Nina kiasi cha shilingi million 7,500,000 itamaliza ujenzi wa vyumba 3

Duh matajiri hewa 😇😇😇
 
Pesa nyingi sana hiyo mkuu.
Hapo unaweza kujenga ghorofa na kufungua biashara kubwa tu.
Milioni 7,500,000 uliyonayo inakupa hadhi ya ubilionea mkuu,hongera sana!.
Uko sawa kabisa labda angesema mil 7.5 ila kwa hiyo mil 7,500,000 ni kubwa mno.
 
HELA inaweza ikatosha ama isitoshe kwakuwa hujatoa maelezo ya kutosha I'll ufanyiwe tathmini, maana mikoa inatofautiana kulingana na uhitaji ila kwa dar inatosha
 
inategemea na maeneo ambayo unataka kufanya hivyo mm naishi kisemvule mkuranga uku viwanja 1.5ml adi 2ml mchanga haununui hivyo unawewez kutumia 6ml umepata nyumba tena tofaur ukipiga mwenyew adi 5ml unatumia karibu kisemvule nikupatie kiwnja kwa bei poa
 
Hongera kwa makusanyo.
Wewe ni mbarikiwa.

Wasiliana na Uvimo kituo cha huduma cha huduma zote za ujenzi.

Itapigiwa gharama zote za ujenzi ikiwemo ramani na kujengewa mwanzo mwisho.


0629361896
0753927572 - What'sApp
 
Ndugu, ukisikiza ushauri wa wadau humu hutojenga miaka na mikaka.

Ukiwa kwenye group letu la UVIMO PUBLIC CENTER utajifunza namna ya kufanya maamzi mbalimbali yahusuo ujenzi.

Kutana na wataalam wetu ,magwiji wa ujenzi na washauri makini hutojuta.

Wapigie.
0629361896
0753927572 - What'sApp
View attachment 2000887View attachment 2000888View attachment 2000889View attachment 2000891View attachment 2000890View attachment 2000892View attachment 2000893
 
Hauwezi ngoja niondoe matofali tuangalie gharama za baadhi ya vifaa vichache tu.
1.Bati G30 120×24000= 2,880,000
2.Mchanga tripu 3×100,000= 300,000
3.Nondo Y12 36×26000= 936,000
4.Kokoto trip 1 × 300,000= 300,000
5.Mbao 2×4×12 167×7000=1,269,000
6.Mbao 2×2×12 160×3500= 560,000
????

Hauwezi kujenga kwa milioni saba acheni kupotosha
 

Wewe ndio unapotosha. Kwa kukariri.. hizo bati 120 zote za nini. Wakati nusu mgongo wa tembo bati zinalalia upande mmoja tu. Na bati 8 zinatosha chumba kimoja cha ft 11, na hata bei umeongopa.. bati gauge 30 - Alaf bando moja inayokuwa na pcs 16 inauzwa laki 3 tu. Na hivyo vyumba ni bati 24 tu zinamtosha,,Hata mbao umeongopa pia idadi. 4x2 na hata 2x2 zote ukichanganya pamoja za vyumba vitatu tu hazizidi laki 9 buguruni. Kokoto pia kwa staili niliyosema hapo lori dogo tu linatosha..

Una uongo mwingi sana yaani mchanga trip 3 za mende kwa ajili ya vyumba vitatu kamili tu?

Kaka mimi kujenga najenga kila mwaka. Ndio maana nimeeleza afanyeje ili itoshe
 
Shilingi million 7,500,000..... Hii Nchi hii... ndio mana Makonda alisema WATU WAKE NI TAJIRI SANA....
 
huwezi, sikukatishi tamaa, ila huwezi. niko kwenye ujenzi pia sasahivi mkoa fulani, nakushauri jipigepige ufike hata 25 au 30m.
Mimi najikita kwenye lugha tu. Kwenye kichwa cha habari ondoa neno 'million'. Maneno yanayobakia ndiyo sahihi kueleza uyatakayo. La sivyo, andika '...milioni saba unusu'; au kwa tarakimu '...milioni 7.5'.
 
Nyumba hutaweza mkuu, ila kibanda inawezekana.
 
Mkuu hapana

Kabisa mkuu
Naomba hivyo wapaswa una 18m +
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…