NIMR ni kimeo, haina faida kwa nchi, ifutwe tu

NIMR ni kimeo, haina faida kwa nchi, ifutwe tu

Tatzo la NIMR ni kutokukubali kuendana na wakati yani kwenye upigaji ndo wako vizuri hasa kwenya uendeshaji wa miradi ya malaria, kichocho, na matende hapo huwa ni kula hela tu, ila kwenye tafti ni blaa blaa tu
Hizo kazi za kuendesha miradi ya malaria, kichocho na matende zingeweza kufanywa na watu wa idara mojawapo pale wizara ya afya na kwenye halmashauri zetu, siyo na taasisi ya medical research. Hizo ni public health projects, na hazihitaji kuongozwa wala kusimamiwa na medical researchers, hizo hata watu waliosomea community development na sociology ndio kazi zao kupita kwenye jamii kuhimiza matumizi ya chandarua, matumizi ya choo bora nk. Tunaona hata huku mitaani watu wanaohimiza kwamba "Usichukulie Poa Nyumba ni Choo" ni akina Mrisho Mpoto na Shilole, wasanii wenye influence kwa hadhira.
Medical Researchers hawapaswi kuvamia kazi ambazo sio medical research. Wanapaswa wafanye tafiti za tiba walete majibu ya changamoto zilizoko katika tiba ya binadamu: dawa bora, vifaa tiba, mbinu bora za operesheni na mengine ya aina hiyo katika tiba.

Sasa hawa wenzetu huko NIMR baada ya kuona medical research imewashinda ndio tunawasikia kila siku wakiimba matende na mabusha na kugawa dawa za minyoo mashuleni. Dawa hizo zilitafitiwa zamani na kuthibitishwa ubora wake huko zilikotoka kwa mabeberu, hapa kwetu zimepata usajili na kuruhusiwa kutumika, eti NIMR wako busy kugawa dawa! Hiyo kazi hata ukimpa mwalimu wa shule ya msingi ukamwambia gawia kila mtoto kidonge kimoja anywe na glasi moja ya maji atashindwa?
 
Ni usenge mtupu ,na hapa ndo tatizo lilipo ,kama Raisi anadoubt chanjo from abroad , kule ambako wenzetu hawalali they are fighting to the bitter end kuhakikisha wanakabiliana na Korona ,...Sisi kama nchi tunafanya juhudi gani scientifically, NIMRI wako wapi ??? Wanafanya nini pale ?? Fukuza wote , they are useless, kuweka doubt kwenye chanjo ya Korona huku wewe ukiwa na zero effort hamna kitu unakifanya..... unapopinga silaha ya mwenzako inabidi na wewe uwe na silaha inayokupa jeuri au ndo ujinga wa kujifukiza na kupiga ramli , na kujificha kwenye kichaka cha Mungu anaponya , Muujiza hauji mahali pa wajibu ....Kwa style hii tutaendelea kuzika mizoga ya wazee wetu wapendwa .... Na hata JPM mwenyewe yupo kwenye extremely danger kama mtu wake wa ofisi anaenda na Korona .... Yeye usalama wake uko wapi ..na itakuwa aibu ya Karne
Unamapepo wewe sio bure,
 
Hebu tuorodheshee tafiti ambazo NIMR imefanya na faida ambazo nchi imepata kwa tafiti hizo. Usilete madesa utaumbuka, watu wanayo majibu hapa.
Nimejaribu ku-search kwenye intene t nimekuta these achievements
•Contributed to efficacy data for reviewing National Antimalarial Drug Policy in mainland Tanzania (CQ to SP and SP to ALU), also for Zanzibar (CQ to AQ/AS)

•Provided data to support use of Albendazole / Ivermectin for global elimination of lymphatic filariasis and Onchocerciasis

•Pioneering data to show ITNs can reduce malaria morbidity
•Still responsible for 4 out of 8 sentinel sites for monitoring antimalarial efficacy
•Malaria vaccine trials, RTS,S /AS02 and MSP3.
•Capacity building through research activities
 
Wewe jiwe vipi? Kwani kozi zinazohusu afya ni udaktari na unesi tu? Hakuna kozi za IT mahususi kwa ajili ya afya,hujawahi kusikia kozi za business Administration katika masuala ya afya?
Haya mjibie mwenzako "anayejua vizuri Muhimbili" Unaweza kuwa msemaji wa hospitali kubwa kama Muhimbili bila kuwa na background ya masuala ya Afya?
Hilo ndilo suali la msingi huko kwingine mnarukia rukia tu.
Swali lingine, mtu wake aliyesoma mifugo atafafanya kazi kitengo gani Muhimbili?
Dogo ebu kua basi..we unadhani wanao lipa mshahara pale muhimbili ni madaktari..wanao endesha IT ni manesi..kua na akili hizi ni taasisi zinachukua watu wa taaluma mbalimbali ili kuwezesha utoaji wa huduma.

#MaendeleoHayanaChama
 
Tatzo la NIMR ni kutokukubali kuendana na wakati yani kwenye upigaji ndo wako vizuri hasa kwenya uendeshaji wa miradi ya malaria, kichocho, na matende hapo huwa ni kula hela tu, ila kwenye tafti ni blaa blaa tu
Pale hamna kitu naona wahusika wameanza kuja kujitetea na kudefend humu ....
 
Hata jeshi, polisi na TISS ni taasisi, unaweza kuwa msemaji wa hizo taasisi kama wewe sio mmoja wao?
Dogo ebu kua basi..we unadhani wanao lipa mshahara pale muhimbili ni madaktari..wanao endesha IT ni manesi..kua na akili hizi ni taasisi zinachukua watu wa taaluma mbalimbali ili kuwezesha utoaji wa huduma.

#MaendeleoHayanaChama
 
Nakumbuka mwaka flani tuliwapa NIMR pesa ili wakatafiti cases za cholera mtaani. It was more of an assessment na sio “research” as such. Professor ndio alitaka kulead hiyo assessment

Hii ndio NIMR yetu.
Pole sana mtaalam. Ni kimeo hiyo kitu inayoitwa NIMR.
Kama nchi tunahitaji kutafakari tena kama tunahitaji NIMR au la. Kama kweli tunahitaji taasisi inayofanya medical research, NIMR kwa hakika haifanyi kazi hiyo. Inahitaji kufanyiwa marekebisho makubwa sana ya kimuundo ili iweze kuendana na dhima ya medical research.
Vinginevyo kwa kuwa medical research zinazofanyika Muhimbili, Bugando, Benjamin Mkapa, MOI na kwingineko zinatufaa na matokeo yake yanaonekana, basi tuimarishe tafiti katika taasisi hizo tuachane na kimeo cha NIMR.
 
NIMR wanafanya kazi nzuri ila kwasababu vitu wanavyofanya siyo vya level yako ya intelligence unahisi hawafanyi kitu. Research inasaidia kusuluhisha matatizo na kuleta ugunduzi. Hapa issue ni visibility, wanapaswa kuuambia umma mafanikio yao. Nina question uwezo wako wa akili,huwezi kushawishi taasisi ya utafiti ifutwe, kama ni performance wawekewe malengo na wayatimize. Unashawishi taasisi ya utafiti ifutwe ili tuanzishe taasisi ya kukuza utamaduni na kulinda historia? Leo kwa mara ya kwanza nimesoma upumbavu mwingi sana ukiwa sehemu moja.
Labda tukuulize wewe ipi kazi nzuri imefanywa na NIMR ? Mtoa mada ametoa data za kutosha kuonyesha NIMR ni wastage of money ..... Wewe unaita ameandika upumbavu ...basi thibitisha upumbavu wake la sivyo ukishindwa wewe ndo kilaza wa kiwango cha Tarmac road..et intelligence, intelligence gani hyo taasis nying duniani za tafiti tiba zina outbreak news namna zinavyokabiliana na Korona kutafta chanjo , NIMRI wako kimya et intelligence ..huu ujinga sjui unatokea wap hii nchi
 
Wapi nimesema kwamba wote wanoafanya kazi Muhimbili lazima wawe wamesoma medical?! Huna hoja kilichobaki unalazimisha kusema kitu ambacho huwezi kukithibitisha.
Nimekuuliza msemaji wa hospitali nyeti kama ya Muhimbili inawezekanaje akawa mtu asiye na background kwenye masuala ya AFYA!
Mpaka sasa hujajibu umebaki kuruka ruka tu kama maharage yanayochemshwa kwenye sufuria na madai ya kishamba kwamba unaijua Muhimbili yote na TISS wote.Jibu hoja zangu, acha kutishia nyau watu wazima.
Wewe unachosha sana unakiwango kidogo.sana. cha ufikiri sina haja kupoteza energy kubishana na layman, umeeleza.mwenyewe hapo juu kuwa muhimbili kuna watu wenye fani mbalimbali kuanzia IT, Uhasibu nk. Sasa kwa ufahami wako mdogo unadhani wote hao wamesomea medical?! Kuna mpaka madereva kibao kule ndani hawana background yoyote ya medical acha ubishi wakishamba bwana mdogo, sina muda wa kubishana kishamba, wewe muhimbili unapasikia tu radioni , Mimi nimeingia pale nikiwa kama sehemu ya mradi Fulani kwa miaka zaidi ya mitano, so huwezi kunifundisha kitu, huna ujualo, jifunze kukubali kujifunza,na hao tiss unaowasikia kwa watu sisi tuko nao huku na wengine ndugu zetu tunaelewa utendaji wao, hatuadithiwi kama wewe, kuanzia wanaokaa pale kota za nyuma ya ikulu, mpaka kule kwenye kota zao nyingine nyuma ya hospital ya kairuki mission, mikocheni. Achana na wale wapale makumbusho. Kwahiyo usikariri utendaji wao, wanaweza kuingia popote wakati wowote!
 
Evil!!! Malecela team typical hii!! na wenzako wote ndiyo mnao iponda NIMR !!! sababu tu mlitumbuliwa sasa mnachuki na walee walio baki NIMR, mnaanza kuchombeza fitna kwa uongozi wa sirikali ujao!! lengo ni ili wafikirie kuifuta NIMR eti haina faida!!

kumbuka nyie na kundi lenu lile la ulaji ndo mmeifikisha NIMR hapo ilipo mliifanya kuwa Mali yenu binafsi ya kufadisha marafiki na familia zenu mnachaguana! chaguana tu kindugu kirafiki na kulindana kimaslahi!! mliifanya km kijiwe binafsi!

Ulikwa ukiwa na msimamo tofauti tu na huyu mtoto wa Malecela unafutwa kazi! sasa amefukuzwa kitambo ana kinyongo na hii hali anaona km ameonewa kijicho anataka rudi imeshindikana!! wewe na mnao fanana na hao tunawajua vizuri sana hapa NIMR.

Baada ya wana NIMR kuona hamfai kuongoza Organisation hii!! na kuwaambia wazi wazi mkachukukia, baadhi yao mkawapiga chini!! baadae tuliobaki mkaona km tumewachongea kwa Rais, tuna roho mbaya, chuki, hatuwapendi tuna chuki binafsi!!

Kutumbuliwa kwenu ndo sababu za chuki zooote hizi zenye chokochoko mlima!! kuwa NIMR haina maslahi kwa taifa wakati nyie mpo mbona Maneno km haya hayakuwepo haya yoote??? nchi kama Nchi Medical research ni uhai wa taifa!!! chunguza Duniani poote!

Uta chunguza vipi magonjwa na tiba muafaka ya watu wa jamii yako pendwa yaani wananchi bila chombo hiki? pia kumbuka NIMR inaushirika na mashirika mengi ya kimataifa Duniani km CDC tunashirikiana nao kufikia lengo letu la kitabibu !!

kifupi ni uhai wa Dunia, siyo uhai wa Tanzania tu pekeyake!!! Dunia ya leo tunahitajiana mno kitiba, ki afya !! kiuchumi pia Kuliko unavo dhani kibinafsi yako! umeeleza kiwivu wivu sana!! labda ungesema tuifanyie mabadiliko inapo bidi! hapo ningekuelewa!

Ndg Rais utakaekuja na uliepo sasa!! jiulize kwa nini NIMR ipondwe kwa wakati huu wa utumbuaji moto moto na si kabla? hao hao waliokuwa wanaiyumbisha NIMR ndo wanaleta za kuleta sasa , sababu wanaijua mwanzo mwisho! Malecela Group!

NIMR haitafutwa ila tutawafuta watendaji/ wafanyakazi/washirika wasio kuwa na tija, wabovu wavivu, wazembe wasio wabunifu!! wala hatuna mpango wa kujaza tu Medical personel kwenye chombo hiki pendwa hayo siyo malengo ya NIMR!!!

Lengo letu kitaaluma ni sisi kama NIMR watu wenye;

Mtizamo chanya

Nidhamu za kitafiti

Upeo!

Ari!

Uwezo wa kitafiti!

Nia! sababu

capacity

Malengo,
Nidhamu nk kwa ajili ya kufikia malengo yetu muanana ya kitafiti!! hatukurupuki kuajili wafanyakazi wa kufanya tafiti tuliyo yafanya ni mengi sina haja ya kuyaorodhesh hapa! umesema kwa ajili uko full jazba .kisasi mtuache tufanye kazi!

Uhai wa Idara ya Afya ni Muhimu sana kuliko unavodhani, na tuna tabia ya kuwakaribisha Madaktari wote TZ kufanya nao majadiliano ya research za kiafya Mfano EBOLA walikuja Madaktari wote TZ Kina Dr Manyonyi, Dr kingu. Dr Mnzava, Dr Ulusubisya, Dr Liburu, L. Chipata, Dr Liwa na

Wengine weeengi kutoka kila kanda sasa wewe kwa mawazo yako unawaza usawa wa kinywa! na chuki fupi fupi!! utafiti wa afya ni wa kila kada ili mradi tu umeonyesha nia na mwelekeo chanya wa kufikia malengo ya Taifa,

Usitufundishe kazi iliyokushinda!! kaa pembeni!!! daima humu NIMR ni ya wote tuko hivo na tutakuwa hivo, kikubwa zingatia nidhamu zaa kitafiti!! utakaa nasi!! usijaribu kutupangia wala kuingiza siasa za maji taka!

Sisi ni wataalamu!! yes!! tuko hivo kwani nini bana!! hata Rubani. Mwanasiasa!! Mwanga, mwenye maono ya Kitabibu au kiujumla kiafya tunamkaribisha kwa mikono miwili! tunajua tunakokwenda na tunako toka!

Hatuyumbi na kila upepo unao vuma eti kwa sababu tulikufukuza weee!! thubutu!! fikiria mara mbili ndivo tulivo! kazi yetu sisi ni utafiti wa magonjwa ndo tulivo amua! tuna tambaa na ruzuku tofauti na unavo fikiria! chapa kazi acha majungu!!

Tunacho jali ni uwezo wa mtu yeyote, mwenye nia na sababu za kutatua tatizo la kiafya Duniani, kuna mpaka waganga wa kienyeji humu, hata wewe km ukijirekebisha na umekuja na wazo jipya tutakurudisha tena!

Tatizo lenu waswahili mnaendekeza ulaji wa kishamba mnooo!! kisa vijisenti!
NIMR ISIFUTWE KAMWE, ILA IFANYIWE MAREKEBISHO TUUUU!! NARUDIA SIJAKOSEA...........IKITOKEA imefutwa kwa chuki za kisiasa na ujinga wa ki tz KM HUU itakuja kwa umbo lingine tofauti Kabisaa!!
Naona umekuja kimipasho. Funguka zaidi.
Katika porojo zote hizi ulizoandika, umejibu hoja ipi?
Umezidi kuthibitisha kuwa NIMR haina tija. Kazi kulamba ruzuku tu, hakuna suluhisho lolote la changamoto za tiba mliloleta tangu hii NIMR ianzishwe hadi leo, mnarithishana vizazi vya wapigaji tu
 
kitu kipo ila hakitoshelezi na kuna sababu kwanini hakitoshelezi
Sababu gani ?? Lack of fund? Yaan mnakaa kimya mpak wananchi tuanze kuchunguza chunguza et kuna sababu ..aiseee Raisi anatakiwa ashushe nyundo Kali Sana hapo NIMRI to fu-ck them .....
 
Nakubaliana na wewe mkuu100%.Niliwahi kusema humu siku moja .kuna taasisi za serikali sizionagi kazi ya kim kakati.Mfano,naona hata taasis za elimu ya juu ni kama tuition centres tuu. Sionagi ile segment ya research inafanyaga nini hasa.

Hebu tuangalie Muhimbili, SUA, UDSM. haya ni mataasisi makubwa lakini sijawahi kusikia wamefanya utafiti wa kutatua changamoto zilizopo. Na wenyewe wameingia katika mtego wa kuazimia kuongeza mapato yatokanayo na karo,ila siyo kushughulikia tafiti ya kutafuta majibu ya changamoto.Angalia watu wanaoitwa Taasisi ya lishe Tanzania.

Sioni wanafanya nini hasa.Taasis zote zimewachia wanasiasa wanatuchanganya na milishe ambayo haijahata hata patiwa approval na TMDA.

Yaani kipindi hiki tunalishwa kila kitu kwa kweli.Nimeona hata UDSM nao walikuja na mchanganyiko wa tiba mbadala.Sasa sayansi waliyosomea imepotelea wapi.ni kweli kwamba wote walisomea tiba mbadala.Kuna Taasisi inaitwa Ifakara Health Institute ,kidogo sana hii imejaribu jaribu kwenye malaria,lakini nayo imejifia yenyewe.

WANASANSI WETU MKO WAPI? MMEISHIA KUTUTISHA KUHUSU CHANJO YA CORONA ILA HAMJABAINISHA KAMA NI KWELI MLIFANYIA UTAFITI HIYO CHANJO AU NA NYINYI MNASIKILIZA HABARI ZA MITANDAONI KAMA SIYE WA HUKU NANJILINJI MTWARA VIJIJINI

Mkuu....SUA wanajitahidi kidogo!
 
Hizo kazi za kuendesha miradi ya malaria, kichocho na matende zingeweza kufanywa na watu wa idara mojawapo pale wizara ya afya na kwenye halmashauri zetu, siyo na taasisi ya medical research. Hizo ni public health projects, na hazihitaji kuongozwa wala kusimamiwa na medical researchers, hizo hata watu waliosomea community development na sociology ndio kazi zao kupita kwenye jamii kuhimiza matumizi ya chandarua, matumizi ya choo bora nk. Tunaona hata huku mitaani watu wanaohimiza kwamba "Usichukulie Poa Nyumba ni Choo" ni akina Mrisho Mpoto na Shilole, wasanii wenye influence kwa hadhira.
Medical Researchers hawapaswi kuvamia kazi ambazo sio medical research. Wanapaswa wafanye tafiti za tiba walete majibu ya changamoto zilizoko katika tiba ya binadamu: dawa bora, vifaa tiba, mbinu bora za operesheni na mengine ya aina hiyo katika tiba.

Sasa hawa wenzetu huko NIMR baada ya kuona medical research imewashinda ndio tunawasikia kila siku wakiimba matende na mabusha na kugawa dawa za minyoo mashuleni. Dawa hizo zilitafitiwa zamani na kuthibitishwa ubora wake huko zilikotoka kwa mabeberu, hapa kwetu zimepata usajili na kuruhusiwa kutumika, eti NIMR wako busy kugawa dawa! Hiyo kazi hata ukimpa mwalimu wa shule ya msingi ukamwambia gawia kila mtoto kidonge kimoja anywe na glasi moja ya maji atashindwa?
Ni kweli mkuu lakini ndo kichaka chao cha kupigia hela tena kwenye hizo project huwa wana mpaka watu wao wameisha wapanga, kwenye suala la utafiti ni changamoto ndo maana unaona hata madawa na vifaa tiba vingi tunategemea kutoka nchi za nje
 
Wapi nimesema kwamba wote wanoafanya kazi Muhimbili lazima wawe wamesoma medical?! Huna hoja kilichobaki unalazimisha kusema kitu ambacho huwezi kukithibitisha.
Nimekuuliza msemaji wa hospitali nyeti kama ya Muhimbili inawezekanaje akawa mtu asiye na background kwenye masuala ya AFYA!
Mpaka sasa hujajibu umebaki kuruka ruka tu kama maharage yanayochemshwa kwenye sufuria na madai ya kishamba kwamba unaijua Muhimbili yote na TISS wote.Jibu hoja zangu, acha kutishia nyau watu wazima.


Acha kuzunguka mkuu, sio wewe. Uliyesema hakuna mtu anayefanyakazi muhimbili bila kuwa na background ya afya?! Huu ni uongo, wako wengi tu hawana background yoyote kwenye medical, nimekuwa nafanyakazi mradi wenye mahusiano na muhimbili kwa zaidi ya miaka 5 , nimeingia pale almost kila week mara 2 au tatu randomly,

Sijui kiwango chako cha elimu na ufahamu , japo Nina doubtful nacho, wapi nimesema naijua muhimbili yote na tiss yote?! Mbona unaanza kuleta maneno yakwenye taarabu. Wewe ni mshamba huna ukijuacho ni taburasala.
 
Naona umekuja kimipasho. Funguka zaidi.
Katika porojo zote hizi ulizoandika, umejibu hoja ipi?
Umezidi kuthibitisha kuwa NIMR haina tija. Kazi kulamba ruzuku tu, hakuna suluhisho lolote la changamoto za tiba mliloleta tangu hii NIMR ianzishwe hadi leo, mnarithishana vizazi vya wapigaji tu
NIMR ilikuwepo!! itakuwepo, ruzuku italambwa sana utakake!!usitake!! vimba pasuka!! wewe ndo unapasha kitu ambacho hukijui!
Narudia haitakufa ukiona imekufa ipo kivingine! siyo ruzuku ya Pesa ya Madafu ile!!! uliza ujibiwe!!
 
Sababu gani ?? Lack of fund? Yaan mnakaa kimya mpak wananchi tuanze kuchunguza chunguza et kuna sababu ..aiseee Raisi anatakiwa ashushe nyundo Kali Sana hapo NIMRI to fu-ck them .....
for your information siko NIMR, ila nasema kinachojadiliwa hapa. Nani kasema lack of funds? inaelekea una ubaya na NIMR... wewe ni kiumbe mdogo kuathiri NIMR. Nenda mabibo uone wanachokifanya, Nenda NIMR makao makuu kaone wanachokifanya, tembelea centres zao uone wanachokifanya
 
Back
Top Bottom