Uchaguzi 2020 Nina mashaka na idadi ya wapiga kura 2020

Chadema na ACT mtapigwa bao la mkono idadi ya wapiga kura ni uongo mtupu sio mil 29 ,halafu watu ambao hawajahakiki vitambulisho vyao vya kura na hata kama hawajabadili makazi wengi wameondolewa kwenye database ya wapiga kura na waliondolewa ni wale wenye mlengo wa upinzani kama una mlengo wa CCM na haujahakiki unaachwa kwenye database.
 
Vigezo walivyoweka wakati wa kuandikisha ndivyo vilileta watu wachache vituoni, kwa ufupi ni kuwa watu waliowengi vitambulisho vya kupigia kura wanavyo. Sio kila raia alitakiwa kwenda kujiandikisha, pitia vigezo vya NEC utapata jibu
 
TOHATO,
CCM walishatangaza hadharani kuwa watatawala milele!

Hivi unadhani kitu gani kinachowaaminisha hivyo, wakati wanajua kwa dhati kuwa unapoingia kwenye ushindani ni lazima ukubali kuwa kuna KUSHINDA na KUSHINDWA

Wanaamini kuwa Mkurugenzi wa uchaguzi, Dr Mahela, ambaye ni kada wa CCM, ni mtu wao, kwa hiyo kushinda ni LAZIMA!

Kwa hiyo Mkurugenzi huyo atafanya mbinu zote chafu na ovu, ili kulazimisha ushindi kwa CCM.

Mwaka huu hatutakubali, tumeshatangaza kuwa, tumeonewa kiasi cha kutosha, SASA BASI!

Hizo hila anazotaka kuzitumia huyo kada wao wa CCM,

Tunamtahadharisha tu kuwa mwaka huu, tunataka uchaguzi ulio HURU na wa HAKI, ama sivyo kwa kutumia hizo hila za kijinga, pengine wampe hifadhi kwenye "army barracks" ndiyo itakuwa salama yake!
 
Acha tusibiri tuone

Kwa mimi nitapiga kura katiba itakapo badilishwa.

Siezi jichafua kidole hali nafaham mkurugenzi, Kiongozi mkuu wa NEC anachaguliwa na ambae ni mgombea pia.. Simlaumu Raisi ila nalaumu Katiba yetu.

Hata ningekuwa mie lazima nitaweka watu wenye manufaa kwangu ambao naeza kaa nao tujue tuendeshaje huu uchaguzi.
 
Cdm munahofu kubwa sana ya kushindwa. Mwisho wa siku mutajikuta hata nyinyi wenyewe hapo ufipa hamuaminiani.
Kama unaona tume imekosea, lete wewe idadi yako iliyo sahihi.


Kwani lini Tanzania kulikuwa na Uchaguzi ??? HIzi ni chafuzi si chaguzi , na mwisho wake ni kudidimia kwa nchi kwani watu imefika mwisho. Hawawezi kuvumilia tena , tusubiri vita vya wenyewe kwa wenyewe tu. Sasa ni zamu yetu. CCM ndio wanatufikisha huko
 
Mkuu,

Hofu yako ni yetu tulio wengi.

Ni hivi:

1) Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imetangaza idadi ya wapiga kura waliojiandikisha (2020) kuwa ni 29,188,347 (Ref: Taarifa ya NEC, August 19, 2020)

2) Makadirio ya Idadi ya watu Tanzania hadi sasa (2020) ni milioni 59,700,000 na idadi hii imegawanyika kama ifuatavyo:-

a) Watu (wananchi) wenye umri chini ya miaka 15 ni zaidi ya 44.8%

b) Watu wenye umri kati ya miaka 15 hadi 64 ni 52%

c) Watu wenye umri zaidi ya miaka 64 ni 3%

Tufanye uchambuzi:

i) Wapiga kura (kwa mujibu wa Sheria ya Uchaguzi) ni miaka 18+

ii) Idadi ya wapiga kura (2020) waliotangazwa na NEC ni takriban 48.9%

iii) Kwa makadirio, idadi ya watu wasioruhusiwa kupiga kura kwa mujibu wa sheria (umri chini ya miaka 18 kutoka kundi 2(b) hapo juu) kuwa ni 1.1% ya wapiga kura wote

iv) Kwa hiyo, idadi ya wapiga kura kwenye uchaguzi wa 2020 ni 50% ya Watanzania wote. Hii ni sawa na watu 29,850,000

Uchambuzi huu hapo juu unamaanisha:

MOJA: Kwamba wakati wa kujiandikisha Watanzania WOTE walikuwepo hapa nchini na walijiandikisha kupiga kura kwenye uchaguzi mkuu 2020;

MBILI: Kwamba kila Mtanzania mwenye umri wa kupiga kura kwa mujibu wa sheria ya uchaguzi amejiandikisha kwenda kupiga kura

Nikiri, tangu Uchaguzi Mkuu wa kwanza katika Tanzania huru, Uchaguzi wa mwaka 2020 ndio utakuwa na maajabu kuwa asilimia mia moja (100%) ya Watanzania wenye umri wa kupiga kura walijiandikisha kupiga kura!

Serikali ya awamu ya 5 inatuona wapumbavu kiasi hiki?
 
Mpango mzima wa wizi wa matokeo huanzia kwenye;

1. Kuandaa idadi ya wapiga kura - lazima hapa data ziwe coocked ili kuja kuhalalisha uongezaji wa kura upande wa CCM bila kuzidi idadi ya waliojiandikisha.

2. Uwepo wa vituo hewa - hii hitumika zaidi katika maeneo CCM ilipo na nguvu. Lengo ni kuongeza kura zaidi za urais kupitia kisingizio cha kushinda ubunge. Mbinu hii hutumika sana kwenye maeneo wapinzani wasiopo na nguvu.

3. Utumaji wa matokeo NEC badala ya kutangaza matokeo ya Urais kila kitu - hii husaidia ku monitor mwenenndo mzima wa idadi ya kura wanazoachwa nyuma CCM ili kuona jinsi ya kutwist vitu na kuongeza kura kwa CCM kufidia na kuzidi zile za wapinzani.

4. Kuamua tu kutangaza kisichokuwepo - inaootoke kila njia ni ngumu, maandalizi ya kiulinzi na usalama huandaliwa ili kutangaza kwa nguvu kwa kutumia Sheria dhaifu ya matokeo ya urais kutohojiwa popote.

Sina hakika kama upindishaji wa matokeo utatoa matokeo Salama mwaka huu.

Huenda historia ikawekwa na mwiko ukavunjwa. Stay tune.
 
Uko sahihi mkuu, idadi waliyotutangazia ni maandalizi ya wizi wa kura. Uchaguzi mwaka huu ni batili. Magu hawezi kuruhusu uchagizi huru unaoweza kumuondoa madarakani
 

Hapa ndo maana suoni haja ya kupiga kura Aisee. Nishawahi sinuliwa na Rafiki yangu alisimamia uchaguzi uke wa marudi Wa SIHA inakatisha tamaa . ki ukweli ni kupoteza muda piga kura kama tume ndo hii
 
NEC iweke majina ,ya wapiga Kura walionao ambao ni 29+ kwenye tovuti Yao watanzania wayaone online. Idadi iliyowekwa sio sawa ni kubwa zaidi . NI sawa na kusema zaidi ya nusu ya watanzania wamejiandikisha Jambo ambalo sio kweli.Pia sio kweli kuwa watanzania wapo 50 m, watanzania ni pungufu ya 50m.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…