Nimuoe nani?

Nimuoe nani?

Sifahamu nafanyaje kumpm mtu
 
Plato kaomba ushauri, ajabu watu wanaanza kumtukana. Kama huna ushauri ni heri ukae kimya, kwani matusi sio ustaarabu. Hata Achebe alisema; " The fox must first be chased, then the hen should be warned about wandering in the bush".
 
Dah pole kaka angu.
Hakuna jaribu lisilo na mlango wa kutokea.
Nimeumia, lakini pia sitakiwi kuhukumu sana, manake sijawahi kuwa safi asilimia mia moja.
Hata kama sio katika uzinzi hata katika mengine tu.

Hebu nyenyekea mbele za Mungu wako, muombe rehema na Neema ya kupita hapo ulipo sasa.
Tulia kimya, kubali kila lawama na neno utakalotupiwa/nenewa na wazazi wa hao mabinti, rafiki na ndugu zao, na machozi watakayolia,
ndiyo, mshahara wa makosa yako. Uwe mpole, huku ukiomba hekima.

Mke mwema hutoka kwa bwana, haijalishi umelipa mahari, au umezalisha, Mungu anawawazia mawazo ya Amani hao mabinti kuliko hata mimi na wewe, tunavyowawazia. Tulia kabisa waombee hao mabinti, hasa huyo mwenye mimba Mungu amjalie ajifungue salama.
Apate nguvu na afya, baada ya hapo naamini hata akili itakuwa imetulia, na utafanya uamuzi sahihi.

Kumbuka ukifanya uamuzi sahihi, itakuwa faida kwenu nyote, kwani ukimuoa yule anayeendana nawewe, utakuwa na amani kwenye familia,
na huyo mwingine naye Mungu atamjalia mume mwema, na ataishi kwa furaha.

Pole sana, hii ndiyo dunia tunayoishi, wewe sio wa kwanza wala hautakuwa wa mwisho. Kikubwa unyenyekevu unahitajika sana hapa.
Ili uvuke salama.

LD nina moja tu la kusema..UNA BUSARA SANA!Mungu akuzidishie.
 
LD nina moja tu la kusema..UNA BUSARA SANA!Mungu akuzidishie.

Ubarikiwe Sweetdada,
Unajua hapa duniani bwana, wakati mwingine, kile unachotamani sicho kinachotokea,
bali lile ambalo hata hukuwahi kufikiria kama utakutana nalo.

Hasa kwenye haya mambo ya mahusiano.
 
Ndg yangu hufai kabisa, kwa upumbavu uliofanya hakuna wakukushauri! Una matatizo ya akili, kwanza nenda kwa wanasaikolojia wakushauri na pia muone dk apime hiyo akili.
 
Dah pole kaka angu.
Hakuna jaribu lisilo na mlango wa kutokea.
Nimeumia, lakini pia sitakiwi kuhukumu sana, manake sijawahi kuwa safi asilimia mia moja.
Hata kama sio katika uzinzi hata katika mengine tu.

Hebu nyenyekea mbele za Mungu wako, muombe rehema na Neema ya kupita hapo ulipo sasa.
Tulia kimya, kubali kila lawama na neno utakalotupiwa/nenewa na wazazi wa hao mabinti, rafiki na ndugu zao, na machozi watakayolia,
ndiyo, mshahara wa makosa yako. Uwe mpole, huku ukiomba hekima.

Mke mwema hutoka kwa bwana, haijalishi umelipa mahari, au umezalisha, Mungu anawawazia mawazo ya Amani hao mabinti kuliko hata mimi na wewe, tunavyowawazia. Tulia kabisa waombee hao mabinti, hasa huyo mwenye mimba Mungu amjalie ajifungue salama.
Apate nguvu na afya, baada ya hapo naamini hata akili itakuwa imetulia, na utafanya uamuzi sahihi.

Kumbuka ukifanya uamuzi sahihi, itakuwa faida kwenu nyote, kwani ukimuoa yule anayeendana nawewe, utakuwa na amani kwenye familia,
na huyo mwingine naye Mungu atamjalia mume mwema, na ataishi kwa furaha.

Pole sana, hii ndiyo dunia tunayoishi, wewe sio wa kwanza wala hautakuwa wa mwisho. Kikubwa unyenyekevu unahitajika sana hapa.
Ili uvuke salama.
Now you are talking,ushauri maridadi kabisa! ngoja nikupige na senks nyingine kwa niaba ya Plato....THANKS....BIG UP LD!
 
Plato, Kama upo serious ni PM nikupe ushauri zaidi kwa hapa nikitoa huo ushauri nitaharibiwa siku, halafu nikijibu BAN juu

we mwaga ushauri hapa. Inawezekana wapo wengine wenye hilo janga. Inawezekana kesho yakamkuta mwingine.
 
Hapa wa kuolewa ni mchumba kwa maana taratibu zote zimezingatiwa. Huyu mwenye mimba atakuwa mtazamaji au ukiendeleza uchakachuaji atakuwa nyumba ndogo @your own risk.
 
ya hii thread imenikumbusha kauchungu ka best yangu, yeye tulikuwa kwenye process za ndoa na ndoa ilikuwa ifanyike after Easter, last 3 weeks best yangu akagundua jamaa alikuwaga na mke na amezaa naye watoto 2,1st born yuko 4m 2 na 2nd one yuko 4m 1 na wameachana na mkewe 3yrs ago. ndo wako kwenye hayo malumbano na kila kitu kimesitishwa mpaka wao waweke mambo sawa.

ili kukwepa usumbufu wa baada ni bora uwe mkweli kwao mapema tuu.
 
kila mmoja mwambie kuhusu mwenzake alafu watachagua wenyewe
 
Multiple choice;
a). Waoe wote kwa maana umejitakia kwa tamaa zako, na uwe tayari kumuongeza na mwingine....! Lakini ujue kuwa kila mwanaume akiwa na wanawake wawili, basi pembeni ana mume mwenzie.....!

b). Waache wote, na hivyo pia uwe tayari kuendelea na maisha ya ukapera daima huku ukiwa na laana zisizo na suluhisho hadi motoni.....!

c). Kaa kimya, kwa maana when the time is over, it will tell who you have to marry.....! Na kwa vyovyote uaminifu hautakuwepo kwenye ndoa hiyo daima maishani mwako....!

d). Yote hayo yakikushinda basi jiue aidha kwa sumu au kwa kamba, ili wote wakukose na uzikwe ukiwa na amani kama ndio kusudio lako....!

d) imeharibu utashi wako wote!
 
Nashindwa kufanya maamuzi.nisaidieni mawazo.yanisaidie kufanya maamuzi. Nina wasichana 2,mmoja ni mchumba wangu,uchumba wetu una miaka 3 sasa,na tumetoa zaidi ya mahari.nilimpromisse kumuoa mwaka kesho akasema atanisubiri na amefanya hivyo.ninampenda sana.nadhani naye ananipenda.lakini upande mwingine rafiki yangu wa miaka mingi(msichana) mhitimu wa university ambaye aliachana na boyfriend wake na akakaa zaidi ya mwaka bila uhusiano.ikatokea tumezoeana sana ndg zake wengi wakanijua tukawa kama ndugu.mwaka jana nikiwa na mchumba tayari tukaanza kuwa na mahusiano ya mapenzi.akawa anaongea kuwa anaridhika nami hata nikimuoa kwani ananifahamu.sasa imetokea akapata mimba,na yeye kafurahi kwamba si nitamuoa.hajui habari za mchumba wa tangu kabla yake.mimba ina miezi 4 sasa.UTATA: Nimuoe nani kati yao,inaniwia vigumu kuvunja promisse kwa mchumba aliyenivumilia kwa miaka 3 sasa,wakati huohuo inaniwia vigumu kumtelekeza niliyempa mimba na kubadili maisha yake.pili nafikiri nn kitatokea kwa uamuzi wowote nitakaochukua.kwangu limekuwa zito,nishaurini.asante




Umekwisha msaliti mchumba wako kwa tamaa tamaa yako,mi naona mweleze ukweli mchumba wako huyo uliye naye kwa miaka mitatu,mwombe msamaha,muoe!Huyo mwingine kubali kugharamia kutunza mimba na mtoto akizaliwa mungu akipenda!Nae mwombe msamaha kwa kumpotezea muda wake!mwambie ukweli kwamba hutamuoa! KUWA NA MSIMAMO KATIKA MAHUSIANO YAKO,yatadumu!
 
love is really complex! unadai unampenda huyo uliyemuita mchumba, lakini nashangaa kama kweli unampenda kwa nini umemsaliti? I dont think is the time to think about ur-self any more, ili uweze kumake right decision think about the life your child will live and about your lovers just be honest to them, then you will be able to decide. To be honest you deserve all the blames, inabidi uombe msamaha + toba na ujirekebishe ili kuepuka laana. pole sana
 
muoe yule uko happy nae.....anayekuridhisha kila kitu,kukufanya usitoke nje! kwa mtazamo wangu hao wawili hawana vigezo vya kukutosheleza ndio maana ukatembea nao wote,cha kufanya wabwage tafuta mwanamke mwenye vigezo vyote unavyovitaka ndio uoe..
 
Back
Top Bottom