa, operations mpya mpya kama hizi za moyo na figo nk. Tunasikia huko Jakaya Kikwete institute, Benjamin Mkapa Hospital na hata MOI wakifanya innovations mpya mpya, lakini mchango wa NIMR kwenye hizi innovations uko wapi?

4. Mkurugenzi wa NIMR ni profesa wa Marine Biology. Hii ndiyo medical research? Hakuna medical researcher nchi hii mwenye sifa ya kuwa mkurugenzi wa NIMR? Sasa marine biologist na medical research wapi na wapi? Ndio chanzo cha kwenda kudesa michanganyiko ya waganga wa kienyeji na kutuambia ni dawa za korona!

5. Kwa ujumla NIMR ni kimeo, haina faida kwa nchi, ifutwe tu.
Umesimuliwa ukakimbilia kuja kubandika bango humo kana kwamba una akili sana kumbe bure tu.

Kama huna uwezo wa kujua taaluma halisi za watu ni ngumu sana kwa ninyi wanasiasa uchwara kuelewa nini maana ya usalama wa nchi na raia wake. Ninaweza kuwa nataaluma yangu halisi lakini ili niweze kuingia mahali fulani ninasomea taaluma nyingine wezeshi kuingia ndicho kilichopo lakini wewe unatupigia kelele kama mtoto mdogo aliyezaliwa leo ambaye ni sharti aliye kuthibitisha ni mzima na ana afya ya kuhisi mazingira yanayomzunguka kwa muda huo sio rafiki.

Rekebisha tabia hiyo kubagaza wanataaluma. Kama ulisomea HGL, HGK, HGE nk lakini hukujiongeza kusomea vitu vingine usiwaonee nongwa wenzio.
 
Back
Top Bottom