Nimsaidieje kisaikolojia atoke kwenye hii hali?

Nimsaidieje kisaikolojia atoke kwenye hii hali?

Tatizo wanawake ni wengi kuliko wanaume, tusipojitolea wapo wanawake watakosa wapenzi kabisa
Kama unajinasibu kuwa una imani ya kikristo na ukajongea Altareni ukafanya AGANO takatifu la ndoa Huna haja ya kusema haya....

kama ni Islam na umefikisha wake wanner Huna haja ya kusema haya.

Kama ni mzee wa mila kwann uweke mchepuko ilhali taratibu za kufata zipo wazi

Lindeni baraka zenu, jiepusheni na laana. Mnajiongezea stress bila kujua resulting ro vifo vya mapema.

Uzinzi ni laana
 
Kuna kipindi nilikuwa sehemu kikazi mbali na nyumbani nikawa na binti mmoja kama tulizo la upweke.

Ilikuwa kila ninapomuhitaji anakuja na shida zake ndogo ndogo namtatulia. Ilikuwa ni binti decent kimuonekano.

Siku moja ilikuwa nina safari ya kurudi nyumbani. Nilishinda nae siku nzima maana safari ilikuwa ni usiku. Mida ya jioni kulikuja wageni ikabidi yeye abaki chumbani mimi nikawa sebuleni. Kabla ya kwenda sebuleni niliweka pesa nyingi kidogo kwenye droo chumbani lakini nilijua kabisa kiasi chake.

Baada ya wageni kuondoka na muda wa safari kuwadia nilitoa zile pesa na kumpa cha kumpa na kuondoka.

Nilipofika airport kuweka vitu sawa nikagundua ile pesa imepungua kama $500, nikajua moja kwa moja ni yeye.

Baada ya wiki nilirudi huko huko kuendelea na majukumu. Kitu ambacho alikuwa hajui yule binti ni kuwa chumbani kuna camera ambazo kama sio mzoefu huwezi kushtukia.

Nilifika nakutoa SD card na kuangalia siku husika na kumuona binti akichukua pesa na kuficha kwenye sidiria.

Nilimpigia kumjulisha nimerudi na kweli akaja kuniona. Nikamuuliza kama alichukua pesa kwenye droo. Demu alikataa kabisa.
Hapo hapo nakamtumia ile clip ya camera ikimuonyesha anachukua pesa. Alipoifungua message na kuona tu alinyanyuka bila kuaga na kutokomea zake.

Sikumuona tena na hata namba yake ikawa haipatikani tena.

Mwanamke akishikwa wizi na pozi linaisha. Huyo wako atajiondoa mwenyewe maana anahisi thamani yake imeshuka kwako kwa kujua ni kibaka.
 
Wakuu habari?

Jana mida ya saa tatu usiku, niliamua kutoka na mpenzi wangu (mchepuko) na kwenda naye katika kiwanja kimoja angalau kujiburudisha pamoja na kupunguza msongo wa mawazo ya hapa duniani.

Tukiwa kwenye hicho kiwanja, tulikula, kunywa pamoja na kucheza mziki; ilipofika saa tisa na nusu usiku tuliamua kurudi nyumbani kwa sababu tulikuwa tumechoka sana pamoja na kulewa.

Baada ya kufika nyumbani na kujisachi kwenye mifuko yangu ya koti, nikagundua kuna kiasi fulani kimebaki na sijakitumia. Nikazihesabu na baada ya kujiridhisha nikaziweka kabatini.

Mwenzangu akajua labda nilikuwa nimelewa na sina kumbukumbu yoyote; sasa leo jioni akawa anajiandaa ili aweze kuondoka, ikanibidi niende kabatini ili niweze kumpatia chochote.

Ile nafika tu, nikakuta salio liko pungufu; ndipo nilipoanza kuhoji, akawa mpole kiasi na kuanza kulalamika hawezi kuchukua chochote bila kuniomba. Mbaya zaidi nikawa namtajia kiasi halisi ya fedha zilizokuwepo, na kumthibitishia sikupoteza kumbukumbu.

Nikawa kidogo mkali, na nikasema sipendi kuwa kwenye mahusiano na mtu mdokozi; ndipo nikaamua kutoka nje ili nimuachie nafasi apumue.

Ile nimekaa nje kama dakika tano hivi, akaniita na kuniambia, ''hela zako ni hizi hapa nimezikuta hapa chini, na huwa sipendi mimi kuitwa mwizi''

Nikamwambia abaki nazo tu, kwa sababu nilishajua zimepotea katika mazingira ya kutatanisha.

Baada ya hapo akawa mkimya na kununa, kuongea hataki; mpaka jamaa wa boda akaja kumchukua na akaondoka bila ata kuniaga.

Nahisi atakuwa ameona aibu na nafsi inamsuta kwa alichokifanya,ingawa mimi nimemsamee na sijamtuhumu kuwa yeye ni mdokozi; mbaya zaidi ana ujauzi wangu.

Najua hii hali itamtesa kisaikolojia, baada ya kugundulika yeye ni mdokozi.

Sasa wakuu, nimsaidieje kisaikolojia atoke kwenye hii hali?​
Mkuu hali iliyokukuta kwa Kiswahili fasaha inaitwa "KIFEWE". Cha msingi utambue mapenzi ni kikohozi, na bibie huwa unampatia pesa kidogo sana za matumizi, mpaka analazimika kukupiga hali ukiwa chakari na umelewa.

Starehe na kumega kitumbua unaendekeza tena kutoka kwa mchepuko! Hali unamfanyia ubahilli hali akitambua fedha za kutosha unazo!?

Tambua yeye ni mdangaji, hivyo ni vyema ukatambua uzito wa wa matatizo yake bonafsi, kisha anza kumpa mtoto fungu la kutosha iñi aweze kutatua baadhi ya shida zake, uone kama atakuja kukuibia tena kwa kificho.

Tambua kila kitu kinachopatikana kwa urahisi huwa kina gharama zake. All in all, kuwa muaminifu katika ndoa yako.
 
Kama unampenda ongea nae ujue shida nini ili uzidishe huduma,Mwite muweke chini baada ya hapo ni mikuno na mikazo tu,kesi kwisha..
 
Kuna kipindi nilikuwa sehemu kikazi mbali na nyumbani nikawa na binti mmoja kama tulizo la upweke.

Ilikuwa kila ninapomuhitaji anakuja na shida zake ndogo ndogo namtatulia. Ilikuwa ni binti decent kimuonekano.

Siku moja ilikuwa nina safari ya kurudi nyumbani. Nilishinda nae siku nzima maana safari ilikuwa ni usiku. Mida ya jioni kulikuja wageni ikabidi yeye abaki chumbani mimi nikawa sebuleni. Kabla ya kwenda sebuleni niliweka pesa nyingi kidogo kwenye droo chumbani lakini nilijua kabisa kiasi chake.

Baada ya wageni kuondoka na muda wa safari kuwadia nilitoa zile pesa na kumpa cha kumpa na kuondoka.

Nilipofika airport kuweka vitu sawa nikagundua ile pesa imepungua kama $500, nikajua moja kwa moja ni yeye.

Baada ya wiki nilirudi huko huko kuendelea na majukumu. Kitu ambacho alikuwa hajui yule binti ni kuwa chumbani kuna camera ambazo kama sio mzoefu huwezi kushtukia.

Nilifika nakutoa SD card na kuangalia siku husika na kumuona binti akichukua pesa na kuficha kwenye sidiria.

Nilimpigia kumjulisha nimerudi na kweli akaja kuniona. Nikamuuliza kama alichukua pesa kwenye droo. Demu alikataa kabisa.
Hapo hapo nakamtumia ile clip ya camera ikimuonyesha anachukua pesa. Alipoifungua message na kuona tu alinyanyuka bila kuaga na kutokomea zake.

Sikumuona tena na hata namba yake ikawa haipatikani tena.

Mwanamke akishikwa wizi na pozi linaisha. Huyo wako atajiondoa mwenyewe maana anahisi thamani yake imeshuka kwako kwa kujua ni kibaka.
Inasikitisha sana
 
Back
Top Bottom