Nimwache akapange au niondoke mimi?

Nimwache akapange au niondoke mimi?

Duh wanasema ukitaka kujua kama kuna watu wanaumwa kuliko wewe basi tembelea hospital. Pole Sana nilidhani me yangu nimakubwa sana kumbe kuna wenzangu wanamakubwa zaidi yangu nilighairi kwenda kujitambulisha mwezi huu kwasababu ndogondogo sana ila acha tu nijipange niende maana yako nimakubwa Sanaa yaani yangu hayaingiii kwako hata robo. Narudia tena pole sanaaa
Hahahahaha nacheka kwa dharaaaaaau.
 
So aliondoka au uliondoka na kumwachia kila kitu?
Mm nilimfanyia busara tu nilimuachia kitanda na godoro na kumpa 200k nikamwambia tu kuanzia mwezi ujao utakuwa unapata matumizi ya mtoto 50k saivi tunaeshimiana vizuri na ninamtu mwingine maisha yanakwenda
 
Kuondoka anasema mpaka mwakani, mimi nimechoka sana na nikimwona najawa na hasira sana kiasi kwamba huwa naondoka tu home na kwenda matembezi yangu sometimes naenda kulewa. I am so stressed kiasi kwamba sitaki ugomvi kabisa
unaona sasa!umeamua hadi kuwa mlevi!achana na huyo kima...kama anataka kuondoka mwakani...ondoka wewe!mtu alishindwa kuishi na dada yake akisingizia ananyanyaswa kumbe yeye ndo alikuwa na tabia chafu...mwachie nyumba usepe!ngoja ngoja atakupiga dafulau hutakuja kusahau!
 
Samaki mkunje angali mbichi, nimesoma huu uzi niakagundua matatizo mengi sana yanayotokea kwenye ndoa/mahusiano chanzo ni sisi wanaume na ujinga wa kujiendekeza, mimi najali na kumpenda mtu sana tena hata pasipo jali napoteza ila mtu akianza kutojali hisia zangu au kunijali mimi huwa napotezea hata kama nampenda kiasi gani mimi huwa napotezea, sasa mkuu wangu umelibeba tatizo kwa muda mrefu unaenda nalo tu, sasa ana mtoto wako swala ambalo linakupa wakati mgumu kuwaza ufanyaje.. Mimi nilikataa kuendeshwa na mwanamke hata kama nampenda kufa kuna mipaka sitaruhusu avuke
 
Habari wanaJF, naomba mnishauri pia kwa hili.

Nilikutana na binti mmoja mwaka 2012 katika mazingira ya kazini na tukaingia katika mahusiano, binti huyo alikuwa akiishi kwa dada yake mkubwa ambaye wamechangia mama. Kwa mujibu wa maelezo yake ni kwamba dada yake huyo alikuwa akimnyanyasa na kitendo kile kiliniuma sana nikaamua kumpangishia chumba akaanza maisha yake hapo, hiyo ilikuwa ni 2013. Tuliendelea na mahusiano mpaka niliamua kujitegemea mwaka 2015 na tangu mwanzo wa mahusiano yetu alikuwa akija mpaka nyumbani kwetu na ndugu zangu wote wanamfahamu. Aliamua kuja kuishi na mimi hivyo nilimkaribisha tukaishi wote, sasa hapa ndo matatizo yakaanza.

Alianza kuzua migogoro ndani na hatukuwa tunaelewana mara nyingi, nilikuwa na biashara nikamweka asimamie biashara ile nilikuwa najua inaingiza kiasi gani lakini tangu aanze kusimamia iliyumba na hakuwa ananishirikisha mauzo ya siku. mostly jibu lake lilikuwa biashara mdogo mdogo, mwaka huo huo akashika mimba na Mungu akajalia akajifungua 2016 March, kipindi hicho nilikumbwa na mtikisiko mkubwa kiuchumi hivyo hali haikuwa nzuri. Katika maisha yetu alikuwa ni mtu wa kufanya maamuzi peke yake na nikijaribu kuhoji inakuwa ugomvi nikaamua kukaa kimya kuepusha shari. Hivyo aliwaleta ndugu zake kuishi kwangu bila idhini yangu maana hali ya uchumi ilikuwa si nzuri. Akaanza kulaumu kuwa ndugu zangu wanamchukia ilhali yeye alikuwa akienda kwetu hafanyi chochote ni kuketi tu muda mwingine hamsemeshi mtu anakuwa busy na simu yake. Tukitoka anaanza kutupa lawama kwangu kwamba ndugu zangu na mama yangu hawampendi. Nilijaribu kumwelewesha na kumwambia kuwa mama hapendezwi na tabia ya yeye kujitenga maana kama anahitaji kuolewa na mimi lazima achangamane na familia yangu lakini haikufua dafu. Hali hiyo iliendelea hata kufikia hatua mama yangu akimpigia simu hapokei kwa makusudi, nikimuuliza anasema hajisikii kuzungumza na simu, mama akipiga kwangu nikimpa pia jibu ni lile lile.

Hali hiyo ilinitesa sana maana nikiangalia maisha yake ya nyuma napata ugumu kumuacha maana namsikitikia mwanangu atateseka sana. Nilifanikiwa kupata kazi nyingine hapa Dar na kuhamia hapa mwaka 2017 July, nilianza kazi vizuri na nikawa natuma pesa za kutumia kama kawaida nilikuwa nikituma laki 2 kila mwezi kwa ajiri ya matumizi, na biashara ile ilikuwa ikiendelea kama kawaida japo sikuwahi kujua mapato yake kabisa. Cha kushangaza ni kwamba kila baada ya wiki mbili niliambiwa hakuna pesa ya kutumia na hakuna chakula mtoto hana chakula pia, ilinibidi nitoe pesa yangu ya kujikimu niitume kwao kitu ambacho kiliendea kuwa hivyo kwa muda wa miezi 5. Wakati mwingine sikuwa na pesa kabisa kwa sababu ya matumizi kwake kuwa mengi na nilijaribu kuhoji pesa inatumika vipi ilizua mgogoro sana. Na alikuwa mtu wa kulalamika na kunitumia sms za matusi[Zipo Zote] kunitukana lakini sikuangalia hayo maana imani yangu ilikuwa ni kujenga familia na huyo dada. Mwaka jana mwezi wa 12 nilimwambia ajiandae ahamie huku hivyo vitu vyote nikampa melekezo avipeleke kwa mama yangu na ndivyo tulivyokubaliana. Nilituma pesa ya nauli Tshs 210,000/= Kwa ajili ya safari (100,000/=) na kumalizia kodi ya nyumba (100,000/=) lakini huwezi amini kabla ya siku moja safari kuanza aliniambia kuwa hana pesa ya nauli nimtumie nauli.

Nilishikwa na hasira sana na tayari nyumba niliwambia wakabidhi kwa mwenyewe, Vitu aliamua kuita ndugu zake wakaja kuchukua bila kunishirikisha. Nilipigiwa simu na mdogo wangu akiniambia mbona mambo yako tofauti na mlivyopanga? kwa hekima niliwaambia wadogo zangu waondoke tu lakini pia haikutosha ndugu zake na huyo dada walianza kuwamwagia wadogo zangu matusi kiasi cha kushangaa kuna nini mpaka iwe hivyo. Nilimpigia huyo dada na kumuuliza kuhusu tukio hilo niliambulia matusi ya ajabu sana na hapo nimetoa tena pesa nyingine ya nauli ili tu mwanangu awe karibu yangu.

Nikajisemea kuwa akifika nitamhoji anieleze vizuri, lakini alipofika alikuwa ni mtu mwenye maneno mengi sana na matusi makali, niliamua kuachana nayo hayo na kufungua ukurasa mwingine wa maisha (Kumsamehe). Tukaishi maisha ambayo kila siku anazua jambo, wakati mwingine namsalimu haitikii, namsemesha hajibu ikafika wakati nikaamua kumtizama tu. Nilipanga niende kwao kutoa mahali mwezi wa 11 mwaka huu lakini kwa tabia hizi sidhani kama naweza. NImeshajaribu kuzungumza naye, kumshirikisha mchungaji wa kanisa analosali, kwa muda fulani nikaona mabadiliko lakini hali ilirudi vile vile. Ilifika kipindi nimetoka kazini nikamkuta ndugu yake kaja kumsalimu, kabla sijaingia ndani nilisikiwa wakinizugumza vibaya sana. Nilichukia sana lakini nikamwambia Mungu kwamba ikiwa mimi ndiye nimemfanya mtu huyu awe hapa sina haja ya kuchukia kwa hiki anachonena kuhusu mimi. Niliingia ndani nikabadili nguo zangu na kutoka kwenda matembezi.

Hivi karibuni kuna ndugu yangu alikuwa anaolewa huko kanda ya ziwa, nikamwambia huyo dada apige hesabu ya mahitaji yake na mtoto kwa ajili ya harusi. Alinipa hesabu yake nikasema sawa ilikuwa around 200K nikatafuta pesa Mungu akajalia nikapata 1M nikamwambia kuna pesa hii imepatikana so wajiandae kwa ajili ya kwenda kwenye harusi. Tulipanga kwenda kufanya shopping the next day. Tulikwenda kariakoo kuanza shopping, cha ajabu yale aliyopanga kununua nikaona anatafuta nguo za mama yake (Kitu ambacho hakuwa amenishirikisha na ilikuwa nje ya budget) nilikaa kimya nikamnunulia mwanangu, yeye alipomaliza kununua alivyokuwa ananunua akanambia anahitaji pesa ya kujinunulia yeye pia.

Seriously nilishikwa na hasira sana maana haikuwa katika budget, na ukizingatia tunakwenda kwa siku chache tu na hatukupanga kufanya yote hayo maana kulikuwa na mambo mengine ya muhumi ya kufanya baada yakurudi dar. Siku hiyo ilikuwa mbaya sana kwangu maana aliongea maneno makali sana kiasi kwamba nikashikwa hasira nikampa hiyo pesa aliyohitaji, aliema asante but sikumjibu kabisa. Tulikwenda nikijua tunafikia kwenye tukio lakini kumbe kwake ilikuwa ni tofauti tulipo fika alinambia nimpeleke kwa dada yake, nilifanya kama alivyohitaji. Nikategemea asubuhi atakuja ajishughulishe katika shughuli za tukio hakuonekana simu hapokei mara nakuja baada ya nusu saa mpaka ikafika jioni. Kesho yake nikamwambia ajitahidi kuwahi aje kujumuika na kusaidiana na wenzake lakini alikuja saa nne asubuhi na kunifuata moja kwa moja anaomba pesa aende salon. Sikumpa nilimwambia sina maana tayari alishaniudhi. Akaingia ndani kwamba anakwenda kubadili nguo aje kufanya kazi, kumbe haikuwa hivyo akaondoka kwenda zake salon. Sasa tangu hapo hakukanyaga tena kwetu, mpaka siku ya harusi yenyewe ndo akaonekana tena. Tulijumuika na baada ya sherehe kuisha nilianza maandalizi ya kurudi Dar, siku iliyofuata akaniambia anahitaji kuzungumza na mama yangu, mimi na ndugu zangu nikasema sawa. Akatuita tukaketi kumsikiliza akaomba msamaha wa kilichotokea na kuhusu matusi yaliyotukanwa kwenye sakata la vitu na mengine mengi wakamsikiliza na wakamwambia wao hawana tatizo kabisa, akanaambia nimsindikize kwenda kwa dada yake nikamsindikiza.

Huko njiani alinitolea maneno makali sana nikajiuliza kwamba huo msamaha aliokuwa akiomba alimaanisha nini? au alikuwa akiwajaribu ndugu zangu na mama yangu? sikutaka mengi wala sikujibu kitu nikamfikisha nikaondoka. Sasa mwezi huu ilikuwa niende kwao nikatoe mahali lakini moyo wangu sasa haumuhitaji tena maana naona tunakoenda nitafanya kitu cha ajabu juu yake kinachoniumiza ni mwanangu tu.

Nilimweleza kuhusu kuachana mimi na yeye akasema ataenda kupanga chumba hapa hapa Dar kitu ambacho nikifikiria mazingira hayo kwa mwanangu siyo kabisa, naombeni ushauri wenu nifanyeje? maana jambo hili limenichosha sana. binti ni mzuri but tabia zimenishinda
Sina hata chakukushauri maana story tu lakini nimeshachukia sana, una moyo mkuu pambana tu, inaonekana kuna kitu nyuma ya pazia hebu mchunguze nn kinamfanya hivyo ni kweli yupo na akili zake timamu au ashachanganyikiwa,tafuta namna yakumnyanganya mtoto wako pia maana hata usalama wako ni tatizo
 
Kwa story hii mkuu... Hilo gari paki, vuta hand break tulia....! Akishuka endelea na safanri..., Amekuhangaisha mpaka umeshindwa kutumia ile akili tulioambiwa tuishi nao hawa wenzetu... Pole sana mkuu!
 
Mkuu umenikera sana kwakweli[emoji48]
[emoji53],, unawezaje kuvumilia ushenzi wote huo kwa muda wote huo na bado unampa na Hela...Kaka usituaibishe wanaume...Tafadhali unapomaliza kusoma hii comment nenda kamlambe makofi mawili ya haja umfukuze mbali sana...mtoto atamlea kupitia ustawi wa jamii...matumizi 50k/month
 
Sina hata chakukushauri maana story tu lakini nimeshachukia sana, una moyo mkuu pambana tu, inaonekana kuna kitu nyuma ya pazia hebu mchunguze nn kinamfanya hivyo ni kweli yupo na akili zake timamu au ashachanganyikiwa,tafuta namna yakumnyanganya mtoto wako pia maana hata usalama wako ni tatizo
kuna kitu anajiamini huyo si bure.
 
Ninampango wa kuondoka nimwachie kila kitu maana uwezo wa kununua vingine upo so vitu kwangu siyo shida, labda nguo zangu tu na vifaa vyangu vya kazi
Tuseme unamwachia nyumba ambayo kwa mwezi kodi ni laki n nusu au laki mbili siku akija kukosa kodi nani atalipa kama si ww au atakuja kukurubuni kuwa kabadilika akakupa na mauno kama yote ukaamini kabadilika kumbe maisha yamemshinda mm nakwambia mwache aende mpe pesa kidogo na vitu vya ndani mgawane usimuonee huruma brooo ivi ushawai jiuliza watoto wanaokaa vijijini bila baba zao tena wamefariki si ww ambaye unatuma pesa unajua wanaishije acha huruma za kijingaa nakwambia mpe fundisho ambalo atajutia maisha yake yote mwache akapange nyumba ya uwezo wake
 
Kama mtoto anaumri mzuri wa kulelewa na bibi yake yaani mama yako basi ni kheir ukaachana nae, beba mwanao peleka kwa bibiake na mwaache akazurure njiani. Ila nafkir ulishaonesha udhaifu mkubwa awali ndio maana ana kuringishia sana.
 
Tuseme unamwachia nyumba ambayo kwa mwezi kodi ni laki n nusu au laki mbili siku akija kukosa kodi nani atalipa kama si ww au atakuja kukurubuni kuwa kabadilika akakupa na mauno kama yote ukaamini kabadilika kumbe maisha yamemshinda mm nakwambia mwache aende mpe pesa kidogo na vitu vya ndani mgawane usimuonee huruma brooo ivi ushawai jiuliza watoto wanaokaa vijijini bila baba zao tena wamefariki si ww ambaye unatuma pesa unajua wanaishije acha huruma za kijingaa nakwambia mpe fundisho ambalo atajutia maisha yake yote mwache akapange nyumba ya uwezo wake
Asante brother
 
Kama mtoto anaumri mzuri wa kulelewa na bibi yake yaani mama yako basi ni kheir ukaachana nae, beba mwanao peleka kwa bibiake na mwaache akazurure njiani. Ila nafkir ulishaonesha udhaifu mkubwa awali ndio maana ana kuringishia sana.
 
Kama mtoto anaumri mzuri wa kulelewa na bibi yake yaani mama yako basi ni kheir ukaachana nae, beba mwanao peleka kwa bibiake na mwaache akazurure njiani. Ila nafkir ulishaonesha udhaifu mkubwa awali ndio maana ana kuringishia sana.
 
Kama mtoto anaumri mzuri wa kulelewa na bibi yake yaani mama yako basi ni kheir ukaachana nae, beba mwanao peleka kwa bibiake na mwaache akazurure njiani. Ila nafkir ulishaonesha udhaifu mkubwa awali ndio maana ana kuringishia sana.
Mtoto ana miaka miwili na miezi sita
 
na una uhakika hajakuloga huyu?siamini km duniani kuna wanaume km ww,ndugu yangu, ww ndo unajua maana ya kupenda khaaaaa
 
Nina uhakila kabisa 100% hunywi bia, Ungekuwa unakunywa ungeliona hili mapema,.na hata muda huu ungekuwa umeshapata jibu Mapema..
Mm ushaur wangu, hebu anza kunywa bia, Halimashauri yako ya kichwa itakushaur nini ufanye
 
Back
Top Bottom